Je ni kweli club ya Simba inahitaji mageuzi katika mfumo wa uendeshaji?

Hii issue sio ya kukurupuka kama wengi wanavyofikiria, Simba/Yanga wana advantage ya kuwa na fan base kubwa lakini viongozi hawajafanya lolote kuwashawishi wapenzi na mashabiki kuwa wanachama.Hivi Yanga/Simba wana wanachama ambao wanaishi Pemba,Mbinga,Sumbawanga au Kigoma ?

Kama zingeweza kuwashawishi/kuhamasisha wapenzi na mashabiki wao wakajiunga kuwa wanachama Tanzania nzima na wote wakashiriki uendeshaji wa klabu tayari wangekuwa level nyingine. Kama wapenzi/mashabiki wanaweza kulipia viingilio uwanjani au kwenye TV je wangeshindwa kulipia ada ya uanachama ?

Assume Simba/Yanga ina wanachama hai 100,000 na walipe ada ya uanachama kwa mwaka (mfano 10,000),Kwa mwaka klabu inaweza kuingiza 1,000,000,000 (bilioni moja ),na kama klabu itawatumia vizuri hao wanachama na kutengeneza bidhaa mbalimbali(jezi,skafu,key holders,kalenda,gazeti) za klabu na kuwauzia wanachama huoni kwamba klabu itakuwa imepiga hatua
 
Kwanini usiwe muwaz tu kuwa uongoz ulioko madarakani ndo tatizo kwa simba? Kabla ya hawa watu mbona simba ilikuwa poa?
Endelea kusoma maoni yangu utanielewa sijasema huu uongozi ni mzuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…