Je, kwa nafasi yako wewe hili ungelifanyaje?

Je, kwa nafasi yako wewe hili ungelifanyaje?

Kipenzi Chao

Member
Joined
Oct 12, 2010
Posts
99
Reaction score
4
Ukiwa mwanaume, umeoa na umekuwa na mzunguko wa hapa na pale katika kutafuta mkate wa familia. Umebahtika kumpata mtoto wako mmoja....! Umekuwa ni wa dunia ya leo na hivyo ukawa mmepanga na mkeo kuweka interval fulani katika maamuzi ya kumtafutia mwana wenu mdogoye...! Lakini ukiwa safarini ukawa na tabia ya kuwasiliana na mkeo mara kwa mara, na katika mawasiliano hayo mkeo akakudokeza jambo lilikupelekea kuumia ilhali imekuwa vigumu kuamini; ya kuwa mama yako mzazi eti anamshauri mkeo abebe mimba without your concern....!!!

Uliporudi ulimuuliza mkeo vizuri kwa kuwa fikra za kwamba huenda mkeo anamsingizia mama yako jambo kama hilo, na akafafanua kwa undani. Nawe ukaamua kufanya uchunguzi wa kina, na hatimaye ukabaini ya kuwa ni kweli mama yako alipata kumshauri mkeo jambo kama hilo...!

SWALI:


  1. Ukiwa mwanaume utalishughulikiaje hilo swala?
  2. Ukiwa mke wa mtu, je, wewe ungechukua hatua ipi juu ya ushari wa mama mkwe?
  3. Ukiwa mzee, mwenye kulea ndoa ya wanao, ni nini hasa kinachowafanya wazee kuwa na tabia kama hii?
 
Ndoa ni ya watu wawili ukishaanza kuingiza mtu wa tatu tu kwisha habari yake
 
Ubaya ungekuwa abebe mimba ya mtu mwingine...

Wamama hupenda kupata wajukuu wengi wawaone kabla hawajafa...
 
ndoa ni ya watu wawili ukishaanza kuingiza mtu wa tatu tu kwisha habari yake


baadhi ya ndoa kutegemea na tamaduni
familly member wanahusika kwenye watoto,
waitwe majina gani,walelewe vipi,
 
Mjomba wangu mkewe alijifungua mm akili zikiwa zishaanza kujua baya na zuri. Babu akataka kumpa jina yule binamu yangu..... Uncle akamuuliza Babu, kwani yeye (Uncle) alipewa jina alilo nalo na nani? Babu akasema yeye mwenyewe (Babu) ndio alimpa hilo jina. Basi Uncle akasema niache na mimi nimpe jina maana ni wangu kama ulivyotumia nafasi yako kutupa majina.

Ingekuwa ni mm ningetumia maamuzi haya ya Uncle...........
 
baadhi ya ndoa kutegemea na tamaduni
familly member wanahusika kwenye watoto,
waitwe majina gani,walelewe vipi,

Baada ya watoto kuzaliwa sawa wanaweza kuchangia mawazo na kutoa mapendekezo.Ila sio kuwapangia wazae lini..wangapi kwasababu wenye ndoa ndo wanaojua kwanini wamepanga wanavyokua wamepanga.After all..wao ndo watakaokua responsible kwa hao watoto na sio ndugu wengine!
 
baada ya watoto kuzaliwa sawa wanaweza kuchangia mawazo na kutoa mapendekezo.ila sio kuwapangia wazae lini..wangapi kwasababu wenye ndoa ndo wanaojua kwanini wamepanga wanavyokua wamepanga.after all..wao ndo watakaokua responsible kwa hao watoto na sio ndugu wengine!

kweli but wazazi huwa hawaelewi
ukiwaambia huzai eti huna pesa...
Wao wanataka wajukuu wengi iwezekanavyo
 
Maamuzi ni ya watu wawili, wazazi wanapenda iwe hivyo lakini nyie ndio wahusika wakuu kwenye maisha yenu cha msingi ni kupanga kuendana na matakwa yenu
 
kweli but wazazi huwa hawaelewi
ukiwaambia huzai eti huna pesa...
Wao wanataka wajukuu wengi iwezekanavyo

Matokeo yake ikitokea wazazi wakafariki kundi la watoto linanyanyasika kwasababu hamna atakae wapokea...au wanchukuliwa kufanywa vijakazi!
 
Panga maisha yako kulingana na kipato chako na asitokee mtu wa kukusukuma kufanya maamuzi ambayo unakuwa huwa radhi nayo,mama atabaki katika nafasi yake ya umama na mpaka wake kwa familia yako unaishia hapo na si zaidi ya hapo.
 
Back
Top Bottom