Nakubaliana na hoja. Pia hii ni zao la uongozi mbovu kupita yote ya ccm tangu tupate uhuru.Hao Ndo mwanzo wa mdororo mkubwa wa kiuchumi hapa nchini pmj na viongozi wa serikalini......mbaya Zaidi wanatuaminisha kuwa nchi kuwa ya wachuuzi Ni bora Zaidi kuliko kuwa ya viwanda kisa wanakusanya kodi nyingi kutoka kwa wafanyabiashara
Nakubaliana Nawe kuwa hii Ni taasisi ya hovyo Sana sana
We tatizo hapa ni maamuzi ya matumizi ya pesa za kodi zetu kuvurugwa.ni kweli kuna changamoto ya umeme nchini na mara kadha wahusika wameshalielezea kwa kina jambo hili na mikakati inayotekelezwa kulikabili .
ni vizuri kuwa na subra na wastahimilivu. Ni vizuri zaidi kuwapa muda wa kitosha zaidi ili walishughulikie kwa uhakika zaidi ili kuondokana na kadhia hii ya kukatikatika kwa nishati hiyo muhimu nchini..
hayo mengine yabaki tu kama maoni na mtazamo utatuzi unakuja.🐒
Yawezekana hakuna!Bila shaka hakuna asiyejua madhara ya TANESCO, iwe mjini au kijijini, awe kiongozi au raia asiye na cheo, awe kijana au mzee, awe msomi au asiyeenda shule kabisa, awe mwenye kiwanda au mmiliki wa genge.
Ni takribani miaka 250 tangu Benjamin Franklin na Michael Faraday walipoweka kanuni jinsi umeme unavyozalishwa na unavyofanya kazi, lakini mpaka leo Tanzania haielewi chochote hata kwa vile vinavyoonekana kwa macho, kuhusiana na umeme. Uzalishaji wa umeme ni kati ya tekinolojia rahisi za kiwaida isiyohitaji elimu na tekinolojia ya pekee, lakini kwa Tanzania, hata kufunga tu wire au kuchomeka nguzo vizuri ya umeme ardhini ili isidondoke, inaonekana ni tekinolojia ngumu sana!!!
Mtanisahihisha, lakini kwa mtazamo wangu, TANESCO ni taasisi muhimu sana ambayo ubora au ubovu wake unagusa kila mahali katika maisha ya Mtanzania. Lakini kwa bahati mbaya sana, taasisi hii iliyo muhimu kabisa, bila shaka wamepewa watu wa hovyo kabisa, wenye uelewa duni kabisa, watu wazembe kabisa ambao upeo wao wa kuona mambo unaishia kwenye vidole vyao vya miguuni. Ukiwaona mitaani ya yale makoti yao unaweza kudhani wanafanya kazi, lakini kwa kiasi kikubwa wanazurura tu bila kuleta matokeo yoyote chanya.
Kuanzia Wizarani ambako kuna waziri, mpaka huko chini kwa wahandisi na mafundi, kote kumejaa watu waongo wanaotaka kuficha ubovu wao kwa kutengeneza hadithi za uwongo. Badala ya kutumia muda mwingi kufikiria namna ya kumaliza matatizo ya umeme, wao muda wote wanafikiria namna ya kutengeneza uwongo.
Miezi miwili iliyopita niitembelea vijiji 4 ambavyo vinatumia umeme kutoka kwenye mradi uliofadhiliwa na Kanisa Katoliki. Katika mwezi mzima, nilishuhudia umeme kukatika mara 2, na mara zote, haikuzidi nusu saa. Mradi huo unaendeshwa na wanakijiji wenyewe, na viongozi na watendaji wote wa mradi, hakuna mhandisi wala mfanyakazi yeyote mwenye hata degree moja. Lakini umeme ni wa uhakika.
Kwa aina ya watu waliopo wizara ya nishati mpaka hao waliopo TANESCO, nawahakikishieni, hata bwawa la Nyerere lianze kufanya kazi, hakuna kitakachobadilika. Maana tatizo kubwa halipo kwenye vyanzo vya umeme bali aina ya watu waliopo.
