Kwa mimi niliyelelewa kijijini huko ndani ndani kabisa, hilo unalouliza haliwezekani, ukweni ni sehemu inayoheshimika sio mchezo, ukienda ukweni unaenda kwa shida maalumu, kama ni kusalimia ni kwa siku maalumu sio kila siku.
Aisee kabila langu lina mambo sio mchezo, huwezi kumsalimia mama mkwe kwa kushikana nae mkono.
Yaani masharti ni magumu mnooo japo nayaona yana maana ya kuweka distance ya kudumisha heshima baina na mtu na wakwe zake.
Maajabu nayaona mjini Dsm ukweni wengi wetu tunachukulia poa tu, any time mtu anapita anakula, anakunywa anasepa, wengine wanahamia kabisa ukweni.
Utasikia aisee baba mkwe kanipa chumba pale nikae maana saivi mambo yangu magumu kidogo
Kudadeki sisi kwetu hakuna hiyo, kama mambo yako magumu tafuta kwingine sio ukweni maana hata mkeo na shemeji zako watakushusha heshima