Je, mechi ya kesho ndani ya Loftus Versfeld tutegemee sura zile zile zilizocheza first leg?

Je, mechi ya kesho ndani ya Loftus Versfeld tutegemee sura zile zile zilizocheza first leg?

vibertz

JF-Expert Member
Joined
Mar 15, 2022
Posts
2,474
Reaction score
4,726
Young Africans kesho watakuwa nchini Afrika kusini kurudiana na timu inayoogopewa kwa Afrika kwa ubora walionao sio wengine ni Mamelodi Sundowns. Kuelekea mechi ya kesho kocha wa Yanga amestua press kwa kuongea maneno yasiyotarajiwa na wengi.

Wengi walitegemea kuona Aucho, Yao na Pacome wangerejea kucheza hiyo mechi. Mamelodi wamekuwa ni moja ya timu yenye bahati kwa kujipima na Yanga bila ya utimamu wa kikosi chao kamili (first eleven) kwa maneno ya kocha huenda kwenye mechi ya kesho wakacheza wale wale au akaingizwa mchezaji mmoja tu katika wale waliokuwa na majeruhi.

"Tunasubiri kuona itakavyokuwa leo kwenye mazoezi ya mwisho, tunaweza kumpata mchezaji katika wale waliokuwa majeruhi.

Ni kweli tunaiwaza nusu fainali ya CAF lakini tunajali pia na usalama wa afya za wachezaji wetu pia. Young Africans haichezi mashindano haya peke yake" Miguel Gamondi
 
Screenshot_20240404_182049_X.jpg
kama kuna hata mmoja atacheza basi ni aucho,
Yao na Pacome hata kwenye mazoezi ya leo hawajapost..., tofauti ya mechi ya juzi na kesho ni kua ya kesho lazima kupatikane goli.
 
View attachment 2953858kama kuna hata mmoja atacheza basi ni aucho,
Yao na Pacome hata kwenye mazoezi ya leo hawajapost..., tofauti ya mechi ya juzi na kesho ni kua ya kesho lazima kupatikane goli.
Dah na mechi iliyopita tatizo ilikuwa kwenye umaliziaji wa nafasi, na mechi ya kesho inahitaji magoli. Dah ngoma imeshakuwa ngumu
 
Kikosi kicheze kilekile kama kuna harihati ya baadhi ya wachezaji kuwa majeruhi. Kama nafasi tulitengeneza nyingi tu kikubwa ni matumizi sahihi ya hizo nafasi basi
 
Young Africans kesho watakuwa nchini Afrika kusini kurudiana na timu inayoogopewa kwa Afrika kwa ubora walionao sio wengine ni Mamelodi Sundowns. Kuelekea mechi ya kesho kocha wa Yanga amestua press kwa kuongea maneno yasiyotarajiwa na wengi.

Wengi walitegemea kuona Aucho, Yao na Pacome wangerejea kucheza hiyo mechi. Mamelodi wamekuwa ni moja ya timu yenye bahati kwa kujipima na Yanga bila ya utimamu wa kikosi chao kamili (first eleven) kwa maneno ya kocha huenda kwenye mechi ya kesho wakacheza wale wale au akaingizwa mchezaji mmoja tu katika wale waliokuwa na majeruhi.

"Tunasubiri kuona itakavyokuwa leo kwenye mazoezi ya mwisho, tunaweza kumpata mchezaji katika wale waliokuwa majeruhi.

Ni kweli tunaiwaza nusu fainali ya CAF lakini tunajali pia na usalama wa afya za wachezaji wetu pia. Young Africans haichezi mashindano haya peke yake" Miguel Gamondi
Yuko sahihi mchezo Hui utakuwa wa kasi Sana mchezaji goigoi hatauweza
 
Hivi wakuu ni Channel gani Dstv chanel number ngapi itaonyesha CAF champions League?
 
Back
Top Bottom