Je, kuna umuhimu muhimu wa Kuanzisha Jukwaa Tanzania Lenye Tofauti na Majukwaa ya Kimataifa Kama YouTube?

Je, kuna umuhimu muhimu wa Kuanzisha Jukwaa Tanzania Lenye Tofauti na Majukwaa ya Kimataifa Kama YouTube?

Davidmmarista

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2024
Posts
1,367
Reaction score
2,451
Kwa sasa, watengeneza maudhui wa Tanzania wamekuwa wakikabiliana na changamoto kadhaa zinazotokana na kutumia majukwaa ya kimataifa kama YouTube.

Mojawapo ya changamoto hizi ni sheria kali ambazo mara nyingi hazizingatii hali halisi ya soko la Tanzania na zinaweza kuwa kandamizi kwa wamiliki wa majukwaa. Vilevile, watengeneza maudhui wanapata malipo madogo sana ambayo hayalingani na jitihada na rasilimali wanazowekeza.

Aidha, kutegemea jukwaa moja bila kuwa na mbadala kunawaweka watengeneza maudhui katika hali ya hatari endapo jukwaa hilo litakutana na matatizo ya kiufundi au litapigwa marufuku. Kutokana na sababu hizi, kuna umuhimu mkubwa wa kuanzisha jukwaa la kiufundi ambalo litazingatia maslahi na mahitaji maalum ya watengeneza maudhui wa Tanzania.

Je unakubaliana na hili Tanzania tuwe na jukwaa letu wenyewe?
 
Kwahiyo unataka usolve hii changamoto ya malipo sio, kwamba unataka uwe unatulipa vizuri kuliko YouTube inavyotulipa.

Kwa kigezo hiki utafanikiwa coz watu hufanya content kwaajiri ya malipo Kwahiyo wakiona kuna jukwaa lingine la maudhui mfanano na YouTube linalipa kuliko YouTube basi watakuja.

Ila nadhani unatakiwa ufanye research yako vizuri kwenye huo upande wa malipo, unaweza ukahisi YouTube hawalipi vizuri coz ni Tanzania ila kumbe yawezekana shida ni traffic ya zone yetu haipo imara kama zilivyo zones zingine. Asante.
 
YouTube wanalipa vzr tu. Inategemea unatengeneza content za mna gani na zinaangaliwa wapi.

Kuna YouTuber mmoja wa hapa Tanzania anapata hadi dollar 2000 kwa mwezi.

Kuna yule Tayo Aina wa nigeria anapata hadi dollar 8000 kwa mwezi. Lakin angalia content zake zilivyotengezwa kwa ufasaha na quality ya hali ya huu, hapa Tanzania sijaona mtu mwenye content zenye quality kama hizo labda yule Malango sijui Bertin naona kidoogo wanajitahidi kuja vzr

Hardwork pays. Watu hawakai wakatulia wakatengeza content zilizotulia
 
YouTube wanalipa vzr tu. Inategemea unatengeneza content za mna gani na zinaangaliwa wap.
Kuna YouTuber mmoja wa hapa Tanzania anapata hadi dollar 2000 kwa mwezi...
Na niches pia, kuna niche ukizifanya unalipwa vizuri sana kwamfano za financial huwa malipo ni tofauti na zile za udaku na kadhalika.

Sema labda hiyo idea yake ya zile sheria yeye aje na zile sheria za awali kabisa zilizokua zinatumika kwamba sio lazima upate subscribers 1000 na views 1000 ndio uanze kulipwa bali ukipost video tu hata kama hauko na subscribers ila as long as video yako inapata engagement ya kutosha basi unalipwa. Then kama alivyosema kwenye kuboresha malipo basi atakua good challenger.
 
ila kumbe yawezekana shida ni traffic ya zone yetu haipo imara kama zilivyo zones zingine.
Sio kweli sababu upo Africa, Tanzania hio ndio sababu

