Je ni kweli maisha ya Ulaya na Marekani ni magumu au ni mwendelezo wa ngozi nyeusi kukatishana tamaa?

Braza Kede

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2012
Posts
3,840
Reaction score
6,844
Wakuu mengi yanazungumzwa kuhusu uzuri na changamoto za maisha ya Ulaya na Marekani.

Wengi wetu tunaamini huko ndo watu wanaishi na sisi wengine huku ni wasindikizaji tu ila kuna wengine wanadai eti maisha ya huku bongo ndo mazuri kuliko huko ng'ambo.

Wakuu ukweli uko wapi maana mwenzenu nshachoka na hizi sarakasi nataka nifanye maamuzi magumu.
 
Inasemekana huli bila kufanya kazi, hakuna mtu anakusaidia au kwa lugha nyingine (anakuungia) ukiwa umekwama au huna. Ni wachoyo na wabinafsi vibaya mno!

Maisha ni ghali na kila kitu kiko systematic. Huwezi kukwepa kodi, internet, sijui maji na huduma zinginezo za kawaida na zisizo za kawaida.

Kuanzisha kampuni au biashara ni very long and complicated proccess hasa ukiwa sio raia au huna makaratasi.
 
true kiongozi
 
Parachichi 1 ni elfu 50 Sasa pima mwenyewe
 
yeah haya nshayaskia sana. laifu ni expensive hakuna kugongea wala uchawa. hakuna wa kupiga naye stori yani we unakuwa men alone kwa 100%.inasemekana wengi wanakata moto kwa upweke.
 
Za kuambiwa changanya na zako.
 
Mkuu uko tayari kukabiliana na Trump ? Maana nyie ndio anawaita wahamiaji haramu. Yaani ukiwa huko huna tofauti na πŸ–πŸ·πŸ½ akiwa Zanzibar
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…