Davidmmarista
JF-Expert Member
- Apr 11, 2024
- 1,367
- 2,451
Mdau karibu utuambie
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Dah pole sana mdauBàada ya kuhama mkoa na wazee wangu, nilikaa nyumbani kuanzia mwezi wa 5 mpaka mwezi wa 8 ndipo nikapata uhamisho, Nilihamishwa shule mwezi wa 8, mwezi wa tisa tukafanya mtihani na nikaongoza kwenye matokeo.
Ilikuwa gumzo shuleni pale.
Hiyo ilikuwa darasa la 5,
Taarifa mbaya sikumaliza hata darasa la saba kutoka na wazazi kupoteza maisha na familia kutawanyika
Hongera bro 🙌🏻🙌🏻Primary school nilikua na vichekesho sana mpaka namaliza la saba halaf nilikua sinaga akili. Vichekesho vilinipa umaarufu sana.
Secondary nilikua serious nikawa napiga sana misuli, nilikuaga top 3 mpaka naondoka form 4 na one kali. Akili zininifanya kuwa maarufu sana.
High school nilikuaga mkarimu sana, maana Boarding school ilikua mkoani kwetu hivyo mamaa na ndugu zangu walikua wanakuja sana kunitembelea na kuniletea mazaga, tranka yangu ilikua ni ta room members woote. Wakija wazee na mazaga ilikuaga bata kwemda mbele hata watu wa room zingine walikua wanakuja kwetu.
Nakumbuka graduation ya form 6 mama na mzee waliandaa party ya jamaa zangu woote wanne kwakua wao walikua wanatokea mikoa ya mbali. Ukarimu ulinifanya wengi kunifahamu , "aahh yule jamaa peace sanaa" ndio msemo uliokua unanitambulisha shulen
🤣🤣🤣Ujohn kisomo 1st form I-IV
Utoro tokea la kwanza mpaka cha six, yani nikienda skuli siku hio napongezwa na wanasema "leo Nomadix kaja mvua itanyesha"