Je ni sahihi kulipa hii faini?

super cup

JF-Expert Member
Joined
Oct 16, 2012
Posts
212
Reaction score
91
Jana wakati natoka zangu mkoa narudi jijini nikiwa na drive nikapigwa tochi kwenye limit speed ya 50km/hr, Mimi nikiwa na speed ya 58km/hr, nikaja kukamatiwa mbele. Askari akanisimamisha na kunionyesha picha.

Kuangalia picha ina mawingu haioneshi plate number ya gari, nikamuambia hii sio gari yangu. Gari yangu ina usajili wa T001 WET, hebu soma plate number ya gari kwenye hiyo picha yako akashindwa kusoma.

Akakomaa kuwa ananiandikia hivyo nitajikuta nadaiwa nikanyamaza, kwa vile alikuwa amechukua leseni yangu toka mwanzo akaipiga picha akapiga na plate no ya gari akanirudishia leseni akaniambia naweza kuondoka.

Nilipofika home jioni nikacheck deni la gari online nikakuta kweli jamaa ameniandikia faini?

Je ni halali kweli mimi kulilipa hili deni?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usilipe nenda kwa RTO

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi unaangaliaje online deni??
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unalipa kwa control number ipi kama hauna risiti?
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…