bombu
JF-Expert Member
- Jun 8, 2011
- 1,127
- 542
Katika jamii nyingi za kiafrika hususani Tanzania, mwanaume ndiye huanzisha mahusiano kwa kumtongoza binti na hata kumchumbia kwa lengo la kuwa pamoja. Sasa inapotokea mwanaume/kijana akamtongoza binti bila kuweka bayana iwapo ana nia ya kumchumbia namaanisha anamuomba wawe wapenzi, na binti akaridhia (akiamini kuwa uchumba utafuata), na katika mahusiano hayo ukapita muda mrefu wa labda hadi miaka mitatu na kuendelea bila kijana wa kiume kutamka uchumba au nia ya kufunga ndoa.
Na katika mahusiano huui wawili hujikuta wanapata m/watoto na mwanamke huonekana kama hakuwa thabiti kwa kukubali kazaa na mtu ambaye hawajafunga ndoa (mtazamo wa jamii). Je, ni jukumu la nani kuhakikisha kuwa panakuwepo uhalalishwaji wa mahusiano (ndoa) kati ya mtu mume na mtu mke?
Na katika mahusiano huui wawili hujikuta wanapata m/watoto na mwanamke huonekana kama hakuwa thabiti kwa kukubali kazaa na mtu ambaye hawajafunga ndoa (mtazamo wa jamii). Je, ni jukumu la nani kuhakikisha kuwa panakuwepo uhalalishwaji wa mahusiano (ndoa) kati ya mtu mume na mtu mke?