Je, niongezee bidhaa gani kwenye kibanda changu?

bichwa mtoto

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2018
Posts
274
Reaction score
563
Habarini wapendwa katika Mungu, lengo la kuja kwenye jukwaa hili ni kutaka wazo la biashara la kuongezea katika kibanda changu nilichoanza.

Mimi nipo Geita Mjini, mwezi mmoja uliopita nimeanza biashara ya M-Pesa na mtaji usio pungua milioni moja kwa kukodi kibanda ambacho ndipo naendeshea, mambo si haba wateja napata kiasi.

Lengo la kuja hapa nimeona kibanda ni kikubwa naweza endeshea biashara nyingine, kupitia nyie wadau niweke bidhaa zipi ambazo zitasaidia pia mzunguko wa fedha angalau kuongezeka?

Ninawaza machine ya popcorn ingawa sina na uzoefu na biashara hiyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Labda vifaa vya simu, flash etc.
Pia kuwa na computer siku hizi watu wengi wana flat unakua unawaingizia movie, music video etc. Movie moja ni jero.
 
Ushauri wa chichiboy1 ni bora zaidi. Weka pia vitafunwa viburudisho kama pipi na biskuti za aina mbalimbali. Hizo bangi zitakufilisi kwani wateja wako ni pamoja na maafisa usalama. Wamezagaa kila mahali.
 
Kitakuwa kilabu cha pombe sasa
Mkuu hapo kwa hicho kibanda nianvyokiona ongeza double kick,cuca,diamond,banana,sportsman,sm,club na maji ya chupa lakini pia na kandoro na usisahau k-vant,konyagi na valuer za kupima

"baba unahonga hawara elfu kumi,
watoto wanakufa na njaa nyumbani"
 
Mzee kama uko siliasi na iyo biashara usiongeze kitu umo ndan sijui maji sijui biscuit wala soda no usiongeze izo mambo deal na iyo iyo biashara ongeza til no za tigo pesa halo pesa na mitandao mingine biashara ikichangamka tafuta mashine za mabenk kama wakala wa nmb mobile au fahari huduma sijui mashine ya ya kununua luku na mazagazaga mengine ya mtandao na pesa

NB nairudia usiweke maji biscuit sijui soda wala sigara kweny kibanda chako ila choice ni yako tafuta Mia ukose buku
πŸ™
 
Mkuu hapo kwa hicho kibanda nianvyokiona ongeza double kick,cuca,diamond,banana,sportsman,sm,club na maji ya chupa lakini pia na kandoro na usisahau k-vant,konyagi na valuer za kupima
ukiweza hili utakuwa umetoboa, ushauri muruwa kabisa
 
nimekuelewa kwa HERUFI KUBWA
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…