Je, kupeana talaka ni hekima? Wanaotalakiana huangalia matokeo yake?

Je, kupeana talaka ni hekima? Wanaotalakiana huangalia matokeo yake?

Caroline Danzi

JF-Expert Member
Joined
Dec 19, 2008
Posts
3,713
Reaction score
1,265
Salaam great thinkers

Talaka zimekuwa gumzo/talk of town.

Kwa mtazamo wako, unahisi nini kinapelekea, watu waliopendana, wakaoana kwa hiari/utashi wao bila shuruti, wakaishi na kupata watoto, wanaamua kuachana kila mtu ashike hamsini zake?.

Sitaki kuhukumu, naamini kila mtu ana sababu muhimu inayomfanya afanye maamuzi ya kuachana.

Je unafikiri maamuzi haya yana hekima? Je kabla ya kuachana huwa tunaangalia matokeo ya kuachana kwetu? Hao watoto tunaweka kwenye hali gani? Familia hizi mbili zilizokuwa connected na wanandoa tunaziweka katika hali gani?


Nawasilisha.
 
Kuna sababu nyingi, lakini sababu kuu ni hii;
Ndoa nyingi hazidumu siku sababu wengi wanaofunga ndoa kabla ya hapo tayari walikuwa kwenye mahusiano na watu wengine. Matokeo yake ndoa zimekuwa hazina thamani.
Mfano, kama mtu alishawahi kuwa na ma-ex zaidi ya kumi na wote hao aliachana nao na kuoa au kuolewa na mwingine, unafikiri mtu wa aina hiyo atajua thamani ya ndoa?

Mtu kama huyo kwanza kishazoea kitendo cha kuacha au kuachwa, akiacha au kuachwa hasikii tena maumivu, kwake yeye ni kitendo cha kawaida sana. Hivyo ukioa au kuolewa na mtu wa namna hiyo, ikitokea mmekorofishana kidogo tu, hatua itakayofuata ni kuachana.

Na yote hiyo imesababishwa na mmomonyoko wa maadili ambao umechangiwa sana na utandawazi. Technolojia imefanya watu kuwa na viburi sana sababu mtu anaamini hata akiachana na wewe leo, siku chache zijazo atakuwa amepata mwingine wa kuishi naye, tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma.
Zamani watu walikuwa wanaogopa sana kuachwa hasa hasa Wanawake, lakini siku hizi Wanawake ndiyo wamekuwa majasiri wa kuacha na kuvunja ndoa zao. Kinachowapa ujasiri ni "utandawazi", mfano social media, Mkeo kasifiwa sana huko kwenye mitandao kuwa yeye ni mzuri, unafikiri mkizinguana hapo ndani atakuwa na muda wa kupoteza na wewe wakati kuna Wanaume elfu huko kwenye mitandao kila siku wanammendea?
 
Kuna sababu nyingi, lakini sababu kuu ni hii;
Ndoa nyingi hazidumu siku sababu wengi wanaofunga ndoa kabla ya hapo tayari walikuwa kwenye mahusiano na watu wengine. Matokeo yake ndoa zimekuwa hazina thamani.
Mfano, kama mtu alishawahi kuwa na ma-ex zaidi ya kumi na wote hao aliachana nao na kuoa au kuolewa na mwingine, unafikiri mtu wa aina hiyo atajua thamani ya ndoa?

Mtu kama huyo kwanza kishazoea kitendo cha kuacha au kuachwa, akiacha au kuachwa hasikii tena maumivu, kwake yeye ni kitendo cha kawaida sana. Hivyo ukioa au kuolewa na mtu wa namna hiyo, ikitokea mmekorofishana kidogo tu, hatua itakayofuata ni kuachana.

Na yote hiyo imesababishwa na mmomonyoko wa maadili ambao umechangiwa sana na utandawazi. Technolojia imefanya watu kuwa na viburi sana sababu mtu anaamini hata akiachana na wewe leo, siku chache zijazo atakuwa amepata mwingine wa kuishi naye, tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma.
Zamani watu walikuwa wanaogopa sana kuachwa hasa hasa Wanawake, lakini siku hizi Wanawake ndiyo wamekuwa majasiri wa kuacha na kuvunja ndoa zao. Kinachowapa ujasiri ni "utandawazi", mfano social media, Mkeo kasifiwa sana huko kwenye mitandao kuwa yeye ni mzuri, unafikiri mkizinguana hapo ndani atakuwa na muda wa kupoteza na wewe wakati kuna Wanaume elfu huko kwenye mitandao kila siku wanammendea?
Kweli usemalo mia mia...yaani ulishachezea mbususu kibao huko nyuma leo hii eti karatasi tuu ikubadilishe...nikujipa matumaini yasiokuwepo
 
Salaam great thinkers

Talaka zimekuwa gumzo/talk of town.

