Uchaguzi 2020 Je, maoni ya wajumbe ni maoni wa wanachama wa CCM?

Uchaguzi 2020 Je, maoni ya wajumbe ni maoni wa wanachama wa CCM?

Loxodona

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2019
Posts
354
Reaction score
618
Hili ni swali linalofikirisha watu wengi sana kipindi hiki ambapo homa ya Uchaguzi inazidi kupambamoto. Swali hili linakuja baada ya wajumbe wengi wa CCM kuamua kwa maksudi kupuuza makatazo na maagizo ya chama na viongozi wake. Maeneo mengi nchini wajumbe wa CCM wakiwemo viongozi wa chama ngazi ya Wilaya wanalaumiwa Sana kwa kupiga kura zao kwa kuangalia nani kawapa rushwa nono na sio kwa mujibu wa sifa na uwezo wa wagombea na maoni ya Wanachama/wananchi wa kawaida.

Kwa muktadha huo, maeneo mengi, wanachama/wananchi wa kawaida wamewatupia lawama wajumbe kwa kupigia kura Watia Nia wasio na sifa wala uwezo wa kuwakilisha wananchi. Kwenye baadhi ya maeneo, wajumbe wamerudisha wagombea ambao walikuwa wanalalamikiwa Sana na wananchi kuwa ni wabunge/madiwani goigoi na wasio sifa wala uwezo wa kuwawakilisha vyema.

Wananchi/wanachama wa kawaida wanatamani Sana vikao vya juu vya chama viwaulize wananchi wa kawaida ni nani wanaona anafaa kuwa mgombea wao kwani maeneo mengi wananchi wa kawaida wamekatishwa tamaa na maamuzi ya wajumbe na hawakubaliani na kile walichokifanya wajumbe.

Kwa kuwa muda wa kuuliza wananchi/wanachama wa kawaida unaweza usitoshe; je,unashauri nini kifanyike ili CCM iweze kupata wagombea wenye mvuto, uwezo na sifa za kukabiliana kikamilifu na wagombea wa upinzani?
 
Wajumbe walijali maslahi yao binafsi.unakuta Jimbo Lina wapiga kura 50,000 na wanaccm zaidi ya 15,000 wajumbe ni 300 Tena wajumbe Wana umri wa miaka 56 Hadi 71 ndio wanapokea rushwa wanatoa mgombea.kundi kubwa la vijana hawakushiriki ujumbe Wala hawajui rushwa ni Nini matokeo yake wanachaguliwa mgombea .nani atampa Kura mgombea asiye na wapiga kura wengi October? CCM wameingia Chaka.

Huku vijijini mabalozi wa mashina ni wazee Tena no wachache kuliko vijana ndio wamepokea rushwa kuchafua wazee wenzao ili wapate diwani, October vijana ni wengi na wamejiandikisha kupiga Kura,watachagua kijana regardless of polical party.mchana mwema
 
WAKATE KUANZIA NAMBA MOJA HADI TANO (1-5) ! BAADA YA HAPO NDIO WAANZE MAAMUZI
 
WAK

WAKATE KUANZIA NAMBA MOJA HADI TANO (1-5) ! BAADA YA HAPO NDIO WAANZE MAAMUZI
Kwa kuwa CCM ilisambaza Vijana wake katika Majimbo yote kwa ajili ya kupata Taarifa, ni vema Taarifa hizo pamoja na maoni ya vyombo vingine juu ya nani anakubalika katika eneo Fulani yakazingatiwa hata ikitokea Mtia nia amepata kura chache apewe yeye ili kupata Chaguo la Kiongozi bora na Chaguo sahihi la Wananchi..,
 
Back
Top Bottom