Ndugu wana JF, wiki moja iliyopita EA TV walikuwa na kipindi juu ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu na mada iliyokuwa inajadiliwa ilihusu jinsi gani Umoja wa Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu Tanzania (Tahliso) watakavyopiga kura wakati watakuwa likizo kwa vile watafungua vyuo baada ya uchaguzi mkuu. Walisema ni agizo lililotolewa na serikali likidai ingekuwa gharama kubwa kwa serikali kama vyuo vingefunguliwa kabla ya kupiga kura.
Walisema kwa vile ratiba ya vyuo huwa inatolewa muda mrefu, mamlaka husika zingeweza kuweka utaratibu mzuri ili wanavyuo hao wajiandikishe kwenye vituo vyao wakiwa likizo au vyuoni. Walidai pia kuwa utaratibu uliowekwa mwaka huu unaonesha una lengo la kuwanyima hao wanavyuo haki yao ya kupiga kura. Pamoja na hayo, walikuwa na matumaini kuwa Waziri Mkuu atawasikiliza na kuwaeleza namna gani watakavyoshiriki uchaguzi mkuu wakiwa likizo. Je, kuna mwenye taarifa nzuri kuhusu hili: yaani, kama Waziri Mkuu amewajibu na ni kitu gani kinaendelea?
Walisema kwa vile ratiba ya vyuo huwa inatolewa muda mrefu, mamlaka husika zingeweza kuweka utaratibu mzuri ili wanavyuo hao wajiandikishe kwenye vituo vyao wakiwa likizo au vyuoni. Walidai pia kuwa utaratibu uliowekwa mwaka huu unaonesha una lengo la kuwanyima hao wanavyuo haki yao ya kupiga kura. Pamoja na hayo, walikuwa na matumaini kuwa Waziri Mkuu atawasikiliza na kuwaeleza namna gani watakavyoshiriki uchaguzi mkuu wakiwa likizo. Je, kuna mwenye taarifa nzuri kuhusu hili: yaani, kama Waziri Mkuu amewajibu na ni kitu gani kinaendelea?