dada wangu?? Duh ! Btw wakenya hawajui kiswahili..
Kwa mda mrefu, nilikuwa nikijua kuwa tunasema "dada yangu." Lakini mda kidogo uliopita, nilikuwa nikitazama runinga ya KBC katika kipindi fulani kinachojihusisha na ukuzaji wa lugha ya Kiswahili, na huyu mhojiwa akasema kuwa mtungo sahihi ni Dada Wangu kwasababu neno "dada" liko katika ngeli ya a-wa. Je, wana JF wasemaje?
Sikuelewi mkuu; jibu ni lipi?
Je wajua Kiswahili kilizaliwa Mvita wala si Ugunja? Kile kilichotuuza ni uongozi mbaya wa kisiasa
Zingatia:
1.Kuku wangu...(kuku yangu X)
2.Dada yangu...(dada wangu X)
ukisoma vizuri ngeli kuna aina za ngeli kulingana na mitazamo tofauti,labda ye sijui anauzungumzia upi?ila nnachofaham mm ni dada yangu ni kiswaili sanifu,kwani unapotaka kutumia upatanisho wa kisarufi utasema dada yangu analima{umoja} pia utasema dada zangu wanalima{uwingi}utapata ngeli ya a_wa pia ukimchukua paka utasema paka wangu analia{umoja}pia utasema paka wangu wanalia{uwingi} utapata pia ngeli ya a_wa sasa kumbe ktk ngeli itategemea nani unaemzungumzia kati ya mtu au kitu,lakini pia tukumbuke kuna udhaifu katika kila ngeli huo pia ni udhaifu wa ngeli ya upatanisho wa kisarufi,huo ndo mtazamo wangu labda tujifunze kwa wadau wengine.
Aliyekuwa akinena haya alikuwa mwalimu wa shule fulani ya msingi, na nikidhani ni mwanafunzi wa yule mwandishi wa Kitanzania Wallah Bin Wallah. Kwa kweli aliponena hayo nilishangazwa sana. Lakini nilipokuja kuitazama kwa undani, niliona ukweli kiasi fulani. Kwa mfano, twasema, "mtoto wangu," ingawa mtoto si mnyama bali ni mtu. "Mke wangu" na "Mme wangu" Kwanini basi baba, mama, bibi ziwe tofauti? Na bwana je? Twasema "Bwana wangu" Kwanini tuje tusememe bibi yangu? Mjomba, Mchumba - wote ni wangu.
Hapa ndio nazidi kuchanganyikiwa zaidi,,,,,,,,dada wangu...!!!Aliyekuwa akinena haya alikuwa mwalimu wa shule fulani ya msingi, na nikidhani ni mwanafunzi wa yule mwandishi wa Kitanzania Wallah Bin Wallah. Kwa kweli aliponena hayo nilishangazwa sana. Lakini nilipokuja kuitazama kwa undani, niliona ukweli kiasi fulani. Kwa mfano, twasema, "mtoto wangu," ingawa mtoto si mnyama bali ni mtu. "Mke wangu" na "Mme wangu" Kwanini basi baba, mama, bibi ziwe tofauti? Na bwana je? Twasema "Bwana wangu" Kwanini tuje tusememe bibi yangu? Mjomba, Mchumba - wote ni wangu.
Aliyekuwa akinena haya alikuwa mwalimu wa shule fulani ya msingi, na nikidhani ni mwanafunzi wa yule mwandishi wa Kitanzania Wallah Bin Wallah. Kwa kweli aliponena hayo nilishangazwa sana. Lakini nilipokuja kuitazama kwa undani, niliona ukweli kiasi fulani. Kwa mfano, twasema, "mtoto wangu," ingawa mtoto si mnyama bali ni mtu. "Mke wangu" na "Mme wangu" Kwanini basi baba, mama, bibi ziwe tofauti? Na bwana je? Twasema "Bwana wangu" Kwanini tuje tusememe bibi yangu? Mjomba, Mchumba - wote ni wangu.