Masokotz
JF-Expert Member
- Nov 26, 2018
- 3,713
- 6,121
Kuna jambo ambalo ninaliwaza.
Najua kwamba Mheshimiwa Rais anazo nafasi kumi za uteuzi wa wabunge kikatiba.Najua pia kwamba anao uhuru wa kuteu mtu yeyote kwa nafasi hizo bila kuulizwa.Katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wa JPM kuna mambo kadahaa ambayo nimeyaona ambayo kama angekuwa na watu sahihi yangeenda vizuri sana ila kwa sababu amezungukwa na watu ambao wakati mwingi wanamzuga anajikuta anabeba mzigo mkubwa sana katika moyo wake na akili yake
Watu hawa ndio ambao walifanya hata kwa mara ya kwanza mitandao ikazimwa wakati wa uchaguzi na hata tukaonekana kama taifa tumerudi nyuma kidemokrasia na kiusalama.Kiuhalisia kama CCM isingechukua hatua ilizochukua hali yao kisiasa ingekuwa mbaya sana ila hali ya TAIFA ingekuwa mbaya zaidi .
Sasa mimi binafsi nimejikuta nikiwaza kwa kina kwamba kuna mambo yanweza yakafanyika vizuri tu bila kuhitaji nguvu kubwa na badala yake yakahitaji akili tu kwani Kufikiri kumekuwa ni moja kati ya jamo adimu sana kipindi hiki.Kwa sababu hio basi nafikiri ni wakati sasa wa kurudishi desturi ya kufikiri kwa kina na nidhamu ya utekelezaji ila kama taifa tuepuke kurudia makosa ya miaka tano iliyopita.
Swali langu JE inawezekana kutuma maombi kwa Mh.Rais ili katika hizo nafasi chache ateue watu fulani ambao watakuwa kama timu yake ya kufikiri kwa ajili ya kupeleka taifa mbele?Wabunge 10 kama wakiteuliwa kwa umakini wanaweza kuwa chachu kubwa sana ya kupeleka mbele maendeleo ya taifa mbele.
Mimi binafsi nimewaza hivi kwa wale ambao bado wanawaza kuhusu uchaguzi uliopita nashauri turudi shambani tukalime tujipange kwa uchaguzi ujao.Wale wabunge wa upinzani ambao wamekosa nafasi basi ni wakati sasa wa wao kuwa wanaharakati na kufanya kazi karibu na wananchi ili kuhakikisha hata kama hawako katika vyombo vya maamuzi wanaendelea kuwa relevant katika siasa za nchi yetu.Kama kuna rafu zilichezwa basi wajipange kutafuta namna ya kuzishinda na kupata ushindi wa haki.
Siasa ni mchezo ambao kila mtu ana namna ya kuucheza
Najua kwamba Mheshimiwa Rais anazo nafasi kumi za uteuzi wa wabunge kikatiba.Najua pia kwamba anao uhuru wa kuteu mtu yeyote kwa nafasi hizo bila kuulizwa.Katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wa JPM kuna mambo kadahaa ambayo nimeyaona ambayo kama angekuwa na watu sahihi yangeenda vizuri sana ila kwa sababu amezungukwa na watu ambao wakati mwingi wanamzuga anajikuta anabeba mzigo mkubwa sana katika moyo wake na akili yake
Watu hawa ndio ambao walifanya hata kwa mara ya kwanza mitandao ikazimwa wakati wa uchaguzi na hata tukaonekana kama taifa tumerudi nyuma kidemokrasia na kiusalama.Kiuhalisia kama CCM isingechukua hatua ilizochukua hali yao kisiasa ingekuwa mbaya sana ila hali ya TAIFA ingekuwa mbaya zaidi .
Sasa mimi binafsi nimejikuta nikiwaza kwa kina kwamba kuna mambo yanweza yakafanyika vizuri tu bila kuhitaji nguvu kubwa na badala yake yakahitaji akili tu kwani Kufikiri kumekuwa ni moja kati ya jamo adimu sana kipindi hiki.Kwa sababu hio basi nafikiri ni wakati sasa wa kurudishi desturi ya kufikiri kwa kina na nidhamu ya utekelezaji ila kama taifa tuepuke kurudia makosa ya miaka tano iliyopita.
Swali langu JE inawezekana kutuma maombi kwa Mh.Rais ili katika hizo nafasi chache ateue watu fulani ambao watakuwa kama timu yake ya kufikiri kwa ajili ya kupeleka taifa mbele?Wabunge 10 kama wakiteuliwa kwa umakini wanaweza kuwa chachu kubwa sana ya kupeleka mbele maendeleo ya taifa mbele.
Mimi binafsi nimewaza hivi kwa wale ambao bado wanawaza kuhusu uchaguzi uliopita nashauri turudi shambani tukalime tujipange kwa uchaguzi ujao.Wale wabunge wa upinzani ambao wamekosa nafasi basi ni wakati sasa wa wao kuwa wanaharakati na kufanya kazi karibu na wananchi ili kuhakikisha hata kama hawako katika vyombo vya maamuzi wanaendelea kuwa relevant katika siasa za nchi yetu.Kama kuna rafu zilichezwa basi wajipange kutafuta namna ya kuzishinda na kupata ushindi wa haki.
Siasa ni mchezo ambao kila mtu ana namna ya kuucheza