Ashasembeko
JF-Expert Member
- Dec 14, 2017
- 225
- 910
Jarida la The African Intelligence liliripoti wiki iliyopita kuwa Rais mstaafu Jakaya Kikwete ndio mshauri mkuu asiye rasmi wa Rais Samia na anatumia ushawishi wake kusukuma agenda za uongozi wake zilizopigwa chini na Magufuli kama mradi wa Bagamoyo.
Jarida lengine la the Africa Report liligusia habari hii na kujaribu kuchambua kama Rais Samia ni Rais au kivuli cha Rais mstaafu Kikwete. Jaridi hili limetumia vyanzo vyao vya siri ambao vimewaeleza kuwa Kikwete amekua na ushawishi kwa Samia hususani kwenye maswala ya jumuiya ya kimataifa na Covid-19.
The Economist Intelligence Unit pia hivi karibuni liliripoti kuwa kuna watu ndani ya CCM, na baadhi ya vyombo vya usalama ndivyo vinaongoza nchi na Samia ni kama Rais mbele za watu, ila hana nguvu ya kufanya maamuzi yenye "substance".
Jana CNN walicover story ya Mbowe kupewa kesi ya Ugaidi. Mmoja wa wachambuzi (ambae alikuwa mmoja ya watu wa mwanzoni kabisa kutoa taarifa ya Magufuli kuumwa) alitabainisha mambo mawili.
1. Yaweza kuwa Samia ni kweli kabadilika na anataka kuonyesha nguvu yake kama Rais kwa kutumia mbinu za kidikteta za Magufuli.
2. Yawezekana watiifu wa serikali ya Magufuli wamegomea mabadiliko Samia anayotaka kufanya na wanapush back. Akasema Samia anaweza kuwa ameshindwa kucontrol serikali yake na viemelea vya serikali ya JPM kwenye usalama, chama na jeshi vinaendesha nchi.
Kuna baadhi ya viongozi kama Zitto Kabqe na Fatma Karume walishaanza kuona dalili za Rais kuendeshwa toka mwanzoni.
Soma hii habari
ke.opera.news
Hizi tuhuma zinafikirisha sana. Je nani anaendesha nchi? Tuna Rais kivuli? Kama ni kweli Samia anakubalije jina lake lichafuliwe? Kama ni kweli maamuzi hafanyi yy kwanini asiachie ngazi?
Tusubiri tuone tunaelekea wapi.
Sent from my SM-G975U using JamiiForums mobile app
Jarida lengine la the Africa Report liligusia habari hii na kujaribu kuchambua kama Rais Samia ni Rais au kivuli cha Rais mstaafu Kikwete. Jaridi hili limetumia vyanzo vyao vya siri ambao vimewaeleza kuwa Kikwete amekua na ushawishi kwa Samia hususani kwenye maswala ya jumuiya ya kimataifa na Covid-19.
The Economist Intelligence Unit pia hivi karibuni liliripoti kuwa kuna watu ndani ya CCM, na baadhi ya vyombo vya usalama ndivyo vinaongoza nchi na Samia ni kama Rais mbele za watu, ila hana nguvu ya kufanya maamuzi yenye "substance".
Jana CNN walicover story ya Mbowe kupewa kesi ya Ugaidi. Mmoja wa wachambuzi (ambae alikuwa mmoja ya watu wa mwanzoni kabisa kutoa taarifa ya Magufuli kuumwa) alitabainisha mambo mawili.
1. Yaweza kuwa Samia ni kweli kabadilika na anataka kuonyesha nguvu yake kama Rais kwa kutumia mbinu za kidikteta za Magufuli.
2. Yawezekana watiifu wa serikali ya Magufuli wamegomea mabadiliko Samia anayotaka kufanya na wanapush back. Akasema Samia anaweza kuwa ameshindwa kucontrol serikali yake na viemelea vya serikali ya JPM kwenye usalama, chama na jeshi vinaendesha nchi.
Kuna baadhi ya viongozi kama Zitto Kabqe na Fatma Karume walishaanza kuona dalili za Rais kuendeshwa toka mwanzoni.
Soma hii habari
Opera News - Neuesten Nachrichten In Germany-German | Aktuelle Nachrichten
Neuesten Germany-German Nachrichten auf OperaNewsApp.com bekommen: Aktuelle Nachrichten und Videos in Germany-German , Fußballnachrichten, Politik, Sport, Unterhaltung, Technik, Handel.
Hizi tuhuma zinafikirisha sana. Je nani anaendesha nchi? Tuna Rais kivuli? Kama ni kweli Samia anakubalije jina lake lichafuliwe? Kama ni kweli maamuzi hafanyi yy kwanini asiachie ngazi?
Tusubiri tuone tunaelekea wapi.
Sent from my SM-G975U using JamiiForums mobile app