Damaso
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 3,978
- 6,739
Habari, nimepata taarifa kuwa mtu akioga maziwa fresh kutamsaidia sana kwenye afya yake ya ngozi. Maziwa ya wanyama kama Punda, Farasi, Ngamia, Mbuzi na Ng'ombe ni tiba nzuri ya ngozi.
Pia kuna sehemu nimesoma kuwa Malkia wa Misri, Cleopatra alikuwa na kawaida ya kuoga maziwa ili apate ngozi yenye afya. Je ni kweli kuhusu jambo hili? Na maziwa yana kitu gani cha upekee mpaka yawe sehemu ya kutumika katika kuimarisha ngozi?