Je, kutoa huduma za kifedha kwa njia ya simu kunahitaji Leseni?

nyumbamungu

JF-Expert Member
Joined
Mar 3, 2017
Posts
1,033
Reaction score
895
Wiki iliyopita nilikuta ubishi kati ya Maafisa wa leseni na Mfanyabiashara, ubishi ulikuwa mkubwa hadi kuwajaza wapitanjia na Wafanyabiashara majirani...

Duka nililokuta hayo mabishano linauza bidhaa mchanganyiko, viti, besini, ndoo za plastiki... subwoofer, deki, televisheni, ving'amuzi.... masufuria, sahani, mitungi ya gesi... ili kumrahisishia mteja aliweka laini za mitandao ya simu wateja wapate unafuu wakutoa pesa... nimetaja kwa ufupi ili mpate picha..

Mfanyabiashara alitakiwa awaonesha leseni ya Biashara kawaida, leseni ya TCRA, leseni ya EWURA, leseni ya BoT,

Kwa wenye kufahamu utaratibu wa Masharti, Kanuni, za utoaji leseni tunaomba kufahamishwa?

Juzi Mh Rais alivyokutana na Wachimbaji, Wauzaji na Wasafirishaji Madini aliagiza kodi Chechefu ziangaliwe upya au zifutwe....
 
Hilo duka lake lote la biashara ukiunganisha na huduma za pesa anatakiwa awe leseni moja tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…