Je roho za mwanadamu na wanyama huweza kuwa na ufahamiano?

Crocodiletooth

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2012
Posts
20,561
Reaction score
24,428
Mbwa huyu kwa jina la Bryan amekuwa na matendo ya kustaajabisha huko uingereza toka waliokuwa wanafamilia wenza kufariki kwa ajali amekuwa akifika kwenye kaburi kwa miaka miwili mfululizo bila kuchoka na kupumzuka hapo kwa nusu saa na kuondoka zake, je katika ulimwengu wa Kiroho huwa tuna mahusiano ya aina fulani.
 
Why?, soul, roho, sio moyo namaanisha pumzi isababishayo uai kwa viumbe hai, tusichanganye na Uwezo wa kiakili, kwani ni vitu tofauti, roho hukupa uhai tu, functions zingine hufanya kazi independently! It's could be roho haina akili bali ndio uhai wenyewe.
Kiranga tafadhali njoo utoe mawili matatu hapa.
 


Kuna mahusiano kati ya kaburi na roho ya mwili uliozikwa kwenye kaburi husika, yaani mtu akifa na akazikwa halafu watu wawe wakizuru kaburi lake basi roho yake huko ilipokuwa huwa ikihisi ujio wa watu hapo kaburini, kwa maana hiyo hizo roho za hao waliokufa huhusi ujio wa huyo mbwa hapo kaburini lakini kama mbwa naye anahisi chochote kutoka kwa hizo roho hilo ni jambo jingine linalohitaji elimu pana ya mambo ya roho.

Mtazamo wangu; Yawezekana kipindi miili hiyo ikizikwa huyo mbwa naye alikuwepo kwenye mazishi na alihisi/alinusa harufu za hao wapendwa wake wakati wakizikwa na hivyo kuweka akilini kumbukumbu kwamba "jamaa" zake (its family members) wamefukiwa hapo hivyo hali ya upweke kuwakosa "jamaa" zake waliozoeana ndio inayomsukuma aje hapo kwani "aliona" kupitia harufu hao "jamaa" zake wakizikwa/wakifukiwa hapo.
 
Ila sio hawa mbwa wa kwetu tunaowapa ugali mara Moja Kwa siku
 
Roho ya ng'ombe na ya mwanadamu ziko sawa?
Hapa ndipo penye maswali, kwa fikra zangu "roho / soul /pumzi, miongoni mwa viumbe hai ni moja. Hakuna kiumbe hai chochote kitakachokuwa kinacheka wakati roho yake ikitoka. Suffocation ya binadamu ngombe na kiumbe chochote ni moja. Utofauti huwa ni kwamba roho hii iliingia kwa ngombe na roho hii iliingia kwa mwanadamu, ambapo viumbe hawa tofauti zao huwa ni majaliwa ya kiakili.
 
Mhu 3:19‭-‬21

Kwa maana linalowatukia wanadamu linawatukia wanyama; jambo moja lawatukia;

anavyokufa huyu ndivyo anavyokufa huyu; naam, wote wanayo pumzi moja;

wala mwanadamu hana kitu cha kumpita mnyama;

kwa maana yote ni ubatili.

Wote huendea mahali pamoja;
wote hutoka katika mavumbi; na hata mavumbini hurudi tena.

Ni nani ajuaye kama roho ya binadamu huenda juu, na kama roho ya mnyama huenda chini?
 
Huko kwa wenzetu shughuri za maziko huhusisha watu wachache sana hasa wanafamilia, ndugu baadhi na marafiki.
Yawezekana huyo mbwa nae alishuhudia hilo tendo pasipo kubughudhiwa na pengine alipewa wasaa wa kutazama nyuso za marehemu waliozikwa kwenye hilo kaburi make treatments za wenzetu wazungu kwa mifugo walofuga na kuishi nayo kwa miaka mingi ni kama sehemu ya familia kabisa!

Kwahiyo ni rahisi sana kwa mbwa huyo kuwakumbuka wapendwa wake na nikawaida kudhulu kwenye hayo makaburi kutokana na vile aliishi nao kirafiki na pia harufu zao bado ana sense akifika hapo kaburini. Yawezekana kabisa kinachomfanya afike hapo anachukulia pengine wapendwa wake wamelala tu ipo siku ataungana nao tena maishani.
 
Ngoja nifungue biblia.
 
 
Umesahau kua binadamu ni mnyama anayeharibu dunia.......
 
Umesahau kua binadamu ni mnyama anayeharibu dunia.......
Kabisa mkuu, ingekuwaje endapo dunia ingebaki na uasili wake bila majengo yaani dunia ikiwa na misitu mito vijito N. K
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…