Shida sio kulalamika, mimi ni miongoni mwa wanataka ada irudishwe ili kuboresha elimu. Hata hivyo na ijulikane wazi kuwa ada haijafutwa ila imebadilishwa jina tu.Haani mtanzania wanapenda kulalamika hovyo mwaka mzima ulipie 6500 kwa form 5 na 6. Unaona kama hiyo ni ada pumbavu.......mawazo ys kimasikini ni ysmasikini siku zote.
Tuongeeni ukweli aisee...Ile 70k haiboreshi chochote kwenye elimu.Shida sio kulalamika, mimi ni miongoni mwa wanataka ada irudishwe ili kuboresha elimu. Hata hivyo na ijulikane wazi kuwa ada haijafutwa ila imebadilishwa jina tu.
DahHeshima kwenu,
Serikali ya awamu ya sita ilitangaza kufuta ada kwa kidato cha 5 na sita kwa shule za serikali ambayo ilikuwa ni shilingi 70,000/=.
Nimepitia fomu za kujiunga na kidato cha 5 mwaka huu 2023. Kuna mchango mpya umeanzishwa unaoitwa mchango wa uendeshaji wa shule kiasi cha shilingi 65,000/=. Hii ni sawa na kisema serikali haijafuta ada bali imeondoa shilingi 5,000/= tu kwa kila mwanafunzi.
Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan hili unalitambua? Waheshimiwa mawaziri wa Elimu na TAMISEMI hili lina baraka zenu?
Semeni ukweli kwa Watanzania.