Je, kuna njia nyingine za kupata watoto mapacha ukiachana na kupandikiza maabara au kutokea tu naturally kama ambavyo tumezoea ?

Emery Paper

JF-Expert Member
Joined
Jun 1, 2019
Posts
1,427
Reaction score
2,728
Habari za wakati huu wanajukwaa!

Niende moja kwa moja kwenye mada. Ni hivi, katika siku za karibuni nimekuwa nikishuhudia ongezeko la idadi ya watoto mapacha kuzaliwa na hili ni kwa watu nnaowafahamu ndio wamehusika katika uumbaji huu.

Swali langu la msingi ambalo nataka kupata ufafanuzi kutoka kwenu madaktari na wataalamu wa afya, je ni kwamba kuna njia zinatumika kitaalamu ukiachana na hizo za kupandikiza sijui maabara au mapacha wanatokea tu naturally kama bahati ?
 
1. Genetics, kama umezaliwa pacha au mama/baba alikuwa pacha una nafasi kubwa ya kupata watoto mapacha

2. Ukiwa unatumia fertility treatment au dawa kuna nafasi kubwa ya zaidi ya yai moja kurutubishwa. Tatizo au faida ya fertility treatment ni kupata watoto quadruplet yaani wanne au zaidi.
 
Duh! Wanne kabisa. Hapo uzao mmoja unakuwa umemaliza kazi aisee.
 
Aiseee
 
Wanne kwa pamoja sio mchezo.
 
Wengine wanapata sita hadi nane hii fertility treatment ni mbolea kweli kweli.
Daaah hiyo hapana kwa kweli naona kama mwanamke atateseka sana kuanzia kuwabeba tumboni, wakizaliwa pia kunyonyesha watoto wanne sio mchezo. Achilia mbali namna ya kuwabeba hata kama atakuwa na wasaidizi wanne hawawezi kumsaidia kila kitu.

Mapacha wakizidi wawili ni jukumu zito kwa kina mama. Hata kama mwanaume cash ipo.
 
Wakiwa nane kwenye hospitali nyingine mama anapewa option wapunguzwe. Wengi wanakuwa na full bed rest mpaka wanajifungua.
 
Mhhh wanne hapana
 
Mmmmmmmhmn mambo ya kumpangia MUNGU uumbaji tutakuja leta watoto wasiokamilika.m au wenye madhaifu katika ukuaji.

Hivi vitu acha vije natural, unajua hivi viburi vya kujiamulia tunachotaka ipo siku tutaelewa kazi ya mikonk ya MUNGU baba....

Amina
 
Uwezekano upo naona wenzang wamewahi kukujibu kuna hizo dawa znazohusiana na fertilization
 
Nzuri..ila changamoto ni hapo kwenye malezi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…