Je mtu ambaye mazoezi ni sehemu ya maisha yake anaweza kupata stroke?

Je mtu ambaye mazoezi ni sehemu ya maisha yake anaweza kupata stroke?

Yeah

Tena kuwa makini haswa hawa body builders..... maana mwili ukiwa mkubwa sana unashindwa kutawalika vema.

Mishipa ya damu inaweza kubanwa na misuli akapata rhabdomyolysis na hata migando ya damu hadi akapata stroke.

Lakini pia mazoezi magumu yanaongeza presha na usipoangalia unaweza kupata stroke.

Muhimu tu kufanya kiafya, sio kimashindano hayo mazoezi menyewe.
 
Eti wakuu hii kitu inakuwaje au ndo hainaga formula maalum?
Habari!

Mazoezi yanaweza kukupa faida au hasara kulingana na utekelezaji wake ili kukukiga na suala husika.

Faida/kuzuia stroke (kiharusi) hutokana na kubadili/modify risks za stroke kama unene/uzito mkubwa, mafuta, kisukari nk.

Swali lako halina jibu la moja kwa moja. Hii inatokana na swali ulilouliza hutegemea vipengele vingine kama:

A: MAZOEZI

1: Aina ya mazoezi (inashauriwa yawe ni aerobics, yanayohusisha viungo vyote vya mwili kama kutembea kwa kasi nk.).

2: Kiasi cha mazoezi(yawe ni ya kiasi ambacho mwili wako unaweza kuhimili bila shida kwa kuzingati: matatizo mengine ya kiafya yaliyopo, umri, uzito nk.)

3: Mazoezi kupita kiasi huweza kuwa chanzo cha stroke na shambulio la moyo pia kuleta athari kwenye figo.(stroke/kiharusi: kwa wenye matatizo ya mapigo ya moyo/arrhythmias, wenye matatizo ya kuta za mishipa ya damu/anyurizimu nk.).

B: MWENENDO WA MAISHA

Mazoezi ni muhimu kuambatana na mabadiliko kwenye maisha.

1: Kunywa pombe kwa wastani

2: Kuacha kuvuta sigara

3: Kula chakula kwa kuzingatia mahitaji ya mwili, kazi au umri.

4: Kutumia dawa kwa usahihi hasa wale wenye matatizo ya kiafya kama: presha, sukari na matatizo ya mafuta/cholesterol.
Pia dawa ya kulainisha damu inapobidi.

5: Kutimia kwa wastani vinywaji vinavyopeleka moyo mbio kama: kahawa nk.
 
Back
Top Bottom