Muda huu ninaoandika, nimewasiliana na watu mbalimbali na kuthibitishiwa kuwa maeneo mengi ya nchi hakuna umeme.
Tujiulize, hivi watu waliyopo huko TANESCO wana uhalali gani wa kuendelea kuwatesa Watanzania kiasi hiki? Na mamlaka za juu, kwa nini zinaamua kuwatesa Watanzania kupitia TANESCO kwa kuwaweka watu ambao kwa kipimo chochote, hawafai na ni hasara kwa Taifa zima? Na sisi wananchi tutaendelea kuwavumilia hawa watu mpaka lini?
Kuna haja ya kuandaa maandamano makubwa dhidi ya TANESCO na watawala. Watawala muda huu ambao sehemu kubwa ya nchi ipo gizani, watawala wamewashiwa generators. Hawana giza.
We tatizo hapa ni maamuzi ya matumizi ya pesa za kodi zetu kuvurugwa.
Magu aliamua kurekebisha hii kitu (upatikanaji wa nishati ya umeme) ili kuimarisha uchumi, aliweza hili kwa kutoongeza misharara(mfano) ili baadae aongeze wakati huo bwawa la umeme liwe limekamilika. Asingekufa nauhakika kabla hajamaliza awamu zake angefaulu. Sasa dada yako kaingia kaona achote pesa akaongeze mishahara ili asifiwe, matatizo yalianzia hapo. Matokeo yake ndio haya mradi wa umeme unayumba mazima na kuua uchumi wa nchi. Nimetoa mfano 1 wa namna maamuzi ya ovyo yaliofanywa na awamu hii. Kukurupuka eti ndio unaleta cheo cha siasa serikakini kuwapoza watu wasipaze sauti. Nawaambieni Teuzi zozote dakika hizi za lala salama ni mbio za mfa maji. Ni sawa na timu ya mpira iliyofungwa gori 5 inaanza kuingiza wachezaji wapya dakika za majeruhi- kuna mambo yatazidi kuyumba kwa hizi pangua pngua hasa pesa zilipelekwa siko na plani ya mtangulizi wake. Hapa tunaongelea tanesco tu, kjuna nyingine zipo ambazo uhuni huu unafanyika, kubwa kuliko bandari ambayo madhara yake ni chini kwa chini sio kama hili ambalo maumivu yake ni papo kwa papo.
Mlinzi wa mipaka keshadokeza kuna wasiostahili wanatuamulia mambo, endeleeni kulala!
cc; chawa wote akiwepo lucas prove me wrong
Tatizo lipo kwa kiongozi mkuu. Yeye ndio anatakiwa awe na ujasiri wa kuminya kitufe kule juu bila kuogopa kilio cha ndugu flani ovyo hapa chini. Ndio mjue nani anastahiki kukaa pale.Yawezekana hakuna!
Tatizo 99% ya taasisi za serikali ziko HOVYO!
Kufanya kazi kwa mazoea..
Nidhamu, ukiritimba, uvivu, hawako creative katika uboreshaji wao wa kazi, hawataki mabadiliko ya aina yoyote kufanya kazi yao iwe rahisi na kumsaidia raia...
Sababu ya kutokuwa na performance review na targets basi wanaingia job na kutoka watakavyo, bila uwajibikaji wa aina yoyote ile!
They are just LUCKY PEOPLE KWA KULIPWA MISHAHARA BILA PRESSURE YA AINA YOYOTE ILE!
Umesoma upumbavu ulioandika lakini au umepost tu?Hiyo mitambo ni ya kisasa, ikihisi hatari inajizima, na haiwaki mpaka hatari iishe, watu wanataka iendelee kuwaka wamulike vitambi vyao walivyoshiba magimbi at the risk ya mitambo kuungua
Hiyo huwa ni sentensi ya kijinga sana.Uache kukumbuka ugali na nyamsa au kumkumbuka Yesu,umkumbuke kibaka?Rot in hell kibaka!Mtanikumbuka 😂
Rais wa awamu ya 2 aliwahi kusema,We tatizo hapa ni maamuzi ya matumizi ya pesa za kodi zetu kuvurugwa.
Magu aliamua kurekebisha hii kitu (upatikanaji wa nishati ya umeme) ili kuimarisha uchumi, aliweza hili kwa kutoongeza misharara(mfano) ili baadae aongeze wakati huo bwawa la umeme liwe limekamilika. Asingekufa nauhakika kabla hajamaliza awamu zake angefaulu. Sasa dada yako kaingia kaona achote pesa akaongeze mishahara ili asifiwe, matatizo yalianzia hapo. Matokeo yake ndio haya mradi wa umeme unayumba mazima na kuua uchumi wa nchi. Nimetoa mfano 1 wa namna maamuzi ya ovyo yaliofanywa na awamu hii. Kukurupuka eti ndio unaleta cheo cha siasa serikakini kuwapoza watu wasipaze sauti. Nawaambieni Teuzi zozote dakika hizi za lala salama ni mbio za mfa maji. Ni sawa na timu ya mpira iliyofungwa gori 5 inaanza kuingiza wachezaji wapya dakika za majeruhi- kuna mambo yatazidi kuyumba kwa hizi pangua pngua hasa pesa zilipelekwa siko na plani ya mtangulizi wake. Hapa tunaongelea tanesco tu, kjuna nyingine zipo ambazo uhuni huu unafanyika, kubwa kuliko bandari ambayo madhara yake ni chini kwa chini sio kama hili ambalo maumivu yake ni papo kwa papo.
Mlinzi wa mipaka keshadokeza kuna wasiostahili wanatuamulia mambo, sasa msitake tuongee ya uvunguni endeleeni kulala!
cc; chawa wote akiwepo lucas prove me wrong
Ni shirika au ofisi gani inayofanya kazi kwa ufanisi na weledi hapa nchini?Hili ndio shirika la hovyo kuliko mashirika yote
Hivi ni lini TANESCO walitoa sababu za kukosekana kwa umeme na wakasema matatizo hayo yataisha lini, halafu ikawa kama walivyosema?ni kweli kuna changamoto ya umeme nchini na mara kadha wahusika wameshalielezea kwa kina jambo hili na mikakati inayotekelezwa kulikabili .
ni vizuri kuwa na subra na wastahimilivu. Ni vizuri zaidi kuwapa muda wa kitosha zaidi ili walishughulikie kwa uhakika zaidi ili kuondokana na kadhia hii ya kukatikatika kwa nishati hiyo muhimu nchini..
hayo mengine yabaki tu kama maoni na mtazamo utatuzi unakuja.[emoji205]
kua mstahimilivu na mwenye subra hivi karibuni tu marekebisho yanayofanyiwa kazi yakikamilika changamoto hii itakua imeisha...Hivi ni lini TANESCO walitoa sababu za kukosekana kwa umeme na wakasema matatizo hayo yataisha lini, halafu ikawa kama walivyosema?
Sioni kama tatizo linashughulikiwa, labda useme kuna watu wanahangaika, kwa maana anayehangaika siyo lazima akuletee matokeo chanya.Rais wa awamu ya 2 aliwahi kusema,
namnukuu...
"Kila zama na kitabu chake"
maana yake kila jamii, jumuiya au familia ina utaratibu wake wakufanya mambo yake...
Huwezi tamani uwe na familia ya watoto 10 kama ya Fulani wakati ata kupata mtoto 1 huwezi kuzalisha [emoji205]
Relax,
Wizara ilishaeleza nini tatizo, Rais alishatoa maagizo na maelekezo kwenye hili, muhimu ni kuwa na subra,wastahimilivu na wangwana.
wakubwa zenu waliwaelekeza mfanye maandamano juzi hili hawakuliona la muhimu kwasabb wanajua linashughulikiwa....
kama umenena yote hayo ili kutoa dukuduku la moyoni na kupata relief, well and good nadhan uko sahihi kabisaaaa, big up sana [emoji205]
But issue inashughulikiwa na bilashaka unajua...