Je, maridhiano ni CCM na CHADEMA au CCM na ACT Wazalendo?

Je, maridhiano ni CCM na CHADEMA au CCM na ACT Wazalendo?

USSR

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2015
Posts
10,904
Reaction score
26,184
Vita ya kugombea maridhiano imekuwa kubwa sana hapa Tanzania as if wananchi wanataka hayo maridhiano zaidi ya chakula.

Baada ya mbowe kufoka kule mwanza kwamba wao ndio vinara wa kupigania uhuru wa mikutano chini ya maridhiano alipoitwa Ikulu na Rais Samia jana ACT Wazalendo nao wameibuka na hoja ya kumpinga mbowe na kusema wao ndio waasisi wa maridhiano yaliyopelekea ruksa ya mikutano ya hadhara.

Hizi vita za kugombea maridhiano inaonesha tulivyo na wanasiasa wa hovyo hapa Tanzania,watu wazima na akili zao wanagombea nani aliambishwa asali akakubali kuwa sambamba na CCM.

Hii vita ya kupambana kati chadema na Act wazalendo utaifanya CCM ipite katikati kisha waje kusema wameibiwa kura.

USSR
 
Utata mtupu

Ndio sababu Shujaa Magufuli hakuukubali huu Upinzani wa Mchongo!
 
Back
Top Bottom