Je, ni Data gani zinapaswa kulindwa katika Sheria ya Ulinzi wa Data?

Je, ni Data gani zinapaswa kulindwa katika Sheria ya Ulinzi wa Data?

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
Copy of You Are Lovely Photo Valentine’s Instagram Post.png



JE, DATA GANI ZINAPASWA KULINDWA CHINI YA SHERIA YA ULINZI WA DATA?

Sheria ya #UlinziWaData ambayo bado haipo nchini Tanzania inaumuhimu mkubwa kwasababu itasaidia kulinda #Data kama zifuatazo:

Majina ya Watu(Wateja kama ni kwenye Kampuni ya biashara), Anuani za Posta na Makazi za Wananchi ambao na Wateja wa Makampuni ya biashara

Barua pepe za watu, hii inajumuisha mawasiliano yote yanayaofanyika kwa njia ya barua pepe na kufanikishwa chini ya uwezeshaji wa mtoa huduma

Namba za simu pamoja na mawasiliano yote yanayofanyika kupitia njia ya simu chini ya Kampuni zinazotoa huduma ya mawasiliano ya simu

Taarifa za Kibenki na miamala yote inayofanyika kupitia Taasisi za Fedha. Sheria itazitaka Kampuni husika kuhakikisha taarifa za wateja wao zinatunzwa

Taarifa za afya za Watu, taarifa hizi hukusanywa na Taasisi mbalimbali zinazotoa huduma ya afya pamoja na mashirika yanayotoa Bima za Afya

Data zozote ambazo ambazo watoa huduma hasa za Kibiashara wanakusanya na kuhifadhi kidijiti zinahitaji kulindwa vizuri. Katika mataifa yaliyotangua kuandaa sheria ya Ulinzi wa Data tayari wao wana muongozo wa njia bora ya kutunza na kutumia data wanazokusanya.

SHERIA

Sheria ya Ulinzi wa Data inaweka vigezo na muongozo wa namna bora Asasi za Kiraia, Serikali na Makampuni ya Biashara yanapaswa kuzingatia namna bora ya kutunza na kulinda taarifa/data za watu au wateja wao. Utunzaji unahusisha kuhakikihsa Data hizo ni Sahihi, Salama, na hazijavunjwa sheria.

Kanuni za utunzaji wa Data zinaeleza yafuatayo:

  • Data zinatumika kama ilivyoelekezwa
  • Data hazitunzwi kupita muda uliowekwa kisheria na bila ya ulazima
  • Zinatumika kwa usahihi
  • Zimetunzwa vizuri na kwa usalama
  • Zinatumika kwa kufuata sheria
  • Hazitumwi nje ya eneo la kiutawala bila ya kufuata kanuni nataratibu
 
Upvote 0
Perspectively kila aina ya data na jumuishi ya privacy ya mtu ni haki yake mwenyewe na inastahili kuheshimiwa, kuhifadhiwa na kulindwa.

Katika kila sector au hatua tanabiha za kimtandao na Kielektroniki, mawasiliano, uchukuzi, kifedha na matibabu na mfumo mzima wa ekolojia ya kimaisha ibaki stahiki rasmi ya mtumiaji na mwenyewe nayo. Kupitia 'Privacy Policy'

Ni wakati sasa kuanda na kutekeleza sheria za 'Data' katika nyanja zote hasa zinazomgusa mtumiaji moja kwa moja.

Ikiwa katika Afya, Mawasiliano, Mifumo ya kibenki na Kielektroniki mtandao haki hizi stahiki zikiyumbishwa basi watoa huduma wapambane na sheria zenye ncha mithili ya wembe.

Katikati ya matikiti basi nanasi haikosi, Mexence Melo ni mfano katika kusimamia, kuendesha na kutekeleza kwa kuhifadhi faragha na tanzu 'DATA' pasipo sheria ni mfano na sehemu ya kuanzia kwa wengine. Nanasi ni 'Catalyst' iliyoweza kuyamudu ma 'Water Melon'.

Hii ni 21st Century ukikubali kulaliwa mwisho wa siku utaliwa, jukumu ni lako sasa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom