Je, nchi inaongozwa kwa utashi wa Rais au kwa Katiba na Sheria?

Je, nchi inaongozwa kwa utashi wa Rais au kwa Katiba na Sheria?

GUSSIE

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2014
Posts
3,880
Reaction score
11,134
Wanabodi, Mada hii ni kutokana na kongamano la kujadili siku Mia moja za Rais Mama Samia Suluhu Hassan, Wasimamizi wa taasisi zote kwa kuzitaja TRA, Bandari, TCRA na Uhamiaji wamejitokeza kwenye kongamano huku wakisifu na kusema wametekeleza kauli, Matamko na hotuba za Rais Samia Suluhu Hassan kwa siku Mia moja na wameona tofauti na awamu iliyopita kwa kukusanya mapato mengi na kuacha watu wawe huru

Je?, kama nchi tunafuata katiba na sheria tulizoziweka au tunasimamia kauli za Rais, Hayati Magufuli alifanya mambo bila kufuata katiba wala sheria na mwisho wa siku ukajengeka ufalme kwa Rais kuikamata mahakama na Bunge. Watu wote ambao Rais Hayati Magufuli kwa mazingira ya kujificha aliweka mkono wa kuwahukumu kupitia mahakama kesi zao zinafutwa na Sasa Wengine wanarudishiwa Faini zao

Kama Rais ndio katiba na yupo juu ya katiba na sheria kwanini tuwe na Bunge na Mahakama, Rais anaweza kuilazimisha mahakama yaani majaji na Mahakimu kufuata atakavyo na kutenda atakayo, Ni muda muafaka kwa watakao anza kujadili katiba waufute muhimili wa mahakama kabisa na kuanzisha Mahakama ya Rais nchi nzima itakayotekeleza kauli za Rais na sio kuwa na mfumo wa mahakama kama sasa

Je? Bunge la Job Ndugai ni Bunge linalomilikiwa na utashi wa Rais au lipo kwa Katiba na Sheria, Kama ni Bunge la katiba kwanini linawakumbatia Halima mdee na wenzake ambao hawatakiwi kuwa Bungeni

Bunge la Job Ndugai limetumika kupora haki za wapinzani kama Tundu lissu kwa kuwa liliendeshwa kwa utashi wa Rais, Bunge lilitumika na kulazimishwa kupitisha sheria kwa utashi wa Rais na hili Job Ndugai mwenyewe anajishangaa na kushangaa kwanini Bunge aliloliongoza lilipitisha sheria za uhujumu Uchumi, uchochezi na kila aina ya vituko
Ni muhimu watakaojadili katiba mpya walifute Bunge la sasa na kuanzisha Bunge la Rais ambalo litatumika kupitisha Matamko, kauli na utashi wa Rais

Ni muda muafaka kuelimisha jamii kuhusu taratibu za nchi, Tunawalaumu watu kama Ole Sabaya na Paul Makonda kuwa walifuata utashi wa Rais na sio sheria na katiba, Yawezekana Sabaya na Makonda waliyafanya waliyoyafanya baada ya kuona Rais ndio katiba na Rais yupo juu ya sheria, Rais ana uwezo wa kuliamuru Bunge na kuilazimisha mahakama kufuata ngoma na mdundiko auchezao Yeye Rais na sio katiba na Sheria


Bila umakini wa katiba kila Rais atajifanyia atakalo kwa kisingizio cha Maendeleo, kujenga nchi au kujenga Uchumi huku akiminya uhuru wa Raia wa kisiasa na kukosoa

Mjadala wa katiba ni muhimu sana
#Katiba mpya kwa maslahi ya Tanzania mpya
 
Hoja nzuri sana mkuu.
Ingawa kuna Lumumba wenzio kina elitwege and co hawaoni umuhimu wa katiba mpya. Lakini kwa mambo yalivyoenda na yanavoenda sasa katiba mpya ni muhimu sana.
 
Magufuli alisema anataka kuwaachia huru mahabusu wote. Ukisema "Magufuli mkali kafunga watu,Samia mpole kawaachia huru," you are falsifying history.

Rather,Samia Suluhu anaendeleza dhamira ya Magufuli ya kutaka kuwaachia huru wale watu.

Ukisema"yule bwege kaondoka,sasa watu wanaweza kuachiwa huru",you are falsifying history.

It was unprecedented,haijawahi kutokea katika historia ya nchi yetu. Magufuli alisema anataka mahabusu wote wote waachiliwe huru,na mahabusu ipigwe deki.

Lakini watu walishindwa kuelewana DPP au DPP alishindwa kuelewana na watu wale.

Na kwa hiyo hawa watu wameachiwa huru,not so much because they are innocent ,isipokuwa sasa umeanza Awamu Mpya, unataka kuianza kwa good will,kwa hiyo unaweka reset button.

Kwa maana kwamba utatosheka kuwakamata wezi walioiba wewe ulipoanza kazi,na hao wezi wa zamani,utawasamehe.

Kuhusu ESCROW tulisema wakati ule,ukiwaibia wakulima wa Tanzania watakusamehe,mradi tu usifanye mazoea.
 
Leo Mama kasema anajenga Uchumi kwanza
 
Ni ngumu sana kwa kiongozi wa Africa kufata katiba hata tukibadili katiba na kuweka katiba mpya rabda katiba hyo isimamiwe na JWTZ ndo rabda watakuwa na uwezo wa kumwambia Rais kuwa anavunja katiba akawasikiliza nje ya hapo tutakuwa tunapoteza Muda tu

Ukiangalia serikali inayojiita ya awamu ya 6 japo watu wanawaona ni wazuri lakini hakuna watu wavunja katiba kama serikali hii sema kwa vile wapiga matarumbeta na wachawa wapo busy kusifia tu unawezaje ndani ya miezi 3 kuanza kutoa waharifu jela je hawa waharifu wanatoka kwa utashi wa kisheria au kimahakama au kuna mtu ameamua tu kwa maono yake watoke? Siku Tanzania ikipata Rais mwendawazimu anaweza kutuletea matatizo makubwa sana kwa vile anaetaka nchi ifanye nini na iweje ni mtu mmoja tu
 
Katiba mpya ni inevitable.
Kwani suala la mikutano ya hadhara likoje kwenye katiba ya JMT.?
 
Back
Top Bottom