Je, Mchungaji Kimaro anaweza kuanzisha Huduma yake bila kutoka KKKT kama alivyo Mwalimu Mwakasege?

Je, Mchungaji Kimaro anaweza kuanzisha Huduma yake bila kutoka KKKT kama alivyo Mwalimu Mwakasege?

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Nauliza tu kama hilo linawezekana kwa sababu mchungaji Dr Kimaro amekuwa ni hitaji la wanajamii wengi bila kujali madhehebu wala dini

Enendeni Duniani kote mkahubiri Injili kwa kila kiumbe Marko:16:15-18 hili ndio agizo kuu la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo

Mbarikiwe sana!
 
Nauliza tu kama hilo linawezekana kwa sababu mchungaji Dr Kimaro amekuwa ni hitaji la wanajamii wengi bila kujali madhehebu wala dini

Enendeni Duniani kote mkahubiri Injili kwa kila kiumbe Marko:16:15-18 hili ndio agizo kuu la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo

Mbarikiwe sana!
Hao wanatangaza injili Dar sio duniani
 
Nauliza tu kama hilo linawezekana kwa sababu mchungaji Dr Kimaro amekuwa ni hitaji la wanajamii wengi bila kujali madhehebu wala dini

Enendeni Duniani kote mkahubiri Injili kwa kila kiumbe Marko:16:15-18 hili ndio agizo kuu la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo

Mbarikiwe sana!
Mwakasege huyu huyu aliyeenda mbinguni na kurudi ?
 
Kama wachawi wanaenda kuzimu na kurudi, kuna ajabu gani kwa mtoto wa Mungu kwenda Mbinguni na kurudi?
Hivi Mbinguni unakuchukuliaje kwa mfano?.Unajua mijitu mieusi sisi ni mijinga sana tunamuamini mtu mazima na tupo tayari kudanganywa,Kwamba Mwakasege hana Mapungufu ya Kibinadamu?,Ikiwa anayo sasa huko mbinguni ataendaje na kisha kurudi ili hali imeshaandikwa kuwa "Kamwe hakuna kinyonge chochote kitakachoingia huko..."?!!Ufunuo 21:27.Jamani msilete mzaha na Mbinguni nyie.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
 
Hawezi, ndio maana aliomba msamaha akarudi Kanisani. Wale waandamanaji wasiojitambua sijui walienda wapi.
 
Mungu ana watoto?
Ndiyo. Kila binadamu aliyepo hapa duniani ana baba yake wa kiroho. Ni ama mtoto wa Mungu au wa Shetani.

Wote waliompokea Yesu ni watoto wa Mungu kama Yesu alivyo mtoto wa Mungu.

"Wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio Jina Lake".
Yohana 1:12
 
Hivi Mbinguni unakuchukuliaje kwa mfano?.Unajua mijitu mieusi sisi ni mijinga sana tunamuamini mtu mazima na tupo tayari kudanganywa,Kwamba Mwakasege hana Mapungufu ya Kibinadamu?,Ikiwa anayo sasa huko mbinguni ataendaje na kisha kurudi ili hali imeshaandikwa kuwa "Kamwe hakuna kinyonge chochote kitakachoingia huko..."?!!Ufunuo 21:27.Jamani msilete mzaha na Mbinguni nyie.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
Ni kweli ndugu. Ujinga ni mbaya sana, lakini si Sheria kuwa Mwafrika awe mjinga. Maadam unajua kusoma na kuandika, wekeza kila dakika yako utakayokuwa free kwa kusoma Biblia na vitabu mbalimbali. Uzuri mmoja mambo ya kiroho ni very practical. Usikubali tu kwa kuwa mtu kasema, naam, na usivikubali ikiwa havikubaliani na Neno la Mungu.

Kuna mengi yaliyoandikwa kwenye Biblia ambayo kama Wakristo wangeweza kuyaishi kama ilivyoandikwa, "wangeubadilisha" ulimwengu kwa dakika chache sana.

