Je kuna uwezekano wa seroconversion kutokea!?

prince22

Senior Member
Joined
May 8, 2015
Posts
188
Reaction score
217
Heshima kwenu wakuu, mwaka huu nimepitia mtihani mgumu mno na usioelezeka kirahisi, nilikutana na binti mmoja ambaye baada ya kufahamiana tukaanzisha mahusiano ya kimapenzi. Ilikuwa tarehe 21/06/2017 tulipokubaliana kufanya mapenzi tukitumia condom. Bahati mbaya tukiwa tunagegedana condom ikapasuka.

Baada ya condom kupasuka tukiwa tunagegedana nikamwambia tukapime akakubali alionyesha hofu lakn alijitahidi kuificha.

Tukaenda wote tulipopimwa tukatoka nje kusubiri majibu. Baada ya dakika 20 akaitwa na kuchukuliwa damu mara ya pili.

Muda wa kupewa majibu ukafika. Kweli bhana kumbe anaishi na maambukizi ya VVU.

Nikaeleza mbivu na mbichi nikapewa PEP(TLE). Nikazimeza kwa mwezi Mzima. Dawa zile ni kali mno, zinalevya mno na kuchosha. Ndoto za maruweruwe ya kutisha.

Nilipomaliza dawa nikaenda CTC pale Amana. Nikapima Nikaambiwa sina maambukizi. Nikakaa mwezi mmoja nikapima tena nikaambiwa sina.

Yule mwanamke huwezi kumdhania kabisa. Tena ni mnene na ana kalio la haja linaloweza kukudanganya. Kumbe ndani ameungua.

Leo ni siku ya 35 tokea nimalize dose ya pep. Lakn pia ni siku ya 65. Nimepima tena na majibu ni negative. Je kuna uwezekano kwa tukio hilo la mwezi sita na baada ya Pep, seroconversion ikatokea!? Sijawahi kufanya mapenzi tena tokea nipatwe na mkasa huo
 

Attachments

  • IMG_20170823_162649.jpg
    60.7 KB · Views: 92
  • IMG_20170823_162829.jpg
    133.5 KB · Views: 54
Mchimba kisima huingia mwenyewe
 
PEP uliyopewa ni mchanganyiko wa dawa ipi na ipi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…