engmtolera
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 5,149
- 1,441
Wadau
nimejikuta naumiza kichwa kila ninaposikia matatizo ya Ardhi na mapigano kati ya wakulima na wafanyakazi yanayotokea hivi sasa Tanzania,nikajiuliza ktk hii Rasimu ya pili ya Katiba ina ongelea serikali 3 tu pekee yake?
Nikiangalia Rasimu ya pili ya katiba ktk SURA YA PILI.MALENGO MUHIMU, MISINGI YA MWELEKEO WA SHUGHULI ZA SERIKALI NA SERA ZA KITAIFA kinasema
(v) kuweka mazingira bora kwa ajili ya kukuza kilimo, ufugaji na uvuvi kwa kuhakikisha kuwa wakulima, wafugaji na wavuvi wanakuwa na ardhi na nyenzo kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao;
ktk hiki kipengere,hakisemi wazi ni aina ipi ya ardhi itatengwa kwa ajili ya wakulima,wafugaji,ugomvi wa sasa ni kwamba wakulima wanalalamika kuwa wafugaji wanalisha mifugo yao ktk mashamba ya wakulima na tunaelewa madhara ya mifugo kama itapita kwa muda mrefu ktk ardhi ambayo inafaa kwa kilimo,kwanini wanasiasa wanaopigia kelele serikali tatu wasijikite pia ktk kutafuta dawa ya haya matatizo ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji?
Lakini pia ktk hiki kipengere kinachohusu Haki za makundi madogo katika jamii.
(c) kutengewa maeneo ya ardhi ambayo kwa desturi makundi hayo huitumia kama eneo la kuishi na kupata riziki ya chakula.
ktk hiki kipengele tunaona kuwa makundi hayo madogo ya kijamii hayajatajwa kwa majina ni makundi yapi hayo,je wakulima na wafugaji wamo ktk hilo kundi?
kiujumla rasimu hii haijataja njia mbadala itakayotumika ktk kutatua matatizo ya ardhi yanayojitokeza sasa hususani haya makundi mawili ya wakulima na wafugaji.Ni vyema wanasiasa wakaelewa kuwa serikali tatu ama mbili ama moja haitakuwa na maana kama tu mapigano ya wakulima na wafugaji hayatapatiwa ufumbuzi wa kudumu.kwani 80% ya watanzania ni wakulima na hawa hawana habari ya serikali tatu ama 2 ama 1,wao wanachokiangalia zaidi ni uwepo wa ardhi yenye rutuba itakayowasaidia wao kuweza kulima na kujipatia chakula chao cha kila siku na wafugaji pia wangependa wawe na maeneo yao rasmi yatakayowawezesha kufuga na kulisha mifugo yao pasi ya kuingilia maeneo ambayo ni mazuri kwa kilimo ama kutumia mashamba ya wakulima kama ndio maeneo ya marisho ya mifugo yao.
Kutokana na matatizo yaliyopo sasa juu ya wakulima na wafugaji ni vyema rasimu hii ikasema wazi juu ya maeneo yapi hayataruhusiwa kwa kilimo na maeneo yapi hayataruhusiwa kwa ufugaji,maeneo yapi ni kwa ajili ya wakulima na maeneo yapi ni kwa ajili ya wafugaji.
nimejikuta naumiza kichwa kila ninaposikia matatizo ya Ardhi na mapigano kati ya wakulima na wafanyakazi yanayotokea hivi sasa Tanzania,nikajiuliza ktk hii Rasimu ya pili ya Katiba ina ongelea serikali 3 tu pekee yake?
Nikiangalia Rasimu ya pili ya katiba ktk SURA YA PILI.MALENGO MUHIMU, MISINGI YA MWELEKEO WA SHUGHULI ZA SERIKALI NA SERA ZA KITAIFA kinasema
(v) kuweka mazingira bora kwa ajili ya kukuza kilimo, ufugaji na uvuvi kwa kuhakikisha kuwa wakulima, wafugaji na wavuvi wanakuwa na ardhi na nyenzo kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao;
ktk hiki kipengere,hakisemi wazi ni aina ipi ya ardhi itatengwa kwa ajili ya wakulima,wafugaji,ugomvi wa sasa ni kwamba wakulima wanalalamika kuwa wafugaji wanalisha mifugo yao ktk mashamba ya wakulima na tunaelewa madhara ya mifugo kama itapita kwa muda mrefu ktk ardhi ambayo inafaa kwa kilimo,kwanini wanasiasa wanaopigia kelele serikali tatu wasijikite pia ktk kutafuta dawa ya haya matatizo ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji?
Lakini pia ktk hiki kipengere kinachohusu Haki za makundi madogo katika jamii.
(c) kutengewa maeneo ya ardhi ambayo kwa desturi makundi hayo huitumia kama eneo la kuishi na kupata riziki ya chakula.
ktk hiki kipengele tunaona kuwa makundi hayo madogo ya kijamii hayajatajwa kwa majina ni makundi yapi hayo,je wakulima na wafugaji wamo ktk hilo kundi?
kiujumla rasimu hii haijataja njia mbadala itakayotumika ktk kutatua matatizo ya ardhi yanayojitokeza sasa hususani haya makundi mawili ya wakulima na wafugaji.Ni vyema wanasiasa wakaelewa kuwa serikali tatu ama mbili ama moja haitakuwa na maana kama tu mapigano ya wakulima na wafugaji hayatapatiwa ufumbuzi wa kudumu.kwani 80% ya watanzania ni wakulima na hawa hawana habari ya serikali tatu ama 2 ama 1,wao wanachokiangalia zaidi ni uwepo wa ardhi yenye rutuba itakayowasaidia wao kuweza kulima na kujipatia chakula chao cha kila siku na wafugaji pia wangependa wawe na maeneo yao rasmi yatakayowawezesha kufuga na kulisha mifugo yao pasi ya kuingilia maeneo ambayo ni mazuri kwa kilimo ama kutumia mashamba ya wakulima kama ndio maeneo ya marisho ya mifugo yao.
Kutokana na matatizo yaliyopo sasa juu ya wakulima na wafugaji ni vyema rasimu hii ikasema wazi juu ya maeneo yapi hayataruhusiwa kwa kilimo na maeneo yapi hayataruhusiwa kwa ufugaji,maeneo yapi ni kwa ajili ya wakulima na maeneo yapi ni kwa ajili ya wafugaji.