Tetesi: Je, mifumo ya Mamlaka ya Mapato (TRA) inachezewa?

Tetesi: Je, mifumo ya Mamlaka ya Mapato (TRA) inachezewa?

CWR2016

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2017
Posts
2,773
Reaction score
6,349
Habari Watanzania,

Katika miezi kadhaa sasa, kuna jambo limekuwa likijirudia sana.

Jambo hili ni ZITO sana na wala si la kuchukulia mzaha hata kidogo.

Jambo lenyewe ni hili:
Mfumo wa TRA, hasa TANCIS ambao ndio unaotumiwa na Idara ya Forodha (Customs) kukusanya Mapato ya bidhaa zinazoingizwa nchini, umekuwa ukifanya kazi either nusu, au kuzima kabisa kwa muda.

Mfano tangu jana tarehe 09/09/2022, saa tano (saa 5:00 usiku) usiku, mpaka sasa muda huu saa 12 jioni tarehe 10/09/2022, mfumo huo wa TANCIS umesimama kutoa Control Number za kulipia ushuru/maduhuri ya serikali.

Ifahamike kwamba kusimama kwa mfumo kutoa hizo Control Number, hakuna malipo yanayoweza kufanyika.

Nisingeandika jambo zito kama hili kama lingekuwa limejitokeza mara moja.

Wanaoweza kufuatilia zaidi, wajiridhishe.
Hii hutokea karibu kila wiki, inaweza kuwa siku moja, au masaa kadhaa ya siku flani.

Sisi wateja tunapata changamoto sana.

SWALI LA MSINGI NI HILI;

Je, wakati mfumo unasinzia kufanya kazi kitu flani, ni nini huwa kinaendelea huko ndani?

Je, baada ya mfumo kurejea, tuna uhakika gani kwamba malipo kadhaa hayajachezewa?

Na kwa nini itokee kila wiki, au mara mbili kwa mwezi? Ni kina nani wanufaika wa hili jambo zito hivi?!

Asante.
 
Wakisha zima wanalipia manual, alafu hawapeleki malipo kama yalivyolipwa bank system ikirejea, Mh. Waziri Mkuu alilisema sana hili na akalikemea kwa ukali, kama miezi 3 hv iliyopita, naomba serikali ikiwa kuna mtu au kikundi cha watu wanafanya huu uhuni na wizi mbaya sana iwakamate kuwafungulia mashtaka na kuwanyonga kabisa hadi wafe. Huu ni uhujumu uchumi na ufisadi mbaya sana sana kuliko wowote ule.
 
Wakisha zima wanalipia manual, alafu hawapeleki malipo kama yalivyolipwa bank system ikirejea, Mh. Waziri Mkuu alilisema sana hili na akalikemea kwa ukali, kama miezi 3 hv iliyopita, naomba serikali ikiwa kuna mtu au kikundi cha watu wanafanya huu uhuni na wizi mbaya sana iwakamate kuwafungulia mashtaka na kuwanyonga kabisa hadi wafe. Huu ni uhujumu uchumi na ufisadi mbaya sana sana kuliko wowote ule.
Tuko kwenye nchi ambayo lolote linawezekana. Na dawa hatujaijua bado.
 
Sasa tusipozimazima system mapema ili mzoee tutalipiaje manually mabasi kumi kati ya yale 60 yaliyoagizwa na Mpakwa mafuta Migulubaja Chemba!!
 
Sasa tusipozimazima system mapema ili mzoee tutalipiaje manually mabasi kumi kati ya yale 60 yaliyoagizwa na Mpakwa mafuta Migulubaja Chemba!!
Naomba hiyo System ya kulipia huduma mannually mzee, mfano nataka kulipia ushuru wa gari nafanyaje kulipia kwa mannually?? Na kama ipo hiyo Option kwann ulalamikie mfumo haufanyi kazi?? Si una uhakika unaweza kulipua mannually na mamba yakawa fresh tu??
 
Kwa Tanzania hupaswi kushangaa kuhusiana na huduma mbovu, hiyo ni jadi yetu.

Ukipewa huduma nzuri ndio unapaswa kujiuliza kama kweli unastahili au kuna jambo nyuma yake.
 
Eleza wewe kinachoendelea mbona unazunguka mzee, we si unajua? Eleza hapa watu wajue sasa. Huna unalojua kilaza wewe, unakaa kuweka lawama na akili za kijinga kudhani watu wanaiibia serikali.
Basi kama hujui, hakuna hiyo loophole ya kulipia mannually, acha chuki za kijinga kwa taasisi fulani kisa njaa zako.

Nakupa Mfano, unaweza kuprint leseni ya gari ya Mtu bila kulipia pesa??

Unawezaje kutoka Gari kwenye mfumo bila kulipia pesa au hujui unalozungumza??

Acha kujaza mashudu humu jukwaani.
CARDLESS hunifahamu.
Nina elimu ya mambo haya kuliko unavyofikiri.
Pili sina njaa hizo unazofikiri.
Tatu usitoe mifano ya importation za magari.
Naelewa nachokisema, nimeandika kwa ufupi ili wabobezi wachimbe ndani kutunza kumbukumbu.

Hazitafanyiwa kazi sasa. Zitatunzwa kwa kazi za baadae, miaka ijayo .
 
Back
Top Bottom