Je, Mama Samia ataweza kuvaa viatu vya JPM kwa ukamilifu? Nafahamu ana washaauri lakini nasi tumshauri pale tunapoweza

Je, Mama Samia ataweza kuvaa viatu vya JPM kwa ukamilifu? Nafahamu ana washaauri lakini nasi tumshauri pale tunapoweza

Trust None

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2018
Posts
1,260
Reaction score
4,419
Tunafahamu JPM (R.I.P) alikuwa rais mwenye msimamo mkali na maamzi magumu. Swali hapa ni je, mama atafuata nyayo zake au atakuja na sera mpya?

Je, haya yafuatayo atayashughulikia vipi?

- Suala la wafanyabiashara kuhamishia biashara zao nchi za nje.

- Suala a ajira rasmi kwa wahitimu.

- Suala la bei za mazao na malipo kwa wakulima.

- Suala la nyongeza ya mishahara, kupanda madaraja na kubadilishiwa vyeo au muundo wa utumishi kwa waliojiendeleza kasomo.

- Manunuzi ya ndege zaidi na uendeshaji wake.

-Uhusiano wa CCM na vyama vingine vya siasa.

- Suala la KIKOKOTOO kwa wastaafu.

Karibuni tumshauri kiongozi wetu. Mimi naanza kumshauri auze 80% ya ndege za ATCL halafu pesa hiyo iboreshe usafiri wa reli nchini.
 
Back
Top Bottom