Je? Maziwa ya viwandani (ya pakiti) ni maziwa kweli?

ymollel

JF-Expert Member
Joined
Aug 23, 2012
Posts
3,096
Reaction score
2,287
Habari zenu,

Ni matumaini yangu mu wazima kimwili na kiakili. Nimepata mawazo sana kuhusiana na hili swala la maziwa ya viwandani ya kwenye pakiti kama vile brookside, azam, parmalat na mengineyo. Je, haya maziwa ni ya ng'ombe kweli au ni milk flavoured drink?

Je, yana virutubisho au hayana?

Je, tunapaswa kuyaita maziwa?

Je, tunapaswa kuyatumia kama mbadala wa maziwa ya ng'ombe?

Je, vipi kuhusu madhara ya matumizi yake endapo yana kemikali hatari?

Je, yana tofauti gani na maziwa ya unga?
 
Maziwa ni yang'ombe tu na ukiyata nenda kwa ng'ombe kwani huko viwandani wana weka kemiko za kutosha tu.
 
Yalikuwepo pale ubungo kiwanda kikafa.sasa haya yaliopo ni maji waliyobadili rangi.tbs wapo mbali nao.
 
Vipo viwanda ambavyo vina ranchi zao za kufugia ng'ombe kwa ajili ya hayo maziwa(mfano ASAS na Tanga Fresh) ambayo hupitishwa kiwandani na kuwekewa preservatives lakini ni hakika kua haya maziwa hayana bacteria yeyote sababu yamefanyiwa process inayoitwa pasteurization. ( Kitu ambacho hupati kwenye maziwa halisi).
Ila sio maziwa yote ni ng'ombe halisi mfano azam milk.
 


Asante sana mkuu,
 
ntarudi hapa baadaye kupata maelezo zaidi
 
Azam Milk ni maziwa ya unga ambao ni imported kutoka nje. Kwa uzoefu wangu maziwa mazuri ni yale yalikamuliwa kutoka kwa ngombe wa kienyeji directly. Haya unayachemsha na kunywa yakiwa bado fresh. Lakini ukiweka kwenye friji basi unayaharibu ata ladha inapotea. Na hii ni kwa vitu vyote. Ata samaki mzuri ni yule alitoka baharini mpaka jikoni.
 
Ahsante sana mkuu kwa ufafanuzi huu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…