Na ni kweli Mbinguni hakitaingia kilicho kinyonge. Lakini ujue kuwa mtu aliyempokea Yesu Kristo si "kinyonge" tena, bali Mungu amtazamapo, anamwona kama amwonavyo Yesu.
~ "... Yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja Naye" 1Kor. 6:17

~ "... kama Yeye alivyo, ndivyo tulivyo na sisi ulimwenguni humu" 1Yohana 4:17

Unasemaje kwa habari ya Isaya?
Isaya 6:1-7

Na Paulo je?

"Namjua mtu mmoja katika Kristo, yapata miaka kumi na minne... Mtu huyo alinyakuliwa juu mpaka mbingu ya tatu. Nami namjua mtu huyo...ya kuwa alinyakuliwa mpaka Peponi, akasikia maneno yasiyotamkika, ambayo haijuzu mwanadamu ayanene." 2Kor. 12:2-4

Umeona hiyo? Paulo alifanyeje? Alinyakuliwa mpaka wapi? Mbingu ya tatu. Lakini usifikiri alinyakuliwa akiwa ndani ya mwili. Alitengana na mwili wake kwa muda.

Wasomi wa Biblia wanalihusisha hilo tukio na kipindi Paulo alipopigwa kwa mawe kisha akaachwa ikiaminika kuwa alishakufa, na inawezekana ndivyo ilivyokuwa. Lakini"waliomwua" walipoondoka, "akafufuka" na kusimama.

Mimi sikusikia alichosema mtumishi wa Mungu Mwl. Mwakasege. Lakini najua kuwa inawezekana mtu kutoka kwenye mwili wake, kwamba, roho yake ikaiacha mwili na kisha kusafiri mpaka eneo fulani na kisha kurejea kwenye mwili wake. Hata humu Jamii Forum kuna mada inayoongelea jinsi ya kutoka kwenye mwili. Sasa hiyo ni ya kibinadamu, na ni kinyume na Maandiko, ninaamini.

Lakini Mungu akitaka mtu aende Mbinguni au kwingineko kabla ya kufa, hawezi kushindwa kufanya hivyo. Hata Yohana alipokuwa kule kwenye kisiwa cha Patmo, alishaenda mpaka Mbinguni na kurudi. Hakuwa amekufa. Kilichoenda si mwili wake, bali roho yake.

Na ujue, mtu ni roho, na mwili wake ni makazi yake ya hapa duniani. Akifa, anauacha mwili na roho inaenda inakostahili. Ndicho kinachotokea mtu anapokufa. Roho yake hutengana na mwili wake.

Kwa hiyo, inawezekana Mwakasege alishapata experience kama hiyo ya mwili na roho kutengana kwa muda kwa kusudi maalum.
 
Ila Waafrika tunapigwa sana.Eehh?!,Huko mbinguni alikoenda na kurudi ilikuwa lini?.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
Mkuu, kwani mtu akisema kaenda Mbinguni au kuzimu na kurudi kutakugharimu nini?

Hakuna mtu anayejua kila kitu. Unaposikia kitu ambacho si cha kawaida kwako, usikimbilie kwenye hitimisho kuwa "haiwezekani". Badala yake, msikilize kwanza, halafu ukipata nafasi, mwulize maswali yatakayokusaidia kuelewa alichokisema.

Naupenda ushuhuda wa Kenneth Hagin kwenye kitabu cha I BELIEVE IN VISION. Anaeleza jinsi alivyotokewa na Yesu na akamfundisha somo la Imani.

Lakini kabla Yesu Hajaondoka kwake, alimwambia hatakubaliana na alichosema isipokuwa tu kama atampa Mistari mitatu ya Maandiko kutoka Agano Jipya yanayoliunga mkono hilo somo.

Yesu hakumkasirikia. Badala yake, alitabasamu na kumwambia atampa Mistari minne. Na akafanya hivyo.
 
Back
Top Bottom