Je, nadharia ya karma ina ubaguzi?

Je, nadharia ya karma ina ubaguzi?

Blueface

Member
Joined
May 2, 2020
Posts
46
Reaction score
47
Kwa mujibu wa nadharia hii ni kwamba kwa kila tendo liwe zuri au baya utapokea malipo yake hapahapa duniani kabla haujafa. Kwa baadhi ya watu nadharia hii inafanya kazi ila kwa watu wengine inakataa kwa nini?

Kwa mfano viongozi wa nchi ya Marekani wameamrisha mauaji ya watu wengi duniani, wamesababisha vita visivyoisha sehemu nyingi. Nchi nyingi zimesambaratika watu wake wanaishi maisha dhiki kuu. Labda ungetegemea karma iwashugulikie na wao wapate misukosuko au hata kurukwa na akili kwa wingi wa damu walizo mwaga lakini wapi, yaani wanaishi maisha mazuri yenye starehe nyingi tena wanaishi umri mrefu hadi miaka 90.

Mfano mwingine, kwenye ukoo wenu wale ndugu wenye roho nzuri za kusaidia wenzao kwa huruma na upendo huwa na maisha magumu tena ya kawaida tu. Lakini wale wachache wenye uwezo wanaweza kuwa wabinafsi wanojijali wao yani mtu anaweza ugua asitoe msaada mpaka mgonjwa akafa ndo anatoa msaada wa mazishi.

Cha ajabu mtu huyu anaendea na maisha yake vizuri na watoto wake watafika hadi chuo kikuu na badae kupata nzuri. Nyie wenye roho za kusaidiana mnaendelea na maisha yenu ya kuunga unga.

Mfano wa mwisho, Tanzania ilisaidia nchi nyingi kupata uhuru kama vile Afrika kusini, Angola, Zimbabwe, Namibia na Msumbiji. Ungetegemea Karma iibebe Tanzania kwa wema wake lakini tumeendelea kuishi maisha magumu ya kimasikini tena tukipitwa kiuchumi na nchi tulizo zisaidia!

Je, hii nadharia ina ubaguzi katika malipo? Naomba majibu yenu wadau.

cc Pascal Mayalla, Mshana Jr r, GENTAMYCINE na wajuzi wengine wa JF.
 
Inafanya kwa kulingana na haki that's why inasubiri wakati muafaka
 
Inafanya kwa kulingana na haki that's why inasubiri wakati muafaka
Wakati upi huo?mfano hao viongozi wa Marekani wamesababisha mauaji mengi duniani lakini hawapati shida yoyote wanaishi maisha ya starehe tena kwa umri mrefu tu hadi miaka tisini hio karma hua haiwaoni iwalipe matendo yao?Wameua watu huko Iraq, Libya, Afghanstan, Yemen, Kongo, Somalia n.k mbona Karma karma haiwalipi?
 
Kwa mujibu wa nadharia hii ni kwamba kwa kila tendo liwe zuri au baya utapokea malipo yake hapahapa duniani kabla haujafa. Kwa baadhi ya watu nadharia hii inafanya kazi ila kwa watu wengine inakataa kwa nini?

Kwa mfano viongozi wa nchi ya Marekani wameamrisha mauaji ya watu wengi duniani, wamesababisha vita visivyoisha sehemu nyingi. Nchi nyingi zimesambaratika watu wake wanaishi maisha dhiki kuu. Labda ungetegemea karma iwashugulikie na wao wapate misukosuko au hata kurukwa na akili kwa wingi wa damu walizo mwaga lakini wapi, yaani wanaishi maisha mazuri yenye starehe nyingi tena wanaishi umri mrefu hadi miaka 90.

Mfano mwingine, kwenye ukoo wenu wale ndugu wenye roho nzuri za kusaidia wenzao kwa huruma na upendo huwa na maisha magumu tena ya kawaida tu. Lakini wale wachache wenye uwezo wanaweza kuwa wabinafsi wanojijali wao yani mtu anaweza ugua asitoe msaada mpaka mgonjwa akafa ndo anatoa msaada wa mazishi.

Cha ajabu mtu huyu anaendea na maisha yake vizuri na watoto wake watafika hadi chuo kikuu na badae kupata nzuri. Nyie wenye roho za kusaidiana mnaendelea na maisha yenu ya kuunga unga.

Mfano wa mwisho, Tanzania ilisaidia nchi nyingi kupata uhuru kama vile Afrika kusini, Angola, Zimbabwe, Namibia na Msumbiji. Ungetegemea Karma iibebe Tanzania kwa wema wake lakini tumeendelea kuishi maisha magumu ya kimasikini tena tukipitwa kiuchumi na nchi tulizo zisaidia!

Je, hii nadharia ina ubaguzi katika malipo? Naomba majibu yenu wadau.

cc Pascal Mayalla, Mshana Jr r, GENTAMYCINE na wajuzi wengine wa JF.
Karma haina ubaguzi na haifanyi kazi kwa matakwa ya kibinadamu... Kama ina ratiba yake, maamuzi yake na namna yake ya kutenda ambayo iko juu ya uwezo wa kawaida wa fikra za kibinadamu

Pili karma sio kitu cha leo ama jana.. Karma iko kwenye kwenye unbreakable life cycle haina mwanzo haina mwisho... Malipizi yake.. Hitting back yanaweza kuchelewa ama kuwahi kutegemeana na uzito, uzuri ama ubaya wa jambo husika

Tatu.. Karma ina viwango vya asilimia... Yaani katika mabaya na mazuri uliyotenda je mizania inaelemea wapi? Kwa kiasi gani?
Nitarejea....

Jr[emoji769]
 
Karma haina ubaguzi na haifanyi kazi kwa matakwa ya kibinadamu... Kama ina ratiba yake, maamuzi yake na namna yake ya kutenda ambayo iko juu ya uwezo wa kawaida wa fikra za kibinadamu

Pili karma sio kitu cha leo ama jana.. Karma iko kwenye kwenye unbreakable life cycle haina mwanzo haina mwisho... Malipizi yake.. Hitting back yanaweza kuchelewa ama kuwahi kutegemeana na uzito, uzuri ama ubaya wa jambo husika

Tatu.. Karma ina viwango vya asilimia... Yaani katika mabaya na mazuri uliyotenda je mizania inaelemea wapi? Kwa kiasi gani?
Nitarejea....

Jr[emoji769]
[/QUOTE
Asante mkuu, naamini utakuja na nondo zingine zaidi tuelimishane
 
Unaweza kuona mtu ana maisha mazuri kwa muonekano wa nje ila hujui ndani anasumbuliwa na nini

Wengine wana*irwa usiku kimya kimya
 
Karma haina ubaguzi na haifanyi kazi kwa matakwa ya kibinadamu... Kama ina ratiba yake, maamuzi yake na namna yake ya kutenda ambayo iko juu ya uwezo wa kawaida wa fikra za kibinadamu

Pili karma sio kitu cha leo ama jana.. Karma iko kwenye kwenye unbreakable life cycle haina mwanzo haina mwisho... Malipizi yake.. Hitting back yanaweza kuchelewa ama kuwahi kutegemeana na uzito, uzuri ama ubaya wa jambo husika

Tatu.. Karma ina viwango vya asilimia... Yaani katika mabaya na mazuri uliyotenda je mizania inaelemea wapi? Kwa kiasi gani?
Nitarejea....

Jr[emoji769]

Kwahio mizan ya mema ikiwa nyingi zaidi je hautolipishwa dhambi za ubaya?
 
Back
Top Bottom