Je ni kweli?

Je ni kweli?

Chapakazi

JF-Expert Member
Joined
Apr 19, 2009
Posts
2,874
Reaction score
316
Mimi sio mwenyeji wa hili jukwaa, lakini napitapita mara kwa mara angalau kusoma mada.
Juzi w/end nilikuwa kwenye kasherehe na vijana wenzangu kutoka mataifa mbalimbali ya Africa (sana Zimbabwe). Mazungumzo yalielekea upande wa ukabili uliopo Zimbabwe - hasa hao Washona na Wandebele. Katika kundi letu kulikuwa na binti mmoja wa ki-asia anaye-mdate mwanaume wa kindebele. Kwa maoni yake, wasichana wa Kizimbabwe hawampendi kwa vile wanaona anachukua mtu wao. Msichana mmoja (mzuri tu) wa kizimbwabwe akasema kuwa wasichana wa kiafrica hawapendi wanaume wa kiafrika wakichukua mataifa mengine. Hii ni sababu ni ngumu kwao (wasichana) kupata mwanaume wa taifa lingine hasa wazungu.
Hii pointi ilinishangaza sana na nimeona niulize hapa kama ina ukweli wowote. Msichana huyu alisisitiza point na kusema hii ni zaidi kwa wasichana walio na very dark skin. Je ni kweli? Je tunahitaji kubadilisha mind-set zetu?
 
Mie binafsi sipendi kabisa nikiona dada zetu wanachukuliwa na hao ngozi nyeupe
 
Hisia zako zinakuambiaje? Hicho unachohisi ambacho hutaki kusema ndio ukweli mtupu...!
 
I cant speak for everyone ila for me unless kama I have some sort of interest on the said guy, then I could careless who he dates and whatnot. Ila kama I like the guy, then the presence of a girl, be it "white" or "black" may bring this sense of disappointment, and/or "kijiwivu" that he is taken,and all that lakini si chuki.
 
Hisia zako zinakuambiaje? Hicho unachohisi ambacho hutaki kusema ndio ukweli mtupu...!

Mimi kweli im indifferent! Kama demu anampenda jamaa kwa dhati au jamaa anampenda demu kwa dhati, hiyo ni haki yao. Mimi binafsi siwezi kuoa mzungu kwa vile naamini marriage lazima m-share kitu kikubwa kinachowaweka pamoja. Na hii nimeona hata kwa wazungu waliokulia africa na wanajiita waafrica. Lakini ikifika kwenye ndoa, utaona anaoa mzungu. It used to bother me, lakini kwa sasa naona ni sawa tu. Kinachonisikitisha nii hii mentality ya hawa wasichana. Kwa namna moja au nyingine anaweza kujiona inferior! Na hilo ni tatizo kubwa sana!
 
Mie binafsi sipendi kabisa nikiona dada zetu wanachukuliwa na hao ngozi nyeupe

Kwa nini mkuu? Kuna wale ambao unaona kabisa hakuna kitu hapo. Unakuta mtu anafanya kazi ya ziada katika ku-maintain hiyo relationship!
mimi kwanza naona mara nyingi wasichana wa kizungu wanaona kama vile sisi waafrika tunawataka wao tu! sijui hiyo mentality wametoa wapi.
kuna siku natembea kurudi nyumbani usiku na demu wa kizungu anatembea mbele yangu. Wacha aogope. Kwa bahati mbaya tulikuwa tunaelekea njia moja. Si akadhani ninamfuata. Akaita polisi....
nilimmaindi huyo polisi na kuanza kumtukana. Alafu eti akanitisha atanikamata. Hajui sie tumebobea kwenye sheria! Nikamwambia twende...
 
Sioni kwanini mtu awe na tatizo na kitu kisichomhusu!!!Kwani asingekua na huyo mzungu ndo angekua nae??!Ni ulimbukeni tu unawasumbua!!
 
Sioni kwanini mtu awe na tatizo na kitu kisichomhusu!!!Kwani asingekua na huyo mzungu ndo angekua nae??!Ni ulimbukeni tu unawasumbua!!

Nadhani ukichukulia context ya kuwa mbali na nyumbani...anaweza kuwa na madai/wivu sahihi? Maana huku tunaweza kusema market imepungua. Tuseme kama wewe binafsi unaishi sehemu yenye watz au waafrika wachache. Alafu katika hiyo limited market ukute mtu anachukua au anachukuliwa na mzungu! Siyo sahihi kuwa na wivu au tatizo na hilo?
 
Nadhani ukichukulia context ya kuwa mbali na nyumbani...anaweza kuwa na madai/wivu sahihi? Maana huku tunaweza kusema market imepungua. Tuseme kama wewe binafsi unaishi sehemu yenye watz au waafrika wachache. Alafu katika hiyo limited market ukute mtu anachukua au anachukuliwa na mzungu! Siyo sahihi kuwa na wivu au tatizo na hilo?
Labda kama huyo dada alikua interested na kaka tangu mwanzo...and even if that was the case still hana haki ya kukasirika kisa kachukuliwa mzungu!!!Zaidi ya hapo bado sioni huo usahihi unatoka wapi...unless huyo kaka nar amependa rangi na sio mtu ndo naweza kuelewa akisema kitu kama hathamini vyakwao ila kama kampenda mtu basi kampenda....huyo dada nae atafute mzungu wake!!!

Na ukichunguza sana utakuja kugundua kwamba huyo dada hata akiona weusi wawili bado roho itamuuma kwasababu yeye hana wake...kwa mzungu katumia tu kisingizio cha bei rahisi kuonyesha chuki yake kwa mwanamke mwingine yeyote yule aliyebahatika kupata ampendae!
 
Labda kama huyo dada alikua interested na kaka tangu mwanzo...and even if that was the case still hana haki ya kukasirika kisa kachukuliwa mzungu!!!Zaidi ya hapo bado sioni huo usahihi unatoka wapi...unless huyo kaka nar amependa rangi na sio mtu ndo naweza kuelewa akisema kitu kama hathamini vyakwao ila kama kampenda mtu basi kampenda....huyo dada nae atafute mzungu wake!!!

Na ukichunguza sana utakuja kugundua kwamba huyo dada hata akiona weusi wawili bado roho itamuuma kwasababu yeye hana wake...kwa mzungu katumia tu kisingizio cha bei rahisi kuonyesha chuki yake kwa mwanamke mwingine yeyote yule aliyebahatika kupata ampendae!

huyu demu wa kizimbabwe alisema hiyo as a general statement! Sio kwamba yeye ndio mwenye wivu! Na kwa madai ya pili kuwa ni vigumu kwa wanaume wa kizungu kutoka na wasichana wa kiafrika...yana ukweli?
 
huyu demu wa kizimbabwe alisema hiyo as a general statement! Sio kwamba yeye ndio mwenye wivu! Na kwa madai ya pili kuwa ni vigumu kwa wanaume wa kizungu kutoka na wasichana wa kiafrika...yana ukweli?
Kama asingekua n chuki asingesema hivyo!!!Nwy sioni ukweli wowote maana wadada kibao nao wako na wazungu!!!
 
Kama asingekua n chuki asingesema hivyo!!!Nwy sioni ukweli wowote maana wadada kibao nao wako na wazungu!!!

hawezi kuwa na chuki kwa sababy hamjui huyo mwanaume! ni kweli kuwa kuna wasichana wapo na wazungu...lakini swali linabaki ni ngumu?
 
penzi halichagui rangi,dini, kabila, kimo au baraunalotokea achia mbali nchi au kijiji...
 
Back
Top Bottom