Watu wanaambiwa walipwe kimataifa M12 per month Serikali inaingilia kati inasema wakilipwa hivyo watakua viburi walipwe 500k just imagine from 12 million to 500k
 
Kwahiyo unataka usolve hii changamoto ya malipo sio, kwamba unataka uwe unatulipa vizuri kuliko YouTube inavyotulipa...
Ila wangetakiwa watulipe vizuri mbona kwenye nchi zao wanalipa content creator wao vizuri mfano ukiweka matangazo ya adsense kwenye blog yenye maudhui ya kitanzania watembeleaji wakawa wa bongo basi malipo huwa ni kidogo sana ila kwa upande wa wenzetu wanalipwa vizuri hii inaonesha wazi kuwa Hawalipi content creators wetu vizuri.
 
Sio kweli sababu upo Africa, Tanzania hio ndio sababu

Watu wanaambiwa walipwe kimataifa M12 per month Serikali inaingilia kati inasema wakilipwa hivyo watakua viburi walipwe 500k just imagine from 12 million to 500k
Kwahiyo kumbe ni gavoo ndio inawabania watengeneza maudhui sio
 
Ila wangetakiwa watulipe vizuri mbona kwenye nchi zao wanalipa content creator wao vizuri mfano ukiweka matangazo ya adsense kwenye blog yenye maudhui ya kitanzania watembeleaji wakawa wa bongo basi malipo huwa ni kidogo sana ila kwa upande wa wenzetu wanalipwa vizuri hii inaonesha wazi kuwa Hawalipi content creators wetu vizuri.
Kwahiyo katika research yako unahisi shida ni nini?
 
Maana
Kwahiyo unataka usolve hii changamoto ya malipo sio, kwamba unataka uwe unatulipa vizuri kuliko YouTube inavyotulipa...
Kwa platform kama X(Twitter) inawalipa content creators vizuri sana pia wanasheria ambazo hazimkandamizi content creator kama Google pia telegram nayo inawalipa vizuri wamiliki wa Telegram Channel
 
Ila wangetakiwa watulipe vizuri mbona kwenye nchi zao wanalipa content creator wao vizuri mfano ukiweka matangazo ya adsense kwenye blog yenye maudhui ya kitanzania watembeleaji wakawa wa bongo basi malipo huwa ni kidogo sana ila kwa upande wa wenzetu wanalipwa vizuri hii inaonesha wazi kuwa Hawalipi content creators wetu vizuri.
Chanzo cha yote sio Google chanzo cha yote ni serekali yako ndio inaamua Wewe alipwe kiasi gani local local 1 viewer eti ni 0.0000009 USD serekali hii
 
Maana

Kwa platform kama X(Twitter) inawalipa content creators vizuri sana pia wanasheria ambazo hazimkandamizi content creator kama Google pia telegram nayo inawalipa vizuri wamiliki wa Telegram Channel
X wanalipaje na Telegram wanalipaje? Hapo sijagusa mtandao wa vichaa tiktok
 
Kwahiyo katika research yako unahisi shida ni nini?
Tunahitaji platform yetu ya kibongo ambayo tutashare na wenzetu jirani kama Kenya na nchi nyingine za Africa lengo ni kwamba content creators walipwe vizuri,tusiwe wategemezi na vya watu,njia nyepesi ya utoaji wa pesa na pia sheria zisizo mkandamiza content creator
 
X wanalipaje na Telegram wanalipaje? Hapo sijagusa mtandao wa vichaa tiktok
X ukisha verify account unaanza kulipwa na pia telegram unaomba matangazo nadhani alfu waki display matangazo kwenye channel yako mnagawana 50/50 na telegram
 
X ukisha verify account unaanza kulipwa na pia telegram unaomba matangazo nadhani alfu waki display matangazo kwenye channel yako mnagawana 50/50 na telegram
Hapo sawa na malipo wanapanga wenyewe maana naona Google wameshikwa Masikio unafanya kazi kubwa unalipwa kiduchu
 
Back
Top Bottom