Je "kuropoka" Kwa Mzee Yusufu Makamba kwenye Mkutano Mkuu wa CCM uliopita, kunaweza kuleta ukombozi Kwa Taifa letu?

Je "kuropoka" Kwa Mzee Yusufu Makamba kwenye Mkutano Mkuu wa CCM uliopita, kunaweza kuleta ukombozi Kwa Taifa letu?

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Mzee wetu Ysufu Makamba, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM alitoa kauli yenye ukakasi mkubwa Sana kwenye Mkutano Mkuu uliopita, kuwa eti viongozi wema huwa hawafi na akatolea mfano wa JK na Kinana, kuwa Bado wako hai hadi Leo, Kwa kuwa wamewatendea mema watanzania!

Ingawa kauli hiyo Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan alijaribu kuisahihisha Kwa kusema kuwa Mzee wetu Makamba alikuwa ameteleza ulimi Kwa kuyatamka maneno hayo.

Ni nahau nzito Sana na inabidi uitafakari Kwa makini Sana, Ili ujue Mzee wetu Makamba alimaanisha Nini katika kuyasema hayo maneno?

Hata hivyo Kwa kufanya tafsiri yangu ya namna nilivyoyaelewa maneno hayo ya vijembe, ni kuwa hata ule msiba mzito tulioupata kama Taifa mwaka Jana, ulitokana na "maamuzi" ya Mungu ya kutuondolea kiongozi wetu, kutokana na "maovu" yake mengi Sana, aliyowafanyia watanzania, hususani wapinzani wa nchi hii.

Nimesema kuwa maneno hayo yanaweza kuwa ni ukombozi Kwa Taifa letu.

Watu wengine wanaweza kuniuliza ni Kwa vipi maneno hayo yanaweza kuwa ni ukombozi Kwa Taifa letu?

Jibu ni rahisi tu, Kwa "nature" ya kibinafamu ni kuwa ingawa kifo tumeumbiwa sisi binadamu, hata vitabu vya dini zetu vinabainisha hayo.

Kwa mujibu wa maandiko kwenye Biblia yanasema, tuliumbwa Kwa mavumbi na tutarudi Kwa mavumbi na kwenye Quaran imeandikwa kuwa Kila nafsi itaonja umauti.

Kwa hiyo katika dini zote zimebainisha kuwa ni LAZIMA itafika siku sisi binadamu tutakufa.

Hata hivyo Kwa "nature" ya binadamu yeyote, anakiogopa kifo, Kwa hiyo Kwa "kuwakumbusha" viongozi wetu kuwa, watu wema ndiyo wenye maisha marefu hapa Duniani, kutawafanya viongozi wanaotutawala watende mambo mema na watende haki, wakati wa utawala wao, Ili waweze kuishi maisha marefu zaidi.

Kwa watawala wetu kututendea mambo mema watanzania, kama vile kuwa na utawala Bora, unaozingatia Sheria, kuzingatia usawa katika utawala wao, na siyo kuvinyanyasa vyama vya upinzani wakati vinatekeleza wajibu wao Kwa mujibu wa Sheria za nchi hii na kuepuka kufanya ufisadi, ndiko kunakoweza kuwa mwanzo wa kulikomboa Taifa letu.

Hongera Mzee Makamba Kwa kuyatamka hayo maneno hadharani

Mungu ibariki Tanzania
 
Si Wakristo Uraia wetu ni wa mbinguni duniani tunaipita tu by Askofu Gamanywa
Ni kweli alichotamka Askofu Gamanywa, kuwa sisi binadamu, siku za kuishi kwetu hapa Duniani siyo nyingi, na makazi yetu ya kudumu ni mbinguni, lakini "by nature" sisi binadamu tunatamani kuishi maisha marefu hapa Duniani
 
Bila kupepesa macho, kwa mujibu wa thread yako, upeo wako wa kufikiri upo chini sana. Ndo maana hukuelewa kwanini hadi Samia alijaribu kusema ulimi umemteleza Makamba. Hakuna binadamu mwenye akili timamu anaweza kuongea yale maneno. Ni mpaka nati ziwe zimelegea kichwani.
 
Bila kupepesa macho, kwa mujibu wa thread yako, upeo wako wa kufikiri upo chini sana. Ndo maana hukuelewa kwanini hadi Samia alijaribu kusema ulimi umemteleza Makamba. Hakuna binadamu mwenye akili timamu anaweza kuongea yale maneno. Ni mpaka nati ziwe zimelegea kichwani.
Ok. Ila kumbuka Kuna nati hulegea kwa sababu maalum....
 
Futa neno "kuropoka"!Mzee Makamba alitumwa na Mungu kuongea maneno mazuri.Atakayeshikwa na hasira ana lake jambo.Mwovu haishiwi hasira.
 
Bila kupepesa macho, kwa mujibu wa thread yako, upeo wako wa kufikiri upo chini sana. Ndo maana hukuelewa kwanini hadi Samia alijaribu kusema ulimi umemteleza Makamba. Hakuna binadamu mwenye akili timamu anaweza kuongea yale maneno. Ni mpaka nati ziwe zimelegea kichwani.
Weye ndiyo uwezo wako wa tafakuri upo below negatives nyingi.Makamba amepiga mumo kwa pale.Tafakari.
 
Bila kupepesa macho, kwa mujibu wa thread yako, upeo wako wa kufikiri upo chini sana. Ndo maana hukuelewa kwanini hadi Samia alijaribu kusema ulimi umemteleza Makamba. Hakuna binadamu mwenye akili timamu anaweza kuongea yale maneno. Ni mpaka nati ziwe zimelegea kichwani.
Mzee Makamba ana ugonjwa wa akili? Labda wampime milembe akithibitika tutamsamehe
 
Hii post nimechelewa sana kuisoma mana HAKUNA UMEME HUKU NI MGAO NAPOKAA au nayo makamba kazungumzia [emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom