OLS
JF-Expert Member
- Oct 12, 2019
- 426
- 685
Ili kupunguza tatizo la ajira nchini, serikali kupitia Halmashauri zote nchini na Mfuko wa Rais, wanatoa mikopo isiyo na riba kwa vijana, wanawake na walemavu
Halmashauri zinatoa asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kwa vijana, wanawake na walemavu, ikiwa ni asilia 4, wanawake, asilimia 4 vijana na asilimia 2 walemavu
Masharti sina shaka nayo kwa sababu kwa namna moja au nyingine yanafanana na taasisi nyingine za mikopo.
Mfuko wa Rais (PTF) pia unatoa mikopo kwa vijana, ila hawa wamelenga zaidi kwa vijana wanaotoka VETA.
Hii yote ni kupunguza tatizo la ajira nchini, lakini naona vijana na wanawake wana ufahamu zaidi kuhusu mikopo inayotolewa na FINCA, PRIDE, nk. Mikopo ambayo imekuwa mwiba kwa watu wengi kwa kuwa na riba kubwa na muda mdogo wa kurudisha mikopo hiyo
Pia watu wamepoteza vitu vyao kwa kujihusisha na mikopo hiyo. Lakini ikumbukwe serikali inasisitiza vijana wajiajiri, lakini nawaona hawafanyi marketing kiasi cha kutosha ili vijana waweze kujiajiri
Soon nitakuja na suggestion ya kitu gani kibadilishe kwenye mikopo hiyo ili kuwafiki wengi na kuwa na tija kwa vijana walio wengi ambao wana mawazo ya biashara lakini, hawana mitaji ya kuweza kujiajiri
Lakini watu wengi wamekuwa wakitafuta mikopo katika mashirika binafsi yenye riba kubwa, ambayo hata ukusanyaji wake umewafanya watu hao kuwa masikini zaidi kama tafiti mbalimbali zinavyoonyesha
Biashara matangazo, serikali sio kama inafanya biashara lakini kama ina nia ya kuwaokoa vijana na wanawake kwenye mambo ya kujiajiri inaonyesha wazi utangaziji wao hauko sawa na mashirika binafsi ya kutoa mikopo
Halmashauri zinatoa asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kwa vijana, wanawake na walemavu, ikiwa ni asilia 4, wanawake, asilimia 4 vijana na asilimia 2 walemavu
Masharti sina shaka nayo kwa sababu kwa namna moja au nyingine yanafanana na taasisi nyingine za mikopo.
Mfuko wa Rais (PTF) pia unatoa mikopo kwa vijana, ila hawa wamelenga zaidi kwa vijana wanaotoka VETA.
Hii yote ni kupunguza tatizo la ajira nchini, lakini naona vijana na wanawake wana ufahamu zaidi kuhusu mikopo inayotolewa na FINCA, PRIDE, nk. Mikopo ambayo imekuwa mwiba kwa watu wengi kwa kuwa na riba kubwa na muda mdogo wa kurudisha mikopo hiyo
Pia watu wamepoteza vitu vyao kwa kujihusisha na mikopo hiyo. Lakini ikumbukwe serikali inasisitiza vijana wajiajiri, lakini nawaona hawafanyi marketing kiasi cha kutosha ili vijana waweze kujiajiri
Soon nitakuja na suggestion ya kitu gani kibadilishe kwenye mikopo hiyo ili kuwafiki wengi na kuwa na tija kwa vijana walio wengi ambao wana mawazo ya biashara lakini, hawana mitaji ya kuweza kujiajiri
Lakini watu wengi wamekuwa wakitafuta mikopo katika mashirika binafsi yenye riba kubwa, ambayo hata ukusanyaji wake umewafanya watu hao kuwa masikini zaidi kama tafiti mbalimbali zinavyoonyesha
Biashara matangazo, serikali sio kama inafanya biashara lakini kama ina nia ya kuwaokoa vijana na wanawake kwenye mambo ya kujiajiri inaonyesha wazi utangaziji wao hauko sawa na mashirika binafsi ya kutoa mikopo