Je, kuna kuna mchekeshaji ambaye aliwahi kuchekesha na kukonga nyoyo za watu redioni kama Mzee Jangala?

Je, kuna kuna mchekeshaji ambaye aliwahi kuchekesha na kukonga nyoyo za watu redioni kama Mzee Jangala?

Akilihuru

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2022
Posts
1,512
Reaction score
2,980
Kwema wakuu, mishe zinaendeleaje,

Wakuu kwa wale wakongwe wa miaka ya 80s, bila shaka mtakuwa mnafahamu mchekeshaji huyu ambae alijizolea umaarufu mkubwa kutokana na fani yake ya uchekeshaji yani comedian.

Mzee Jangala alikuwa na timu yake ambayo ilisheheni watu waliokuwa wamebobea katika tasnia hiyo miaka hiyo kama vile mzee Kabunga, Mshamu na wengine wengi ambao nimewasahau.

Sehemu yake kubwa ambayo ilichekesha watu wengi kama sio Tanzania yote, ni kile kipande chake cha mahojiano yeye na mtoto wake (wa kuigiza) alieitwa mshamu. Mahojiano yalikuwa hivi 👇
Jangala: Mshamu hivi siku hizi unakwenda madrasa kweli?
Mshamu: Ndio baba, kwani vipi?

Jangala: kwa sababu nataka kujua unachokisoma huko madrasa.
Mshamu: ah hilo mbona halina shaka mdingi wangu.
Jangala: kweli eeh?
Mshamu: Yes father, tena siku hizi hata kizungu tunafunzwa madrasa.
Jangala anacheka kidogo 😂😂😂 afu anauliza.
Jangala: Sasa hivi uko sura gani?
Mshamu: Nipo ile ile sura ya siku zote uijuayo ya alkariatu. Kuna swali lingine?
Mzee Janganga anakuja juu 😂😂
Jangala: Sasa wewe wenzako kila siku wakienda madrasa wanabadilisha sura, ila wewe kila siku ni alkariatu yani ni kujikalia tu kujikalia tu mshen..z..i mkubwa 😂😂😂😂.
Anamtoa nduki Mshamu anatoka ndugu huku kisigino kinagusa chogo.

Aisee miaka ile tule enjoy sana, pamoja na kwamba nchi haikuwa katika wakati mzuri wa kiuchumi, lkn michezo ile ya Jangala iliwasaidia wengi kukumbuka shida wanazopitia kwa siku kutokana na hali ya maisha.

Anaejua alipo huyu mzee amfikishie salam zake, mwambieni wajukuu zake tunam miss sana. Na kama ashatangulia mbele ya haki basi Mungu ampe pumziko la milele amiin.
Dah enzi hizo Majuto bado yupo kwao Tanga huko hakuna hata anemfahamu.
 
Mi nakumbuka ile ya majuto anapika mama lishe akamwambia mkewe aweka hamira sijui ile kweny wali ili punje iwe kama kidole wapige faida...sasa Pale palikuwa Kuna mmakonde kama mteja akauliza "maharage yapo?"
Akaambiwa "we mmakonde usituletee kizaazaa"😂😂😂

Palikuwa kula wateja kibao akiwemo muhindi na mpemba baadae wakaanza kuumwa matumbo ...Kuna sehemu wanaingiza wanavyoharisha ila kwa sauti ya redio..😂😂😂
 
Hakuna aliyewahi kuvunja rekodi zao, yeye na akina kagunga, Pwagu na Pwaguzi na wengi wengineo.
Yan jamaa walikuwa vizuri sana kwa uchekeshaji. Ila sijui ilikuaje kuaje wakaishia njiani!!!
 
Mi nakumbuka ile ya majuto anapika mama lishe akamwambia mkewe aweka hamira sijui ile kweny wali ili punje iwe kama kidole wapige faida...sasa Pale palikuwa Kuna mmakonde kama mteja akauliza "maharage yapo?"
Akaambiwa "we mmakonde usituletee kizaazaa"😂😂😂

Palikuwa kula wateja kibao akiwemo muhindi na mpemba baadae wakaanza kuumwa matumbo ...Kuna sehemu wanaingiza wanavyoharisha ila kwa sauti ya redio..😂😂😂
Dah watu wametoka mbali sana, afu kina Joti walianza juzi wanakuja kuvuta mpunga mzuri wa kusavaivu kimaisha.
 
Asante kwa simulizi nzuri.

Ila Uzi bila picha ya Mzee jangala Haunogi.....!!!!!
Dah mkuu hiyo ilikuwa miaka ya 80s afu tulikuwa tunamsikia kwenye radio tu. Kwahiyo ki ukweli picha yake hata 1 sina mkuu.
 
Dah mkuu hiyo ilikuwa miaka ya 80s afu tulikuwa tunamsikia kwenye radio tu. Kwahiyo ki ukweli picha yake hata 1 sina mkuu.
Huyu hapa
images.jpeg
 
Hii picha ya mwaka gani mkuu? Hivi huyu mwamba bado yupo duniania na sisi au ashawafuata kina mzee Majuto, Small nk?
Mzee Jangala yupo Dar mpaka leo,kuna mahojiano yake ya hivi karibuni kipindi cha Mswahili kinachoendeshwa na Zembwela,niliona Youtube,nenda Youtube utaona hayo mahojiano Mkuu.
 
Kipindi cha mzee Jangala kilikua kinaanza na Wimbo wa mdhamini wa kipindi ambae ni pombe ya Chibuku,

"Tutumieee chibukuuu ni pombe boora...."
 
Back
Top Bottom