Je, ni kwanini teknolojia mithili ya miujiza iitwayo ‘Neuralink’ haizungumziwi kabisa?

Je, ni kwanini teknolojia mithili ya miujiza iitwayo ‘Neuralink’ haizungumziwi kabisa?

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2013
Posts
38,920
Reaction score
44,970
Teknolojia hii inayohusisha kupandikiza kifaa kidogo mfano wa shillingi ndani ya fuvu ambapo viwaya vyembamba mara laki ya unene wa nywele, huchomekwa nankuungwa na neurons za ubongo, itawezesha binadamu kuzunguza kuwasiliana bila kufungua mdomo (sauti) wala kuandika (herufi). Teknolojia hii itawezesha watu kuendesha magari bila kushika usukani, kupiga simu bila kuwa na simu mkononi. Itawezesha kucheza game bila kushika contol, kubadilisha channel za Tv bila kushika remote control, kuwasha taa bila kubonyeza switch. Kuhamisha pesa bila kushika ATM kadi nk.

Hii inawezekana vipi? Ni kwamba utakuwa unaamrisha mifumo ya kidijitali kwa kuwaza tu (wireless transmission), yaani ukiwaza gari liwake, basi linawaka, ukiwaza taa ziwake, zinawaka, ukiwaza TV iwake , inawaka, ukiwaza unampigia simu nduguyo aliye marekani, hapo hapo unaanza kuongea nae, kwa kuwaza tu.

Watu wenye ulemavu wa kuparalyse watatembea, maana miguu yake itaendeshwa wirelessly kwa kutumia bypass ya Neuralink, vipofu wataona, nk, nk. Utaweza kudownload kumbukumbu zako zote na kuzisave kwenye backup server, na ukitaka kuzirestore unazirudisha endapo umesahau, au ukitaka unaweza kuinstall kumbukumbu zako kwenye ubongo wa mtu mwingine, mfano proffessor wa hisabati anaweza kudownload memory zake na kuziinstall kwenye ubongo wa mwanafunzi wake, na akawa proffessor ghafla!!!

Tayari mambo yameanza kuiva, kifaa hiki alifungiwa nyani miezi michache iliyopita, na akaweza kucheza game aina ya ‘mindpong’ bila kushika Joy stick, yaani aliicheza game kwa kuwaza tu. Nyani mwenyewe ndio huyo hapo chini.



INTERNET OF THINGS itaunganisha kila kitu na bongo za kila mtu na kuwa one consiousness, Fahamu moja, as if ni kiumbe kimoja!

=========================
Update: 27/05/2023


===========================
Update: 30/01/2024


View: https://www.instagram.com/p/C2uvtC5sM4n/?igsh=NTc4MTIwNjQ2YQ==
 
Teknolojia hii inayohusisha kupandikiza kifaa kidogo mfano wa shillingi ndani ya fuvu ambapo viwaya vyembamba mara laki ya unene wa nywele, huchomekwa nankuungwa na neurons za ubongo, itawezesha binadamu kuzunguza kuwasiliana bila kufungua mdomo (sauti) wala kuandika (herufi). Teknolojia hii itawezesha watu kuendesha magari bila kushika usukani, kupiga simu bila kuwa na simu mkononi. Itawezesha kucheza game bila kushika contol, kubadilisha channel za Tv bila kushika remote control, kuwasha taa bila kubonyeza switch. Kuhamisha pesa bila kushika ATM kadi nk.

Hii inawezekana vipi? Ni kwamba utakuwa unaamrisha mifumo ya kidijitali kwa kuwaza tu (wireless transmission), yaani ukiwaza gari liwake, basi linawaka, ukiwaza taa ziwake, zinawaka, ukiwaza TV iwake , inawaka, ukiwaza unampigia simu nduguyo aliye marekani, hapo hapo unaanza kuongea nae, kwa kuwaza tu.

