Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ohooo na POLISI tena kwani ni uhalifuNnavyojua mim ni watatu, ila kuna rafki angu mke wake amejifungua watoto5 wanne kwa operation na mmoja wa mwisho amejifungua kawaida, ila alitaftwa na polisi akatembea
Sasa hivi wanadai ni wanne
Nnavyojua mim ni watatu, ila kuna rafki angu mke wake amejifungua watoto5 wanne kwa operation na mmoja wa mwisho amejifungua kawaida, ila alitaftwa na polisi akatembea
Wawili tu?? Kwa usalama wake?? Nini hatari ta kuendelea kuzaa?kifupi anaweza kujifungua wengi tu kama usalama wa kiafya kwa mama ukizingatiwa.
Ila kwa utaratibu (sio sheria) wa sasa yaani mpya, upasuaji kwa sababu za uzaji mwisho mara mbili (hapo elewa sijasema mwisho watoto wawili, ila upasuaji ndio mwisho mara 2), yaani mama akijifungua kwa upasuaji leo anatakiwa kupewa elimu kuwa kama ikitokea akijigungua kwa upasuaji tena katika mimba inayofuata basi ndio iwe mwisho aombe kufunga kizazi, hii ni kwa ajili ya usalama wake yeye.
Niliweka mpaka maelezo ya ziada kwenye mabano lakini umeshindwa kuelewa mbona no tatizo. Sijasema wawili, nimesema mara 2, hebu soma tena mkuu.Wawili tu?? Kwa usalama wake?? Nini hatari ta kuendelea kuzaa?
Thanks sana mkuu usichoke kuelezea watu wanahitaji elimu mkuuNiliweka mpaka maelezo ya ziada kwenye mabano lakini umeshindwa kuelewa mbona no tatizo. Sijasema wawili, nimesema mara 2, hebu soma tena mkuu.
Madhara pitia comment ya mdau hapo juu pia, ishu kubwa ni kuhofia mfuko wa uzazi kupasuka wakatiwa wa ujauzito hasa mama akiwa kwenye uchungu maana unakuwa umelegea kwa makovu.
Nb: kovu likipata muda mrefu wa kupona linakuwa si hatari sana, ila tahadhari ni bora kuliko baya litokee.
asante sana mkuu kwa maelezo mazuri umewaokoa wengi ila nina swali zaidi KWANINI WAMAMA WENGI WANAJIFUNGUA KWA OPERATION SIKU HIZI KULIKO MWANZO?Binafsi nimeona mama amejifungua kwa operation mara tano na yupo salama mpaka hivi ninavyoandika hapa..
Kusema kweli kibinadamu hatuko sawa..kwa hiyo kinachozingatiwa ni uimara wa kizazi cha mama kuweza kuhimili makovu yatokanayo na operations hizi..
Namanisha nini? Jinsi kizazi kinavyokuwa na makovu mengi ndivyo na uimara wake unavyopungua..kuna mama mwingine hata kufanyiwa mara mbili tu,kizazi unakikuta kimechoka sana..so,kivyovyote vile kumruhusu kuendelea kushika mimba ni kumweka ktk hatari kubwa..
Kwa uzoefu na simple majority, wamama wengi wanaweza kuhimili operations 2 - 3, na pengine labda ndipo hiyo perception ya operations 2 au 3 linapotokea..ila ukirudi kwenye uhalisia,swala hili linategemea namna gani kizazi kinahimili makovu yatokanayo na operations..
Lakini kama tungezingatia hatari kubwa inatokanayo na makovu haya,mjadala wetu usingekuwa mara ngapi mama anatakuiwa kupasuliwa! Pengine labda tungejikuta tunakubaliana kwamba labda mama akishajifungua kwa operation asirudie tena!!
Ni vema tufahamu kwamba,kwamba mshono/kovu likifumuka,mtoto anatoka ndani ya kizazi,anaelea tumboni kwa mama,na damu nyingi inamwagika ndani kwa ndani..ktk mazingira kama haya,hatuzungumzii tena kukosa mtoto(maana hawezi kusurvive hata kwa dakika chache) bali kwamba kama tutachelewa kuchukuwa hatua stahiki,tutamkosa na mama pia..
Mara nyingi kupasuka kwa mshono hutokea mama anapokuwa ameanza uchungu..sasa fikiria mama ananza uchungu akiwa mbali na hospitali!
Na bahati mbaya asilimia kubwa ya wamama hawana uhakika na lini mara ya mwisho kuona siku zao za hedhi na hii huleta tabu ktk makadirio ya siku za kujifungua! Kwa hiyo mama anataja tarehe yoyote tu ilimradi kujibu swali aliloulizwa klinik..matokeo yake ni makadirio ya uongo..na mbaya zaidi mama anazingatia tarehe hii ya kujifungua ambayo ni ya uongo!
Sasa fikiria mama anazingatia tarehe ya uongo,anaendelea na shughuli zake,mimba inafika wakati wa kujifungua,mama hana habari(maana tarehe ya makadirio bado sana)..uchungu unamuanza yupo shambani,safarini,harusini...mshono unaachia!!! Hivi kuna maana hapa kuendelea kubishana idadi ya operations jamani?!!
asante sana mkuu kwa maelezo mazuri umewaokoa wengi ila nina swali zaidi KWANINI WAMAMA WENGI WANAJIFUNGUA KWA OPERATION SIKU HIZI KULIKO MWANZO?
Kwa nini polisi wamtafute?Nnavyojua mim ni watatu, ila kuna rafki angu mke wake amejifungua watoto5 wanne kwa operation na mmoja wa mwisho amejifungua kawaida, ila alitaftwa na polisi akatembea