Aisee, pole sana n hongera sana kwa moyo wako wa huruma na ukarimu na wa upendo juu ya binti tajwa.Nimesoma comments zote nimeweza kugundua kuwa wewe na binti tayari mlisha fanya mapenzi, wakati mlipoonana. na hili umelisema uliposema you had good time together.
Pia nimegundua kuwa bint yuko muwazi sana kwako na wewe binafsi moyo wako umefunguka sana kwake kiasi kwamba now you feel guilty of breaking up, na siyo hilo tu bali pia bali unamuwazia ataachwa na wangapi, na unahofia akieza soma hisia zake kuwa sababu ni hayo matatizo basi ataumia sana.
By considering all these facts kwanza naomba nijaribu kubuni familia hii inatatizo gani. Yawezekana kabisa hii familia ina ugonjwa wa kifafa, kitaalamu huitwa seizure disorder. tatizo hili laweza kuwa pronounced under the following headings:-
•Nervous system conditions -hizi hushambulia mfumo wa ufahamu hasa nerves na neurones
•Seizure conditions -hiki huwa ndio typical kifafa chenyewe
•Brain conditions- hii hushambulia zaid ubongo
anyway am not a doctor but just giving you a lead.
sasa kutokana na hayo symptoms na treatment waweza kuzijua vizuri utakapomwona Dr kwani nikiandika hapa ni ndefu sana. Kutokana na hali halisi magonjwa kama ya kuzimia na kichaa ni possible kabisa kwa hii familia na ukisoma vizur you will understand what i mean.
Back to the point, nikirejea nyuma katika maelezo yangu ya awali, na kwa kuconsider factors zote sisemei ushabiki na niko radhi kupingwa she is your true wife. sina cha kuongeza zaid ya hapo.
ushauri mpeleke hosp akapimwe vizuri ili ujue wawezaje kujikinga na madhara ya baadae. Kurith kwa wanao au la kunategemea mambo mengi pia. Pia wewe mwenyewe assess ukoo wako kama kuna vichaa, au watu wenye vifafa basi usioane na huyu binti manake hapo unaongeza risk ya kuzaa disabled kids ila kama hamna its not a big deal as you can work on the matter before. siku hizi technology imepanuka sana ukimuoa na b4 conception mkaenda kwa dr atawashauri na hata mwez wa kwanza wa conception pia atawashauri nini cha kufanya ili kuwakinga wanenu na possible effects.
....kwa nini anazimia? kichaa sijui upo wapi ila huku ughaibuni watu wanaishi normal sema wanahitaji long term medication to control it...kama upo bongo nadhani upige mahesabu ya kulipia hayo madawa ya kucontrol kichaa chake...na pia kuna chance ukarithishisha wanao,chance ni 50,50......sasa wewe mwenyewe weigh the risks uone kama utaweza kuubeba huo msalaba ama la....
Yani leo nimekuwa katika wakati mgumu kushauri,huruma imenijia nashindwa nianzie wapi. Ila na kushuri umsaidie kwanza huyo binti kwakweli umetuweka katika wakati mgumu sana.thread yako ni ngumu sana ndugu. Naomba ujaribu kumpeleka hospital kwanza apate vipimo.
Ndugu mkuyati unaonekana una roho ngumu sana,piga picha haya matatizo yangekukuta wewe,alaf watu wana mshauri mtu wako akuache.
hmm jaman kweli kuna mengi dunian..msaidie tu huwezi jua jicho la mungu linakuangalia kiasi gan....atakuepushia na hayo unayohisi yatakuja tokea
unaweza usimuoe kwa sbb kuna walakini tayari!!unaonaje ukimfanye dada wa hiari!naona ni mtu mwema kwako!!au mpeleleze kujua kama anachokisema ni kweli labda anataka kuona msimamo wako uko vipi!
Duh inasikitisha ndugu
Maana kwa akili ya kibinadamu ni ngumu sana sana kuamua hii, kuna uoga wa kuwa nikimuacha niweza kupata shida baadae au kupata mwingine aliye na tatizo kubwa zaidi ya hili, au nikiendelea kuwa naye matatizo nikayokabiliana nayo hata kwenye kizazi chako kijacho.
Kama we ni mtu wa imani basi nakushauri muombe sana Mungu katika hili, na mwisho utapata jibu la mwisho na utapata kuwa amani na ili usije kuwa unajutia kila mara. Lakini hata ikiwa hutakuwa naye kama mke basi endelea kuwa mtu wa karibu kwake.
Kila la heri kaka.........
Hujafa hujaumbika!
Mzima wa leo, kilema wa kesho!
Wewe kuwa mzima si juhudi zako binafsi au wazazi wako!
unamaanishaa?mkuu najua na ndo kitu kinanipaa ugumu katika moyo wangu,leo na mkimbia yeye ila kesho yananikuta makubwaa zaidi kwanngu,pia na fikiria kuhusu feture yangu kama kijana ambae ndo naaza maisha itakuwa vipi?asee naombaa mungu sana
dah!!sio bange ni kitu cha kwelii na kinaniwekaa katikaa wakati mgumu sanaa,nashindwa kuamuaa,baada ya kufikiria mabange nipee mawazo bana smile
habarii wakuu wa mji huu, ma greater thinker ngoja nitiririkee moja kwa moja kwenye point...
Mienzi kama miwili iliopita nikiwa kwenye pilika pilika zangu nilikutana na binti kweli ni mrembo na alinivutia,nikatupaa ndoano akanikubali, kwakuwa nilikuwa kibiashara nilivyo maliza kazi ilio nileta niliondoka,ila kwa makubaliano tutaendela kuwasiliana ili yeye anifate huku mkoani kwangu, katika mazungumzo ya kuendelea kujuanaa, katika kumpeleleza yule binti aliniambia yeye hakusoma sana, na alishindwa kumalizaga shule, katika kutaka kujua why? Akaniambia alikuwa na matatizo ya kuzimia mara kwa mara so alishindwa kusoma, nikahojii vipi hayo matatizo ameenda hospital akaniambia ameangaika sana kwa miaka minne haja pata ufumbuzi, nikahojii vipi bado anaazimia hadi leo, akanijibu ndio ila hajazimia siku nyingi,nikaona oky siombaya labda naweza kumsaidia kwa kuenda nae maombi au kutafta tiba mbadalaa sikujalii sana.
Juzi nilimpigia simu asubui nikitaka kujua halii yake,ndipo akaniambia huko kwao mambo sio mazurii,kwanii mama ake anaumwa, nikahoji nini zaidi akaniambia mama ake anaugonjwaa wa kichaa ambao unamtokea agaa mara kwa maraa,nilistukaa ila sikuonyeshaa kama nimestukaaa.
Sasa wakuu ni hivi nimeskiaga magonjwa kama hayo mara nyingi yanarithiwa kizazi kwa kizazi, je nikimuowa huyo binti sitakuwaa na tatizo kwenye uzao wangu? Pia halii ya huruma inanijiaa naona hurumaa kumwambia siwezi kuwa nae kwa ajili ya hivyo vitu, je nifanyajeeee?
Mchango wenu wakuu na uhitaji sana.
MKUU KAMA UMEDANDIAA TRENI VILE...kwani mtu wakuowaa unazaliwaa nae au?maana najua hata baba na mama ako walikutana kwanza wakajuana ndio wakaowana,sa bilaa kukutana na kufahamiana utamuowaje,pole kama nimekukeraUngejua kwamba Mwanamke akiolewa haachwagi usingeuliza huu ujinga, mtu mmekutana tu wawaza kuoa! *****