Kwa mtazamo wako, unahisi nini kinapelekea, watu waliopendana, wakaoana kwa hiari/utashi wao bila shuruti, wakaishi na kupata watoto, wanaamua kuachana kila mtu ashike hamsini zake?.

Sitaki kuhukumu, naamini kila mtu ana sababu muhimu inayomfanya afanye maamuzi ya kuachana.

Je unafikiri maamuzi haya yana hekima? Je kabla ya kuachana huwa tunaangalia matokeo ya kuachana kwetu? Hao watoto tunaweka kwenye hali gani? Familia hizi mbili zilizokuwa connected na wanandoa tunaziweka katika hali gani?


Nawasilisha.

Uamuzi wa kuachana huwa ni mbaya sana kwa wale ambao hawahusiki lakini huwa ni uamuzi wenye hisia nyingi sana kwa wale ambao wana achana na mara nyingi ukipewa nafasi ya kuwahoji unaweza kukubali kabisa hawa watu waachane na watakuwa salama kabisa wakiwa mbalimbali!

Kwakweli huwa ni vigu sana kuongelea sana viatu ambavyo hujavaa!

Mara nyingine uamuzi huonekana wa kikatili kwa sababu za watoto sio wahusika!
 
Kwa mtazamo wako, unahisi nini kinapelekea, watu waliopendana, wakaoana kwa hiari/utashi wao bila shuruti, wakaishi na kupata watoto, wanaamua kuachana kila mtu ashike hamsini zake?.

Jibu: 'Upendo' kunyauka, kupoa na hatimaye kufa
 
Kila kitu kina maana na faida kinapofanywa kwa ufasaha na kwa mda sahihi.
Kuna mda talaka inaweza kuwa ndio dawa ya kuwaponesha wale wanaowategemea au ndio ikawa sumu kwao.
 
Kila kitu kina maana na faida kinapofanywa kwa ufasaha na kwa mda sahihi.
Kuna mda talaka inaweza kuwa ndio dawa ya kuwaponesha wale wanaowategemea au ndio ikawa sumu kwao.
Ni kweli, kama magomvi yamefikia kufanyika mbele za watoto, matusi, na malumbano yasiyo na tija, ni vizirui kutengana kwa faida ya wanaowategemea.

Sasa unawaambiaje wale walioamua kuachana wakiwa na watoto? wafanye nini ili watoto waendelee kuupata huduma pande zote. Kuna ile tabia ya mzazi mmoja anajitoa ufahamu eti watoto wasiende kwa baba zao au wa watoto wasiende kwa mama zao?

NI vizuri tuanze kuwa na mkakati jenga hasa kwa hizi familia zilizoshindwa kuishi pamoja.
 
Kweli usemalo mia mia...yaani ulishachezea mbususu kibao huko nyuma leo hii eti karatasi tuu ikubadilishe...nikujipa matumaini yasiokuwepo

Maadili ndio chanzo cha maisha ya ndoa kuwa magumu. Tumeshindwa kutofautisha elimu na ndoa, hela na ndoa, urembo na ndoa, uhandasome-ndoa. Wadada/wakaka wengi tukiona wanaume wanatushobokea au wanawake wanatukimbilia basi unajua kila kitu kinawezekana.

Ukweli ni kwamba, kama umeolewa au kuoa, ukapoteza ndoa ya ujana wako, ukashindwa kujua tabia iliyopelekea kuachana/kushindwa, ni wazi kabisa kwamba huwezi kufanikiwa kwenye issue zinaitwa ndoa.
 