Watu wenye ulemavu wa kuparalyse watatembea, maana miguu yake itaendeshwa wirelessly kwa kutumia bypass ya Neuralink, vipofu wataona, nk, nk. Utaweza kudownload kumbukumbu zako zote na kuzisave kwenye backup server, na ukitaka kuzirestore unazirudisha endapo umesahau, au ukitaka unaweza kuinstall kumbukumbu zako kwenye ubongo wa mtu mwingine, mfano proffessor wa hisabati anaweza kudownload memory zake na kuziinstall kwenye ubongo wa mwanafunzi wake, na akawa proffessor ghafla!!!

Tayari mambo yameanza kuiva, kifaa hiki alifungiwa nyani miezi michache iliyopita, na akaweza kucheza game aina ya ‘mindpong’ bila kushika Joy stick, yaani aliicheza game kwa kuwaza tu. Nyani mwenyewe ndio huyo hapo chini.



INTERNET OF THINGS itaunganisha kila kitu na bongo za kila mtu na kuwa one consiousness, Fahamu moja, as if ni kiumbe kimoja!

Lakini pia papo hapo ndio utakuwa mwisho wa privacy.
 
Usitulemazie akili zetu sisi hebu toka hapa!
Mznwyuu! Tena kweli bhana. Hili ndo kosa kubwa la wasomi wa siku hizi eti kila kitu wana-Google badala ya kuchemsha akili kwanza. Akili wanazipeleka fasta kule kwenye End of thinking capacity mapema mno - yaani Uwezo wa akili bado haujaisha lakini wao wanawahi kule kwenye etc. 😳 😂
 
Mznwyuu! Tena kweli bhana. Hili ndo kosa kubwa la wasomi wa siku hizi eti kila kitu wana-Google badala ya kuchemsha akili kwanza. Akili wanazipeleka fasta kule kwenye End of thinking capacity mapema mno - yaani Uwezo wa akili bado haujaisha lakini wao wanawahi kule kwenye etc. 😳 😂
Hivi nyie mnachangia uzi huu au mnachangia mwingine?
 
Dunia inaenda kasi sana. Mambo ambayo huwezi hata k uwaza kua yanawezekana ndo yanafanyika kabisa.

Ila huwa nikiangalia movie za wenzetu hata hizi za drama/comedy/adventure ambazo zinaonesha uhalisia wa maisha yao achana na hizi sci-fi.
Kwao tech imerahisisha sana maisha aisee kuliko huku kwetu ambako internet tu ni bonge moja tatizo.
 
Dunia inaenda kasi sana. Mambo ambayo huwezi hata k uwaza kua yanawezekana ndo yanafanyika kabisa.

Ila huwa nikiangalia movie za wenzetu hata hizi za drama/comedy/adventure ambazo zinaonesha uhalisia wa maisha yao achana na hizi sci-fi.
Kwao tech imerahisisha sana maisha aisee kuliko huku kwetu ambako internet tu ni bonge moja tatizo.
Na ukifuatilia utakuta sci-fi nyingi zimekuja kuwa kweli
 
Hivi nyie mnachangia uzi huu au mnachangia mwingine?
Ni huu huu mkuu unaohusu tech ya "Neural link". Hapo Mkuu ni kwamba, Watu wanakimbilia ku-Buy hiyo teknolojia (kushabikia)kabla hawajabaini na kujiridhisha kuhusu Faida na Madhara/Hasara yake kwa binadamu hususan sie ambao tech. yetu bado ni changa au ni ndogo ref. Mtoa mada anahoji kwanini haizungumziwi. Wanazungumza tu yale mazuri(Faida) kwamba utaweza hiki, utaweza kufanya kile n.k. n.k. Lakini hatujaweza kuona kwamba kama kompyuta inapata virusi na inafikia mahali lazima ukanunue ant-virus, Je, itakuwaje kama ni Ubongo ukiingia virus? Hatujaweza kuhakikisha pasi na shaka kwamba hiyo imekaa kiBiashara au kiUchumi au ki-Usalama(Security) au ndo wanataka kutugeuza maZombie? Tafakari. Watu wameinyamazia Tech. hiyo ili kupata muda wa kuisikilizia na kuitafakari. Ni hayo tu.
 
Back
Top Bottom