Je nichukue hatua gani kuilazimisha halmashauri kutekeleza hukumu iliyotolewa na mahakama?

Mzee wa Twitter

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2023
Posts
1,483
Reaction score
2,392
Wadau Wanasheria naomba msaada wenu juu ya hatua za kuichukulia Halmashauri iliyokataa kutekeleza HUKUMU ya MAHAKAMA KUU ya Mgogoro wa kiwanja.
Baada ya Kushinda Kesi nilimwandikia Mkurugenzi wa Manispaa juu ya Ushindi wa Kesi ya Ardhi na kuambatanisha Nakala ya Hukumu lakini Sikujibiwa hiyo barua na hakuna Utekelezaji wowote uliofanyika mpaka leo.Je Wanasheria ni HATUA zipi natakiwa Kumchukukia huyo MKURUGENZI wa Manispaa ili Atekeleze HUKUMU iliyotolewa?

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
 
ongeza MAELEZO. Eneo ni kiwanja kilichowazi au kinakaliwa na serikali
 
Mgogoro wa hiko kiwanja, ulikiwa wa aina gani? Fafanua
Unaweza kushinda kesi kumbe wenzio wamekwenda mbali zaidi..
Kuna kitu kinaitwa kukazia hukumu...
 
Kazia Hukumu.

Aidha, kwa kuwa umedai kwamba Kesi hiyo ilikuwa inasikilizwa Mahakama Kuu (Divisheni ya Ardhi), ni vyema ukaambatisha na nakala ya Hukumu ya Kesi ili wajuvi waweze kukushauri vizuri. Au taja namba ya Kesi hiyo ili wajuvi waweze kufanya perusal wao wenyewe kwenye mtandao wa Tanzlii au kwenye kumbukumbu za Mahakama.
 
Kama mahakama imeshatoa hukumu we endelea na shughuli zako tu hapo Kiwanjani, waache halmashauri wao ndo watafute msaada wa kisheria
 
Rudi mahakamani ukakazie hukumu.
Pia tafuta wakili akuongoze maana unavyoianika hii ishu hapa unawapa nafasi watesi wako wajipange
 

Mzee wa Twitter haya ukitaka kufanya nenda inbox

Mawakili wa kweli humu wanajulikana, kama hapo juu Matola n.k.
 
Rudi mahakamani ukakazie hukumu.
Pia tafuta wakili akuongoze maana unavyoianika hii ishu hapa unawapa nafasi watesi wako wajipange
Sasa kesi ishaa aamuriwa huko Mahakamani, wwe unataka afichefiche nini sasa!!?? Nyinyi watu wa siri siri ndiyo wapigaji wakubwa! Jambo lazima liwekwe wazi ili wenye uwezo wa kusaidia wasaidie hata kwa mawazo ili mtu apate haki yake! Kuzulumiwa haki yako maumivu yasikie kwa mwenzio, usiombe yakukute,hata kama wwe ni mjuzi wa sheria utalia!!
 
Ulishawahi kuwa na akili?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…