Je, ni kweli biashara ya usafirishaji wa abiria Dar - Zanzibar inapaswa kufanywa na wazawa wa visiwani pekee?

sawariya

JF-Expert Member
Joined
Apr 9, 2015
Posts
382
Reaction score
350
Salaam,

Naomba kwa yeyote mwenye kufahamu suala la biashara ya usafirishiji abiria wa kutoka Dar kwenda Zanzibar ipoje?

Ni mtu yeyote anaruhusiwa kuifanya hii biashara? Maana kuna tetesi kuwa biashara ya usafirishaji wa abiria Dar to Zanzibar wanaoruhusiwa ni watu wa visiwani tu, wabara hawaruhusiwi kuigusa hii biashara. Ukweli ukoje hapo?

Nawasilisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kaka unataka kupeleka ule mtumbwi ha ha ha sio kweli broo


Sio comment ya hapa hina Uzi wake
 
Kama unavyombo vya usafiri nenda kaione mamlaka inayohusika wakijilizisha kama umekamilisha vigezo utaruhusiwa

But umejipangaje kiushindani? Unaboat za kisasa kumchallenge Azam?
Anyway kila la kheri mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtu yeyote anaruhusiwa, ila boti nyingi zifanyazo kazi hizo zimesajiliwa upande wa Zanzibar ambapo kuna Open registry hii inamruhusu mtu yeyote kusajili meli hata kama si mzawa na haina masharti magumu kama closed registration tuliyonayo huku bara ambayo kuna kigezo cha kuwa mzawa au ukifanya sharing na watu wa nje lazima uwe na asilimia 50 ya share za umiliki wa kampuni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…