Je, Ni tatizo? Nifanyaje?

Please please! Huo ukoo una matatizo! Kwa nn unataka kujitwisha matatizo hayo? Nakushauri achana nae, tafuta msichana mwingine tulioko pwani tunayajua matatizo hayo. Utakuja kujuta maisha yako yote!
 
nashukuruu mkuu kwa mawazo yako
Please please! Huo ukoo una matatizo! Kwa nn unataka kujitwisha matatizo hayo? Nakushauri achana nae, tafuta msichana mwingine tulioko pwani tunayajua matatizo hayo. Utakuja kujuta maisha yako yote!
 
Kuwa mwanaume kijana! Suppose, umejiandaa kwenda kazini halafu yy hapohapo anazimia? Utakuwa unasubiri azinduke? Wastage of time! Ana ndugu zake let them care for her!:angry:
 
kama unaona mzigo huo utuweza, basi piga moyo konde endelea nae na udumu katika maombi
kama unaona hautauweza,basi si mbaya ukamwambia ukweli mapema na sio kumpa mahope afu dakika za mwisho ukambwaga.
 
Najua wengi jukwaani wataponda kwa sababu za ubinadamu, ila ukweli ni kwamba kama una akili timamu hautamuoa huyo binti. Kwanza nikuhakikishie kwamba kuna uwezekano huyo binti ana/atakula dawa maisha yote, na mamaye pia! Pili, research imeonyesha link kati ya kifafa na ku-develope dalili za uchizi(psychosis). Tatu, psychosis may run in families, so wahurumie wanao watarajiwa. Trust me, I am a Doctor! 🙂
 
pole sana kaka, inaonekana una mapenzi ya dhati kwa huyo dada. Sasa cha kufanya, mchukue huyo dada muende naye hospitali ya maana wasema inakuwaje, na pia wewe binafsi utafute muda ukaonane na daktari umuelezee majibu mliyoyapata huko ili akueleze kama itaathiri uzao wako au la. Baada ya kujiridhisha na vipimo na majibu ya daktari ndipo utafanya uamuzi wa kuwa naye au la.
 
Wewe fikiria mwenyewe ufanyaje, amekuwa mkweli kwako, je angekuficha ukajajua baadae au kupitia kwa wambeya ingekuwaje, na kama unataka kumtosa, mtose kwa namna nyingine, hata kwa kupunguza naye mawasiliano, sio mpaka ashtukie reasonau kama vipi mpeleke kwenye maombi, ataachwa na wangapi my Bro?!
 
Wewe fikiria mwenyewe ufanyaje, amekuwa mkweli kwako, je angekuficha ukajajua baadae au kupitia kwa wambeya ingekuwaje, na kama unataka kumtosa, mtose kwa namna nyingine, hata kwa kupunguza naye mawasiliano, sio mpaka ashtukie reason au kama vipi mpeleke kwenye maombi, ataachwa na wangapi my Bro?!
 
hiloo nenoo ''ataachwa na wangapi>>>najua nikianza kupunguza mawasiliano atajuaa sababu ni hiyo,naofiaa kumvunjaa moyo.rohoni nahisi hurumaa
 
mkuu hana kifafaa anazimia
 
Hujafa hujaumbika!
Mzima wa leo, kilema wa kesho!
Wewe kuwa mzima si juhudi zako binafsi au wazazi wako!
 
She is your wife from heaven
 
unaweza usimuoe kwa sbb kuna walakini tayari!!unaonaje ukimfanye dada wa hiari!naona ni mtu mwema kwako!!au mpeleleze kujua kama anachokisema ni kweli labda anataka kuona msimamo wako uko vipi!
 
Duh inasikitisha ndugu
Maana kwa akili ya kibinadamu ni ngumu sana sana kuamua hii, kuna uoga wa kuwa nikimuacha niweza kupata shida baadae au kupata mwingine aliye na tatizo kubwa zaidi ya hili, au nikiendelea kuwa naye matatizo nikayokabiliana nayo hata kwenye kizazi chako kijacho.

Kama we ni mtu wa imani basi nakushauri muombe sana Mungu katika hili, na mwisho utapata jibu la mwisho na utapata kuwa amani na ili usije kuwa unajutia kila mara. Lakini hata ikiwa hutakuwa naye kama mke basi endelea kuwa mtu wa karibu kwake.


Kila la heri kaka.........
 
hmm jaman kweli kuna mengi dunian..msaidie tu huwezi jua jicho la mungu linakuangalia kiasi gan....atakuepushia na hayo unayohisi yatakuja tokea
 
Yani leo nimekuwa katika wakati mgumu kushauri,huruma imenijia nashindwa nianzie wapi. Ila na kushuri umsaidie kwanza huyo binti kwakweli umetuweka katika wakati mgumu sana.thread yako ni ngumu sana ndugu. Naomba ujaribu kumpeleka hospital kwanza apate vipimo.

Ndugu mkuyati unaonekana una roho ngumu sana,piga picha haya matatizo yangekukuta wewe,alaf watu wana mshauri mtu wako akuache.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…