Jibu: 'Upendo' kunyauka, kupoa na hatimaye kufa
Natamani kujua, huu upendo unanyaukaje? Imagine, mmetongozana miaka 5, mmeona miaka mitatu mnaachana, inaleta picha gani? Kwamba miaka yote mitano mlikuwa mnavunga usakara??? Au kuna kitu kilikufanya umpende mwanamke/mwanaume, baada ya kuoa au kuolewa hukioni tena? Na kama hukioni kwa nini usilize kimeenda wapi ili akirudishe?
 
Ni kweli, kama magomvi yamefikia kufanyika mbele za watoto, matusi, na malumbano yasiyo na tija, ni vizirui kutengana kwa faida ya wanaowategemea.

Sasa unawaambiaje wale walioamua kuachana wakiwa na watoto? wafanye nini ili watoto waendelee kuupata huduma pande zote. Kuna ile tabia ya mzazi mmoja anajitoa ufahamu eti watoto wasiende kwa baba zao au wa watoto wasiende kwa mama zao?

NI vizuri tuanze kuwa na mkakati jenga hasa kwa hizi familia zilizoshindwa kuishi pamoja.
Hapa ndipo busara na hekima inatakiwa. Kwanza lazma mtambue kilichopelekea kitalakiana ni kitu gan na kina husiana vipi na malezi ya watoto wenu ndipo mchukue uwamuzi wakuweke watoto vikwazo ama la.
Mfano:- chanzo cha kuacha ikawa ni mwenza mmoja kuwa mlevi na malaya, hapa sizan kama itakuwa ni sawa kuwaruhusu watoto wawe wanaenda kukaa kwake kisa ni mzazi wao labda chakufanya ni kuweka utatatibu wa yeye kuja kuwaona watoto kwako ama njia nyingne ambayo haitowapa watoto nafas ya kuchukulia maovu yenu kama jambo la kikawaida tu
 
Hapa ndipo busara na hekima inatakiwa. Kwanza lazma mtambue kilichopelekea kitalakiana ni kitu gan na kina husiana vipi na malezi ya watoto wenu ndipo mchukue uwamuzi wakuweke watoto vikwazo ama la.
Mfano:- chanzo cha kuacha ikawa ni mwenza mmoja kuwa mlevi na malaya, hapa sizan kama itakuwa ni sawa kuwaruhusu watoto wawe wanaenda kukaa kwake kisa ni mzazi wao labda chakufanya ni kuweka utatatibu wa yeye kuja kuwaona watoto kwako ama njia nyingne ambayo haitowapa watoto nafas ya kuchukulia maovu yenu kama jambo la kikawaida tu
Naam, umenena vyema. vyovyote vile, kama wanakaa na mama basi baba arushusiwe kuja kusalimia na kushiriki kama baba na kama baba ndio anaishi na watoto basi mama arushusiwe kuwaona wanae. hiyo kidogo itapunguza ukakasi.
 
Bila hata kujua sababu....mie naunga mkono pale watu wanapoona wameshindwa kabisa kabisa kuishi pamoja kwa amani na kuamua kutalakiana. Ni muhimu kwa afya ya akili, hisia & mwili wa hiyo couple na watoto pia.

Kuna watoto wanakoseshwa sana raha kwa kuwa kati ya ugomvi na visirani vya wazazi wanaojilazimisha/lazimika kukaa pamoja. Mwisho wa siku hata ile "for the sake of the kids" inakuwa meaningless maana wanaishia kuteseka tu.
 
Bila hata kujua sababu....mie naunga mkono pale watu wanapoona wameshindwa kabisa kabisa kuishi pamoja kwa amani na kuamua kutalakiana. Ni muhimu kwa afya ya akili, hisia & mwili wa hiyo couple na watoto pia.

Kuna watoto wanakoseshwa sana raha kwa kuwa kati ya ugomvi na visirani vya wazazi wanaojilazimisha/lazimika kukaa pamoja. Mwisho wa siku hata ile "for the sake of the kids" inakuwa meaningless maana wanaishia kuteseka tu.
For the sake of the kids ni ujinga...unawezaje kuwapa wengine furaha wakati wee mwenyewe huna furaha
 
For the sake of the kids ni ujinga...unawezaje kuwapa wengine furaha wakati wee mwenyewe huna furaha
Ndo hapo sasa.🥴🥴

Mwishowe watoto wanaishia kuwa miserable as much as the parents 😐
 
Back
Top Bottom