Je, naweza kushitaki chuo kwa kutonitengenezea cheti changu kwa miaka 6 sasa?

Je, naweza kushitaki chuo kwa kutonitengenezea cheti changu kwa miaka 6 sasa?

Cachondo

Senior Member
Joined
May 6, 2019
Posts
144
Reaction score
139
Habari Wana jamii,

Upande wa Sheria! Nilimaliza masomo yangu ngazi ya stashahada kwenye chuo kimoja wapo cha serikali hapa jijini dsm mwaka 2016. Tatizo likaja sikuwa nimemaliza ada tena hela nyingi tu na hata nilipotoka field nakuandaa ile field report tukazikusanya kwa msimamizi wetu wa pale chuoni, lakini ukipeleka anakwambia njoo na risiti ya malipo ya ada na kama huna hiyo report siipokei. Mi nikampa mezani pale nikasema ada sijalipa ila nitalipa tu sababu sijapata cheti.

Akaichukua akaiweka, sasa 2017 nimelipa ada yote nilipata mfadhili. Ikanibidi nifuate cheti, nakuta hakuna cheti wala transcript, nikauliza kwa afisa wa mitihani kulikon? Akasema ngoja tutizame faili kisha tutakujulisha sasa tokea pale sikutafutwa mpaka 2020 nilipoenda tena nikakuta hakuna cheti, nikauliza tena sasa ikawa Kama ndo wameniona na kusikia jambo lile kwa mara ya kwanza, nikaacha namba yangu ya usajili na ya simu, napo hawakunitafuta.

Wiki mbili mfululizo zilizopita 2022 nimeenda tena kuchukua nakuta hamna, jibu pia la msingi hakuna yani hamna mtu alofanyia kazi swala lile, nikaenda kwa afisa mitihani nikamkuta mpya nikamueleza shida yangu akasema mwambie mtu wa masijala akuangalizie faili kisha lilete kwangu, hapo ndo tatizo lilipo masijala.

Naambiwa njoo kesho, njoo kesho, njoo kesho mpaka wiki 2 zimeisha na nimechoka. Je naweza kwenda kuwashitaki mahakamani kwa kutonitengenezea cheti changu?
 
Wakati ambapo wewe hukutafutwa ilibidi wewe uwatafute. Ofisi za Umma bila kushinikiza matokeo yake ndio hayo.

Pole sana ila siku nyingine jifunze kufuatilia mambo yako kwa ukaribu(mara kwa mara).

Ngoja waje kukupa muongozo
 
Duu! Inasikitisha namna ulivyofwatilia swala lako kwakusuasua, nadhani ungetiliamkazo wakufwatilia Mara kwa Mara ungefanikiwa.

Unaweza kuchukua hatu zakisheria dhidi ya chuo. Lakini unapaswa kufwata utaratibu kwanza wakupeleka malalamiko yako ngazi za juu za uongozi wachuo ili kupata muafaka kabla yakwenda mahakamani.

Tambua ukiruka hatua yakutopitia ngazi za juu za chuo zauongozi na kuwasilisha malalamikoyako kwajili ya kupatiwa ufumbuzi swala lako likifika mahakamani litakuwa premature hivyo litatupiliwa njee.

Kwasasa anza kwanza kuwasilisha malalamiko yako kwenye ngazi za juu za utawala wa chuo then ikishindikana hapo kupata suluhu utaenda mahakamani.
 
Kampala University sio chuo ni uhuni
 
vyuo vingi hasa hv vya serikali vyeti vinatengenezwa nje ya nchi kuepuka kufogi inaelekea jina lako halikupelekwa ndio maana wanarukaruka muone Principal wa chuo chako kwanza kabla ya kwenda Mahakamani
 
Andika barua kwenda chuoni, eleza hatua ulizopitia katka ufuatiliaji na copy ipitie kwa principal wa chuo. Usisahau kubaki na nakala.
 
Kwanini hujataja jina la chuo Inaonesha bado unahuruma nao.

Maelezo ya wadau hapo yamejitosheleza sana
Kwa hatua hiyo kamuone makamu mkuu wa chuo ama mkuu wa chuo kwa mujibu wa vyeo vyao, kama hakutakuwa na muafaka fika mahakamani

Lakini kama walivyosema wadau wenzio vyeti huwa tunapiga kambi hata ya mwezi mzima mpaka wakitoe tuu
 
Kwa Dar hakuna baridi Kama njombe akikuambia njoo kesho wewe nenda asubuhi shinda hapo na ikibidi lala getini na mlinzi mkipiga stori. Nakuapia siku tatu hazifiki umeshapita Cheti chako. Tatizo wewe unafuatilia ukipata Dili linalohitaji Cheti, Dili likipita unaacha kufuatilia mpaka upate tena.
 
Sisi tulifuatilia miska mi4 na hatimae tumepata mwaka huu tangu 2018. Hakuna sehemu ambayo hayukufika. Ilibaki kwa pm rais tu
 
Ndugu yangu mzembe ni wewe. Ulipaswa kupiga kambi hapohapo na ukiwakumbusha kuwa unatumia nauli kutoka mkoani lazma wangekupa
 
Duu! Inasikitisha namna ulivyofwatilia swala lako kwakusuasua, nadhani ungetiliamkazo wakufwatilia Mara kwa Mara ungefanikiwa.

Unaweza kuchukua hatu zakisheria dhidi ya chuo. Lakini unapaswa kufwata utaratibu kwanza wakupeleka malalamiko yako ngazi za juu za uongozi wachuo ili kupata muafaka kabla yakwenda mahakamani.

Tambua ukiruka hatua yakutopitia ngazi za juu za chuo zauongozi na kuwasilisha malalamikoyako kwajili ya kupatiwa ufumbuzi swala lako likifika mahakamani litakuwa premature hivyo litatupiliwa njee.

Kwasasa anza kwanza kuwasilisha malalamiko yako kwenye ngazi za juu za utawala wa chuo then ikishindikana hapo kupata suluhu utaenda mahakamani.
Sawa, asante sana
 
vyuo vingi hasa hv vya serikali vyeti vinatengenezwa nje ya nchi kuepuka kufogi inaelekea jina lako halikupelekwa ndio maana wanarukaruka muone Principal wa chuo chako kwanza kabla ya kwenda Mahakamani
Haya mkuu nimepokea
 
Kwanini hujataja jina la chuo Inaonesha bado unahuruma nao.

Maelezo ya wadau hapo yamejitosheleza sana
Kwa hatua hiyo kamuone makamu mkuu wa chuo ama mkuu wa chuo kwa mujibu wa vyeo vyao, kama hakutakuwa na muafaka fika mahakamani

Lakini kama walivyosema wadau wenzio vyeti huwa tunapiga kambi hata ya mwezi mzima mpaka wakitoe tuu
Sawa sawa, mi nilifululiza kwenda sana. Tatzo lipo pale masijala kuna mabinti pale ni shida kidogo
 
Kwa Dar hakuna baridi Kama njombe akikuambia njoo kesho wewe nenda asubuhi shinda hapo na ikibidi lala getini na mlinzi mkipiga stori. Nakuapia siku tatu hazifiki umeshapita Cheti chako. Tatizo wewe unafuatilia ukipata Dili linalohitaji Cheti, Dili likipita unaacha kufuatilia mpaka upate tena.
Ni kweli, kwa miaka miwili baada ya kumaliza kilikuwa kinanikwamisha ni ada. Sikuwa nimemaliza, sasa nilipomaliza ndo nikaanza kufuatilia ndo nikakutana na majibu yale. 2020 niligombea sehem moja hivi udiwani, kwenye fomu elimu yangu nikaweka nina diploma, sasa kwenye mahojiano nilitaka niende na nyaraka halali ili wasinitoe kwenye reli, basi nikaenda chuo ila sikuambulia kitu
 
Kwanini hujataja jina la chuo Inaonesha bado unahuruma nao.

Maelezo ya wadau hapo yamejitosheleza sana
Kwa hatua hiyo kamuone makamu mkuu wa chuo ama mkuu wa chuo kwa mujibu wa vyeo vyao, kama hakutakuwa na muafaka fika mahakamani

Lakini kama walivyosema wadau wenzio vyeti huwa tunapiga kambi hata ya mwezi mzima mpaka wakitoe tuu
Chuo cha diplomasia pale kurasini jkt mgulani
 
Habari Wana jamii,

Upande wa Sheria! Nilimaliza masomo yangu ngazi ya stashahada kwenye chuo kimoja wapo cha serikali hapa jijini dsm mwaka 2016. Tatizo likaja sikuwa nimemaliza ada tena hela nyingi tu na hata nilipotoka field nakuandaa ile field report tukazikusanya kwa msimamizi wetu wa pale chuoni, lakini ukipeleka anakwambia njoo na risiti ya malipo ya ada na kama huna hiyo report siipokei. Mi nikampa mezani pale nikasema ada sijalipa ila nitalipa tu sababu sijapata cheti.

Akaichukua akaiweka, sasa 2017 nimelipa ada yote nilipata mfadhili. Ikanibidi nifuate cheti, nakuta hakuna cheti wala transcript, nikauliza kwa afisa wa mitihani kulikon? Akasema ngoja tutizame faili kisha tutakujulisha sasa tokea pale sikutafutwa mpaka 2020 nilipoenda tena nikakuta hakuna cheti, nikauliza tena sasa ikawa Kama ndo wameniona na kusikia jambo lile kwa mara ya kwanza, nikaacha namba yangu ya usajili na ya simu, napo hawakunitafuta.

Wiki mbili mfululizo zilizopita 2022 nimeenda tena kuchukua nakuta hamna, jibu pia la msingi hakuna yani hamna mtu alofanyia kazi swala lile, nikaenda kwa afisa mitihani nikamkuta mpya nikamueleza shida yangu akasema mwambie mtu wa masijala akuangalizie faili kisha lilete kwangu, hapo ndo tatizo lilipo masijala.

Naambiwa njoo kesho, njoo kesho, njoo kesho mpaka wiki 2 zimeisha na nimechoka. Je naweza kwenda kuwashitaki mahakamani kwa kutonitengenezea cheti changu?
Unaweza karibu ofisini tukuhudumie 0677 333517
 
Back
Top Bottom