Je, kuna mkubwa anambania Mwakinyo?

Je, kuna mkubwa anambania Mwakinyo?

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Suala la kusema kuwa Rais wa WBO hajalipwa haiingii akilini maana mtu hawezi kutoka alipotoka hadi Tanzania kwa ajili ya mechi halafu awe hajalipwa.

Baadhi ya wadau walisema Hassan Mwakinyo ana-ugomvi na watu wengi kwa hiyo wanambania kwa kumfanyia figisu figisu kama hizi.

Je, unadhani ni nani ambaye anaendelea kumbania Mwakinyo hata baada ya kuwa sawa na Azam Media.

Ieleweke kuwa Mwakinyo wakati anapanda alijisahau akaanza kuwa na ugomvi na kila mdau wa ndondi, aliongea vibaya na kuwatendea vibaya baadhi ya watu. Mathalani aliwahi kuwashtaki Azam Media kwa kurusha ile mechi yake aliyosingizia viatu. Mwanasheria wake alimshauri vibaya maana pambano kurushwa hewani sio suala la bondia bali promota.

Hata hivyo kwa Azam kuikubali mechi ya Mwakinyo na Mghana ilikuwa tayari wameyamaliza, yaani Azam asingeweza kukubali kuharibu biashara yake.

Sasa tupeane za kupeana hapa, ni nani anayembania Mwakinyo?
 
Kuna kautapeli nakaona kwa huyu jamaa....pambano la tatu linayeyuka bila maelezo ya kueleweka
 
Kuna kautapeli nakaona kwa huyu jamaa....pambano la tatu linayeyuka bila maelezo ya kueleweka
Mwakinyo ana ujua ukweli, aliwakosoa watu fulani ni mwendo wa figisu.
Bongo hii inaonekana ukiwa expose kikundi fulani wanakufanyia namna uanguke, wakishindwa kukuangusha watakutafutia kesi
 
Mwakinyo ana ujua ukweli, aliwakosoa watu fulani ni mwendo wa figisu.
Bongo hii inaonekana ukiwa expose kikundi fulani wanakufanyia namna uanguke, wakishindwa kukuangusha watakutafutia kesi
Hii sio bongo tu, popote pale, usiwatukane wakongwe kwenye game bila hesabu. Watakunyamazia lakini watakunyoosha kwa vitendo.
 
Tatizo ni mwakinyo mwenyewe,kwasababu yeye ndiye mchezaji na mchezo anaoucheza kuna wizara,kuna vyama vya huo mchezo kuna mapromota,kuna wadau kibao.sasa inakuaje wote hao washindwe kunyoosha mamno yake kama kuna watu wanamhujumu.Kama jana umeona aliyeomba radhi ni mwakinyo wakati ile ilipaswa kua kazi ya promota aliyeandaa pambano na chama cha ngumi wasimamizi wa mchezo.kwahiyo utaona ubabaishaji ulipo.
 
Unauliza baridi mochwari kama ipo?

Ningekua mwakinyo ningebadilisha uraia

Hapa bongo wachawi na wakuda wengi sana ila yote sababu ya magnjwa ya akili kua mengi ambayo chanzo kikuu ni umaskini.
 
Back
Top Bottom