Pole sana mkuu aliyeseam ujanja kupata si kuwahi alikuwa na maana sana. Tanzania imekuwa corrupted na siasa. Miaka sisi tunasoma ilikuwa kubakizwa kuwa mwalimu wa University ni big deal na wengi walikuwa wanaishi maisha mazuri sana na yenye mafanikio. Kinachoua elimu Tanzania ni greed ya wanasiasa siku hizi utakuta mshahara wa mwanasia mwenye elimu ya darasa la saba aliyejipachika katika nafasi ya uongozi kwa uwezo wa kuchonga mdomo na kusifia waliopo juu yake anaishi maisha ya hali ya juu sana. Ndiyo maana ukiangalia watu wanakimbia chaki madarasani na kukimbia profession zao kuingia kwenye siasa na kugombea ubunge.
Wanasiasa wanajilimbikizia malipo ya kufuru huku watu waliotumia muda wao kusoma kwa ajili ya Taifa wakibakia kuwa ombaomba na watu wa kujipendekeza kwa wanasiasa wenye elimu duni dhidi yao. Nchi yetu imekuwa haiheshimu tena wataalam ndiyo maana wengi wa wataalam wame-compromise taaluma kwa kuwasikiliza wanasiasa wenye uelewa finyu na hata wakati mwingine kudiriki kuwafuata wanavyotaka mradi tu wasipoteze nafasi za kupata hata hicho kidogo.
Bado ninaamini kabisa kama tuna nia ya kuwa-retain watu kama wewe kwenye elimu ya juu tunatakiwa kuwaonesha kuwa education pays. Otherwise sooner or later utajikuta na wewe unapata mawazo ya kupanda jukwaani na kuizika taaluma yako, matokeo yake taifa linazidi kushuka chini. Tokea kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi kumekuwa na ongezeko kubwa sana la wanataaluma kuingia kwenye siasa maana ndipo kunalipa kwa sasa. Ukiangalia baadhi ya taaluma za wabunge waliopo bungeni leo utaona kuwa unaweza kutoa Univeristy moja yenye kukamilika kwenye kila nyanja kwa jinsi wanataaluma walivyojikita huko.
Lakini hata hivyo usikate tamaa, kama una PhD unaweza tafuta kazi nchi zinazothamini elimu kama Botswana na hata Rwanda na kujikuta miaka yako mitatu tu unakuwa sawa na wale uliomaliza nao undergrad. Wao wansisitiza uzalendo huku wakijilimbikizia, its time sasa na wewe kutafuta sehemu muafaka nchi ikitengemaa utarudi kuijenga.
Wanasiasa wanathamini wale watu wanaofanya na kudumisha uwepo katika madaraka kama vile majeshi, polisi tena wale wenye vyeo vya juu. Mwalimu kama wewe unaonekana si lolote kwani suala la elimu bora au duni haliathiri madaraka yao. Mkianza kukimbilia kwenye nchi zenye masilahi kwa wenye taaluma huenda watastuka.
Bonus video hiyo chini, ukiwa na taaluma ni kama vile huyo mwenye convertible car body, hata mtu akikuwahi vipi utapark gari na kumuacha akihangaika kutoka.