Je, ni vitu gani ambavyo umezoea na unajua kuwa ni hatari kwa afya yako?

Je, ni vitu gani ambavyo umezoea na unajua kuwa ni hatari kwa afya yako?

Hamza Nsiha

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2022
Posts
221
Reaction score
197
Ni dhahiri kuwa kuna vitu vingi ambavyo watu wengi huwa tunapenda kuvipuuzia lakina ki_uhalisia ni vitu vyenye kuleta athari kubwa katika afya zetu.

Baadhi ya vitu hivyo ni kama vile:
  • Kukata matunda, na kuyaacha kwa muda fulani. Nadhani umewahi kukutana na sehemu ambazo wanauza matunda yakiwa tayari yamekatwa halafu yakawekwa katika vifungashio tayari kwa kuliwa. Endapo yataachwa kwa muda mrefu bila kufunikwa ni dhahiri kuwa yanaweza kupoteza virutubisho vyake ambavyo ni vitamini.
  • Kupika mboga za majani mpaka rangi yake ya kijani kutoweka. Hii pia ni sawa na bure kwani virutubisho vyote muhimu hupotea kadri rangi yake inavyopotea.
  • Kuongeza chumvi katika chakula wakati wa kula. Pia hili ni jambo ambalo tumelizoea lakini ni jambo hatarishi katika afya zetu.
  • Utumiaji holela wa dawa za kutuliza maumivu kama vile paracetamol.
Hivi ni baadhi tu ya vitu tulivyojizoesha kuvifanya! Kama mwana JamiiForums unadhani ni vitu gani vingine ambavyo tumezoea kuvifanya licha ya kuwa hatarishi katika afya zetu!
 
Mchepuko mlevi aahh kuhonga silazimishwi natoa mwenyewe bila ya kuombwa.
 
Kunywa soda barid hasa pepsi au coca unapopata kiu mda wa mchana ni hatar sana kwa afya
 
Back
Top Bottom