Je, nikimnunulia chupi ya Tsh. 232,602.50/- atazidisha mapenzi?

figganigga

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
25,724
Reaction score
55,906
Salaam Wakuu,

Nina Mwandani wangu nampenda sana. Natamani kuona anakuwa na furaha muda wote na kuniamini. Sasa kuna meseji iliingia kwenye simu yangu bahati mbaya, nikaona amebadilika japo hakutia neno. Nafsi inanisuta sana..

Nikawa natafuta zawadi ya kumnunulia ili iwe kama samahani ya kiutu uzima. Kuna website wanauza mavazi, nikaona chupi nzuri nikaipenda.

Je, nikimnunulia huyo chupi itasuuza moyo wake? Au atasema bora ungenipa hela nijue niifanyie nini. (Akili yangu nahisi ataipeleka VICOBA ikaliwe na Mwenyekiti).

Naomba mawazo yenu

Chupi nilochagua ni hii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…