Je, Kwa hili nitatiwa Hatiani? Naomba ushauri wa kisheria

SHIEKA

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
8,240
Reaction score
4,265
Eneo ninaloishi kuna vibaka wengi sana. Usiku wanaruka ukluta na kuingia uani mwangu na kuondoka na chochote wanachokikuta iwe ni kikombe, ndoo, beseni, nguo nk. Kuna nondo za ujenzi nimenunua na nataka kuzihifadhi uani. Kwa kuhofia udokozi wa vibaka, nataka niunganishe umeme kwenye hizo nondo ili mshenzi yeyote mwenye nia ya kuzidokoa anaswe au kushtuliwa na umeme.

Je, endapo kweli baada ya kuunganisha umeme kwenye nondo kibaka akanasa na kufa, nitakuwa hatiani?

Naomba jibu zuri linalozingatia sheria za nchi hii.
 
Jibu langu linaweza lisiwe zuri kisheria ,ila naamini lazima utoe taarifa kwa watu kuwa kuna umeme umeunganishwa na akishika ni hatari,
Japo namimi nawaza pia ,je kuna ulazima?
 
Jibu langu linaweza lisiwe zuri kisheria ,ila naamini lazima utoe taarifa kwa watu kuwa kuna umeme umeunganishwa na akishika ni hatari,
Japo namimi nawaza pia ,je kuna ulazima?

Halo Penguin-1 ukuta unaozunguka sehemu ya ua wangu ni tangazo tosha kwamba mtu asivuke na kwamba ni eneo faragha ambalo linatakiwa liheshimiwe. Kwa hiyo kwa maoni yangu, ninavyoona, mtu akiwa na nia ya kuchomoa nondo,' he is doing so at his own terrible risk! na hata akifa sina kosa!
 
Last edited by a moderator:
Angalia usije ukajitega mwenyewe au mmmoja wa wanafamilia wako (kama wapo)
 
Weka Tangazo kwamba Nyumba Hii inalindwa na Mitambo Mahalumu ya kuzuia wezi.
 
wewe kuwa makini na familia yako, mtu yeyoet atakayenasa atakuwa na hatia wala siyo wewe, ( kisheria kwenda kwenye eneo la mtu bila taarifa, na hasa usiku ni kosa) ingawa nia yako haijulikani.
My take angalia sana wanafamilia. hapo utawafanya vibaka wasije tena!!
wakatabahu
 
Mkuu nia yako ni nzuri lakini kwa uzoefu wangu mitego ya namna hii imeishia kuwaumiza wasio walengwa (ndugu/wanafamilia). Ukiamua kufanya hivyo tafadhali chukua tahadhari kubwa!
Mimi si mjuvi wa sheria, wakifikia wenyewe watatuelewesha.
 
Mimi si mwanasheria ila general best practise ni kuweka tahadhari mfano 'Usishike hapa kuna umeme'. Usipoweka mtu akinasa utakuwa na kesi ya kujibu. Ndo maana katika majengo kwenye ngazi wanakutahadharisha 'mind your steps'. Katika mabasi kama kuna kitu kitu unachoweza kujigonga kama vile tv wanaandika 'mind your head'. Kwenye ndege wakati wa kutelemka lazima watoe tahadhari wakati wa kuchukua mizigo. Pasipo tahadhali, mteja akidondokewa na mzigo ana haki ya kuwashtaki. Kuna nchi moja nilitembelea kule ulaya hata kikombe cha chai lazima kiandikwe tahadhali especially nyakati za baridi
 


Hasa! Na hiyo ndo nia yangu vibaka wakimbie kijiji ninamoishi!
 
Angalia usije ukajitega mwenyewe au mmmoja wa wanafamilia wako (kama wapo)

Wanafamilia wote nitawaeleza juu ya nia yangu na kuwatahadharisha. Usongo nilio nao ni wa vibaka tu. Nataka mmoja anase iwe fundisho kwa wenzake.
 
Lazima umweke notice kuwa kuna umeme, pia kama walivyosema watu wengine sana sana utawanasa ndugu zako hasa watoto pamoja na kuwapa tahadhari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…