Je, mikopo isiyo na riba ya serikali inatangazwa kiwango cha kutosha?

Je, mikopo isiyo na riba ya serikali inatangazwa kiwango cha kutosha?

OLS

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2019
Posts
426
Reaction score
685
Ili kupunguza tatizo la ajira nchini, serikali kupitia Halmashauri zote nchini na Mfuko wa Rais, wanatoa mikopo isiyo na riba kwa vijana, wanawake na walemavu

Halmashauri zinatoa asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kwa vijana, wanawake na walemavu, ikiwa ni asilia 4, wanawake, asilimia 4 vijana na asilimia 2 walemavu

Masharti sina shaka nayo kwa sababu kwa namna moja au nyingine yanafanana na taasisi nyingine za mikopo.

Mfuko wa Rais (PTF) pia unatoa mikopo kwa vijana, ila hawa wamelenga zaidi kwa vijana wanaotoka VETA.

Hii yote ni kupunguza tatizo la ajira nchini, lakini naona vijana na wanawake wana ufahamu zaidi kuhusu mikopo inayotolewa na FINCA, PRIDE, nk. Mikopo ambayo imekuwa mwiba kwa watu wengi kwa kuwa na riba kubwa na muda mdogo wa kurudisha mikopo hiyo

Pia watu wamepoteza vitu vyao kwa kujihusisha na mikopo hiyo. Lakini ikumbukwe serikali inasisitiza vijana wajiajiri, lakini nawaona hawafanyi marketing kiasi cha kutosha ili vijana waweze kujiajiri

Soon nitakuja na suggestion ya kitu gani kibadilishe kwenye mikopo hiyo ili kuwafiki wengi na kuwa na tija kwa vijana walio wengi ambao wana mawazo ya biashara lakini, hawana mitaji ya kuweza kujiajiri

Lakini watu wengi wamekuwa wakitafuta mikopo katika mashirika binafsi yenye riba kubwa, ambayo hata ukusanyaji wake umewafanya watu hao kuwa masikini zaidi kama tafiti mbalimbali zinavyoonyesha

Biashara matangazo, serikali sio kama inafanya biashara lakini kama ina nia ya kuwaokoa vijana na wanawake kwenye mambo ya kujiajiri inaonyesha wazi utangaziji wao hauko sawa na mashirika binafsi ya kutoa mikopo
 
Nimekuja likizo kijijini nawaeleza uko Halmashauri Kuna pesa za bwelele kwanza ata ukikopa ukachelewa kurudisha Halmashauri hawadai Kama finca au benki mkopo wanakwambia ulejeshwe ndani ya mwaka mmoja Ila kikundi kinaweza tumia ata miaka mitatu bila kubuguziwa zana wakati mwingine kikundi kisirejeshe kabisa na Halmashauri inakosa Cha kuwafanya.

Kiufupi mm nimeisha zitumia Sana ingawaje mm najitaidi kurejesha kwa wakati hvyo kujenga uwaminifu wa kikundi kupewa pesa nyingi zaidi pindi unapoomba Tena.
 
Jambo la muhimu andaa kikundi Cha watu wasiopungua watano wanaweza kuwa wanawake kwa wanaume au wanawake tu au wanaume tu.

Pili Andi muhutasari wa kikundi kwamba wanachama wamelizia kusajili kikundi Chao

Akikisha kikundi kina katiba ikionyesha idadi ya wanachama, eneo wanapofanyia shughuli zao, uongozi kuanzia mwenyekiti na katibu, namba za simu za viongozi na mengine.

Andika barua ya kuomba kusajiliwa kwa kikundi kwenda kwa mkurugenzi wa Halmashauri usika Ila kupitia kwa mtendaji wa kata usika ili athibitishe uwepo wa icho kikundi usika.

Baada ya kukamilisha hzo nyaraka zote Yani katiba ya kikundi, muhutasari wa kikao Cha wanakikundi wakipendekeza kusajili kikundi Chao pamoja na barua ya kuomba usajili wa kikundi nenda Halmashauri ofisi ya maendeleo ya jamii ukiwa na hzo nyaraka watakupa kimemo uende kilipia elfu kumi Kama sio ishirini kwenye ofisi ya muhasibu mapato ukisha lipiwa nakupewa risti utaludi Tena ofisi ya maendeleo jamii ukiwa na hyo risti uliyo lipia then watakupa hati ha usajili wa kikundi.

Ukisha sajili kikundi Sasa unaweza kuomba mkopo kwa kumuandikia mkurugenzi wa Wilaya barua ya kuomba mkopo ikitaja kiasi na namba ya utambulisho au usajili wa kikundi ambatanisha pia muhutasari wa kikundi wa kinuia kuomba mkopo pamoja na katiba ya kikundi Kisha zipeleke masijala ya mkurugenzi wa wilaya alafu utasubili majibu.
 
Jambo la muhimu andaa kikundi Cha watu wasiopungua watano wanaweza kuwa wanawake kwa wanaume au wanawake tu au wanaume tu.

Pili Andi muhutasari wa kikundi kwamba wanachama wamelizia kusajili kikundi Chao

Akikisha kikundi kina katiba ikionyesha idadi ya wanachama, eneo wanapofanyia shughuli zao, uongozi kuanzia mwenyekiti na katibu, namba za simu za viongozi na mengine.

Andika barua ya kuomba kusajiliwa kwa kikundi kwenda kwa mkurugenzi wa Halmashauri usika Ila kupitia kwa mtendaji wa kata usika ili athibitishe uwepo wa icho kikundi usika.

Baada ya kukamilisha hzo nyaraka zote Yani katiba ya kikundi, muhutasari wa kikao Cha wanakikundi wakipendekeza kusajili kikundi Chao pamoja na barua ya kuomba usajili wa kikundi nenda Halmashauri ofisi ya maendeleo ya jamii ukiwa na hzo nyaraka watakupa kimemo uende kilipia elfu kumi Kama sio ishirini kwenye ofisi ya muhasibu mapato ukisha lipiwa nakupewa risti utaludi Tena ofisi ya maendeleo jamii ukiwa na hyo risti uliyo lipia then watakupa hati ha usajili wa kikundi.

Ukisha sajili kikundi Sasa unaweza kuomba mkopo kwa kumuandikia mkurugenzi wa Wilaya barua ya kuomba mkopo ikitaja kiasi na namba ya utambulisho au usajili wa kikundi ambatanisha pia muhutasari wa kikundi wa kinuia kuomba mkopo pamoja na katiba ya kikundi Kisha zipeleke masijala ya mkurugenzi wa wilaya alafu utasubili majibu.
Hizi ndizo hatua zao, lakini swala langu ni kwenye marketing, je walengwa wana ufahamu na hayo?
 
hiyo mikopo hairejeshwi, wanakikundi wanakopa huko halmashauri, wanaenda kulipa madeni FINCA, tatizo lingine inachukua muda mrefu kupata, na ukimaliza ukitaka kukopa tena, unaambiwa subiri wakope wengine , haina utaratibu mzuri, ni sawa na sadaka tu
 
Hiyo mikopo huwa naisikia kwenye vyombo vya habari tu, sijawahi pata ushuhuda wa mtu ninaemfahamu kuwa kapata mikopo ya vijana, walemavu etc

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ipo Mkuu. Fuatitlia! Kuna pia fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake (WDF) ambazo kimsingi ziko chini ya Uratibu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii), na pia katika Banki ya Posta Kuna dirisha la mikopo nafuu kwa Wanawake ( hili ni dirisha lililorithi shughuli za Benki ya Maendeleo ya Wanawake (WDB).

Fika halmshauri, nenda kwa ofisi ya Maafisa Maendeleo ya Jamii taarifa zote sahihi utapata na wew upate mkopo wako uanze biashara. Kuna halmshauri nyingine, fedha huwa zinarudi baada ya wakopaji kukosekana. Watu wanakopa BRAK, PRIDE, FINCA, TUJIJENGE, sijui PREMIUM kwa riba kubwa wakt zipo halmshauri zisizo kuwa na bugudha.
Hiyo mikopo huwa naisikia kwenye vyombo vya habari tu, sijawahi pata ushuhuda wa mtu ninaemfahamu kuwa kapata mikopo ya vijana, walemavu etc

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Zina riba sema ndogo compare na mabank..Usiseme hazina Riba mkuu
 
Nimekuja likizo kijijini nawaeleza uko Halmashauri Kuna pesa za bwelele kwanza ata ukikopa ukachelewa kurudisha Halmashauri hawadai Kama finca au benki mkopo wanakwambia ulejeshwe ndani ya mwaka mmoja Ila kikundi kinaweza tumia ata miaka mitatu bila kubuguziwa zana wakati mwingine kikundi kisirejeshe kabisa na Halmashauri inakosa Cha kuwafanya.

Kiufupi mm nimeisha zitumia Sana ingawaje mm najitaidi kurejesha kwa wakati hvyo kujenga uwaminifu wa kikundi kupewa pesa nyingi zaidi pindi unapoomba Tena.
Brother naomba unipe mbinu. 0674278639

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jambo la muhimu andaa kikundi Cha watu wasiopungua watano wanaweza kuwa wanawake kwa wanaume au wanawake tu au wanaume tu.

Pili Andi muhutasari wa kikundi kwamba wanachama wamelizia kusajili kikundi Chao

Akikisha kikundi kina katiba ikionyesha idadi ya wanachama, eneo wanapofanyia shughuli zao, uongozi kuanzia mwenyekiti na katibu, namba za simu za viongozi na mengine.

Andika barua ya kuomba kusajiliwa kwa kikundi kwenda kwa mkurugenzi wa Halmashauri usika Ila kupitia kwa mtendaji wa kata usika ili athibitishe uwepo wa icho kikundi usika.

Baada ya kukamilisha hzo nyaraka zote Yani katiba ya kikundi, muhutasari wa kikao Cha wanakikundi wakipendekeza kusajili kikundi Chao pamoja na barua ya kuomba usajili wa kikundi nenda Halmashauri ofisi ya maendeleo ya jamii ukiwa na hzo nyaraka watakupa kimemo uende kilipia elfu kumi Kama sio ishirini kwenye ofisi ya muhasibu mapato ukisha lipiwa nakupewa risti utaludi Tena ofisi ya maendeleo jamii ukiwa na hyo risti uliyo lipia then watakupa hati ha usajili wa kikundi.

Ukisha sajili kikundi Sasa unaweza kuomba mkopo kwa kumuandikia mkurugenzi wa Wilaya barua ya kuomba mkopo ikitaja kiasi na namba ya utambulisho au usajili wa kikundi ambatanisha pia muhutasari wa kikundi wa kinuia kuomba mkopo pamoja na katiba ya kikundi Kisha zipeleke masijala ya mkurugenzi wa wilaya alafu utasubili majibu.
Naomba kusave hiki ulichotuelekeza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huku niliko hizo habar hata hazipo,, zaidi tu zimeibuka ofc nyingi nyingi sana eti za mikopo tena za riba kubwa balaa! Sasa cjui ndo iyo mikopo yenyewe ila waliopewa dhamana wameamua wajinufaishe wenyewe bila kujali walengwa au lah!.

Kwangu mm naona elimu juu ya hili c tu kwamba haitoshi bali haipo kabisa,, na hii ni wazi ni ili watu wapate kupiga pesa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom