Je nafsi hutabiri matukio yajao?

Kacharimbe

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2011
Posts
216
Reaction score
35
Wakuu heri ya mwaka mpya. Kwa muda sasa suala hili limekuwa likinisumbua. Imenitokea mara kadhaa kuwa naweza kuwaza kitu fulani au mtu fulani sura yake ikaja na baadaye kitu hicho hutokea au kama ni mtu unaona anakuja au unakutana naye. Leo nilikuwa naweza jinsi ya kutoka ofisini ili niende kwenye sherehe. Wazo likaniijia kuwa nisingizie kuwa kwa jirani kuna msiba. Wazo hilo nikalifuta haraka sana. Haijapita hata saa moja nikapigiwa simu kuwa jirani yangu amefariki. Hi ni nini au ni coincidence?
 
ni kweli mkubwa nafsi kupitia maumbile zina madaraja mbalimbali,wako watu wanapata ndoto za kweli kama taarifa ya tukio linalotarajiwa,wengine bila hata kuota bali wazo lolote litalomjia bila shinikizo huwa ni taarifa ya kweli,wako pia ambao akikuapiza au kukulaani kwa chochote hutokea kweli,hivi ni sehemu ndogo ya vipawa ambavyo baadhi ya binadamu wamepewa.ndipo wengine wakishajigundua kuwa na mambo kama haya hujifanya waganga kuibia watu.haya ni mambo ambayo manabii walipewa rasmi kabisa kuwa nayo na ndio chimbuko la miujiza,lakini hata watu wa kawaida hubahatika kuwa na baadhi ya mambo.
 
Naam ! Kwangu mimi nadhani hilo lina ukweli....mfano siku anafariki sharomilionea usiku ule anapata ajali nimeota kuna mtu anapata ajali ya gari akiwa pekee yake na anafariki, nashtuka mida ya saa tisa simu inaita Alikuwa ni rafiki yangu ananipa habari kuhusu kifo cha sharo... asubuhi vyombo vya habari vikaelezea ile ajali haikuwa na utofauti wowote na kile nilichoona ndotoni.

Mara nyingi sana huwa naota kweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…